Friday, November 27, 2015

KAMANDA MPINGA AZINDUA OPARESHENI YA PAZA SAUTI DAR


Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani,DCP Mohamed Mpinga, akisalimiana na Mabalozi wa Usalama Barabarani, muda mfupi kabla ya kuzindua Operesheni ijulikanayo kwa jina la “Paza Sauti” yenye lengo la kuwaelimisha abiria ili waweze kutoa taarifa mara wanapoona kuna viashiria vya uvunjifu wa sheria za barabarani. Operesheni hii ilizinduliwa jijini Dar es Salaam leo.


TANZIA:MKURUGENZI MSAIDIZI WA BUNGE HELLEN MBEBA AMEFARIKI DUNIA

Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah, anasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wa Bunge, Bi. Hellen Stephen Mbeba (36)(Pichani kulia), aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi-Shughuli za Bunge, kilichotokea ghafla leo Ijumaa tarehe 27/11/2015 wakati akipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu.

Msiba upo nyumbani kwake eneo la Kisasa, Mjini Dodoma. Taarifa zaidi na taratibu nyingine ikiwa ni pamoja na ratiba kamili ya maziko zitaendelea kutolewa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya Marehemu pindi mipango itakapokamilika.

MUNGU AIWEKE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI AMEN

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
Ofisi ya Bunge
Dar es Salaam
27.11.2015

MAHAKAMA TANZANIA BEGA KWA BEGA NA WAANDISHI WA HABARI

Jaji kiongozi wa Mahakama kuu ya Tanzania Shaaban Lila amesema kuwa majaji wa Tanzania wanabusara katika kufanya maamuzi yao na ndio maana hata vyombo vya habari nchini hata vinapowachafua hawaangaiki kufikisha kwenye vyombo vya dola.

 Jaji kiongozi huyo amesema hayo leo wakati wa kufunga mafunzo ya siku mbili  kwa waandishi wanao ripoti habari za mahakamani yaliyokuwa na lengo la kuwajengea uwezo zaidi wa kuripoti habari za mahakama.


WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSTUKIZA BANDARINI,ATOA AMRI YA KUKAMATWA KWA MAAFISA TRA


Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi maofisa watano na watumishi watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania(TRA)kutokana na upotevu wa makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya sh.bilioni 80.

Akizungumza na viongozi wa mamlaka ya Bandari pamoja na viongozi wa TRA,katika ziara ya kushtukiza leo,Waziri Mkuu amewataka Kamishna Mkuu wa TRA,Rished Bade na Naibu Kamishna Mkuu wa TRA,Lusekelo Mwasena,wahakikishe wanashirikiana na polisi kufuatilia upotevu huo na na kwamba fesha hizo zinapatikana na zinarudi Serikalini.

Akitangaza uamuzi huo baada ya kufanya kikao na viongozi wa Serikali bandarini hapo,Waziri Mkuu aliwataja waliosimamishwa kazi kuwa ni Kamishna wa forodha,Tiagi Masamaki na mkuu wa kituo cha huduma kwa wateja, Habibu Mponezya.


“IGP,Ninaagiza watu hawa wakamatwe na kuisaidia polisi,hati zao za kusafiria zikamatwe na mali zao zikaguliwe kama zinaendana na utumishi wa umma,”alisema Waziri Mkuu.

Watumishi wengine waliosimamishwa kazi ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA,Haruni Mpande,Hamisi Ali Omari(hakutaja anatoka kitengo gani)pamoja na mkuu wa kitengo cha Bandari Kavu (ICD In –Charge),Eliachi Mrema na alitaka wawe chini ya polisi lpaka uchunguzi utakapokamilika.

Thursday, November 26, 2015

RIPOTI YA RUSHWA BARANI AFRIKA KUZINDULIWA, TANZANIA PIA IPO

Transparancy International, inategemea kuchapisha utafiti unaoangalia maoni ya watu uzoefu na mtazamo wao kuhusu masuala ya rushwa katika nchi 28 barani Afrika.

Maandalizi ya ripoti hiyo iitwayo People and Corruption, Africa Survey 2015 Global Corruption Barometer Transparency International imeungana na Afrobarometer, walioongea na watu wasiopungua 43,143, katika nchi 28 katika nchi zilizoko pembezoni mwa jangwa la Sahara.

Kwa mujibu wa African Press Organisation, shirika la Transparency International litachapisha utafiti huo tarehe 1/12/2015, unafuatia ule uliopita uliojulikana kama Global Curruption Barometer, uliochapishwa mwaka 2013

BREAKING NEWS: KADI ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA MARUFUKU




MEGATRADE YAVIPIGA JEKI CHUO KIKUU NA CHAMA CHA SOKA KILIMANJARO.


Meneja masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha,Edmund Rutaraka akimkabidhi hundi ya kiasi cha shilingi Milioni 1.5 ,katibu wa Chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro ,KRFA,Mohamed Musa kwa ajili ya kusadia ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa iliyoanza hivi karibuni.

UZINDUZI WA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA MANYARA, ARUSHA,K'NJARO



Brass Band ya Chuo cha Polisi Moshi ikiongoza maandamano ya uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini .


BRAND NEW RELEASE: BERRY BLACK FT. ALICE&DIGNA - MTUWACHE (VIDEO)






Wednesday, November 25, 2015

BINTI ALIYEJIUNGA ISIS APIGWA MPAKA KUFA ALIPOJARIBU KUTOROKA

Samra Kesinovic, 17, pichani kushoto aliondoka Austria mnamo 2014 mwezi aprili akiwa na rafiki yake Sabrina Selimovic, imedaiwa amepigwa na magaidi wa kundi la magaidi wa Kiislam wa ISIS mpaka kupoteza maisha wakati alipojaribu kutoroka eneo la Raqqa.

Inaaminika kuwa Sabina alifariki mwezi disemba mwaka jana wakati wa kipindi cha mapigano makali. Wasichana hao wawili walionekana katika video ya propaganda za ISIS mda mfupi baada ya kuwasili nchini Syria. Rafiki yake ambaye waliambatana aliuwawa miezi michache kabla yake.

Samra Kesinovic na rafiki yake Sabina Selimovic(kulia) wakiwa katika picha iliyopigwa na kundi la magaidi wa ISIS mda mfupi baada ya kuwasili nchini Syria mwezi aprili 2014.


FAMILIA YA MTOTO ALIYESINGIZIWA KUBEBA BOMU YADAI BILIONI 32

Familia ya mtoto wa Kiislamu aliyekamatwa baada ya kubuni na kutengeneza saa yake na kuipeleka shuleni kisha kudahiniwa kuwa amebeba bomu, wanadai fidia ya dola milioni 15(sawa na takribani shilingi bilioni 32 za Kitanzania)

Familia ya Ahmed Mohamed pia wanadai kuombwa radhi na jiji la Irving pamoja na shule baada ya kijana huyo wa miaka 14 kukamatwa na polisi mwezi wa tisa mwaka huu.

Kwa mujibu wa gazeti la NY Daily, mwanasheria anayewakilisha familia hiyo alituma barua katika jiji la Irving, lililoko mashariki mwa Dallas pamoja na shule ya Wilaya ya Irving Independent School nchini Marekani, akielezea kuwa mwanafunzi huyo wa darasa la tisa alisingiziwa na kukamatwa kisha kuwekwa rumande na kuhojiwa bila wazazi uwepo wa wake.

Familia ya Mohamed inalidai jiji dola za Marekani milioni 10 (sawa na takribani shilingi za Tanzania bilioni 21) pamoja na shule ya wilaya hiyo dola milioni 5(sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 11) lasivyo watafungua kesi ndani siku 60, barua hiyo ilieleza.

BOFYA KUONA KAZI YA MTOTO HUYO. . .


MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI KUFANYIKA SINGIDA


Maambukizi ya ukimwi yameongezeka kwenye kundi la vijana wenye umri wa miaka kati ya 19 mpaka 24 tofauti na ilivyokuwa miaka minne iliyopita, ambako kundi lililokuwa limeathiriwa zaidi lilikuwa miaka kati ya 25 mpaka 34, imeelezwa pia licha ya kwamba kiwango cha maambukizi mapya ya virusi hivyo nchini kimeshuka kutoka asilimia 7 mwaka 2004 mpaka kufikia asilimia 5.3 mwaka huu, takwimu za baadhi ya mikoa ikiwemo Singida, Kigoma,Arusha, Mtwara, Kilimanjaro na Kagera zimeonekana kuongezeka.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids) kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani kwa mwaka huu, Dk.Fatma Mrisho(pichani juu), alisema kazi kwa ujumla kazi kubwa imefanyika.


Tuesday, November 24, 2015

MAKAMU WA RAIS ATETA NA MTANDAO WA WANAWAKE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na uongozi wa Mtandao wa Wanawake na Katiba Tanzania (WFT) ambapo amezungumzia dhamira ya serikali katika kuyatafutia ufumbuzi matatizo mbali mbali yanayowakabili wanawake na watoto wa kike nchini.

Katika mazungumzo hayo Makamu wa Rais aliueleza ujumbe huo kuwa wakati wa kampeni aliahidi pamoja na kazi za kumsaidia Mhe. Rais bado kama mama atafuatilia kwa karibu utekelezaji wa ahadi ya kupatikana kwa maji safi na salama, kuboresha afya ya mama na mtoto, elimu na mazingira.

“Nilipokuwa kwenye kampeni nimejionea shida ya maji na wanawake ndiyo wanaopata tabu ya kutembea mwendo mrefu kutafuta maji. Kwa hiyo, pamoja na kazi zangu za kumsaidia Mhe. Rais nitasimamia miradi yote ya maji, alau tuhakikishe maji yanapatikana umbali wa mita 400 kutoka eneo wananchi wanakoishi au karibu zaidi”.


RC KILIMANJARO AKUTANA NA MAOFISA WA MANISPAA KUJADILI HOFU YA KIPINDUPINDU



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Amosi Makala akiwa katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi,kuzingumza na watendaji wa Afya na Mazingira.

MBUNGE WA CHUMBUNI APOKELEA NA WAPIKA KURA KWA SHANGWE AKITOKEA DODOMA




Mhe Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza AMJAD akipongezwa na Mke wakati alipofika kumpokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitokea Dodoma kuhudhuria hafla ya kuapishwa wiki iliopita.

Monday, November 23, 2015

BREAKING NEWS:SHEREHE ZA UHURU KUTOFANYIKA MWAKA HUU



“Rais Dr. John Pombe Magufuli ameamuru kuwa siku ya Uhuru yaani 9 December hakutakuwa na shamra shamra zozote watu wote watafanya usafi wa mazingira ili kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu kwa maana hiyo hakutakuwa na sherehe za magwaride katika uwanja wa Uhuru kama ilivyozoeleka” amesema Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue alipofanya ziara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

BIMA YA AFYA NHIF YAKANUSHA KUDAIWA NA HOSPITAL YA RUFAA MBEYA


Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini umekanusha kuwepo kwa madai yaliyotolewa na Hospital ya Rufaa Mkoani Mbeya kuwa wanaudai Mfuko jumla ya shilingi bilioni 2 na kwamba wanaudai Mfuko kutoka mwezi Juni, 2015.

Akizungumza jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Ndugu Michael Mhando amesema madai yaliyotolewa na Hospital hiyo ya Rufaa Mkoa wa Mbeya hayana ukweli wowote nakwamba mfuko huo unalipa madai baada ya mtoa huduma kuwasilisha kwenye Mfuko.

STANDARD CHARTERED BANK YAPATA MKURUGENZI WA KWANZA MTANZANIA

SANJAY RUGANI  
MKURUGENZI MKUU
STANDARD CHARTERED BANK TANZANIA 



WAKENYA WAJIANDAA KUMPOKEA PAPA FRANCIS, ULINZI KUIMARISHWA

Serikali ya Kenya imesema maandalizi ya kumlaki Papa Francis nchini Kenya yamekamilika na ziara yake inatarajiwa kuwa ya kufana.

Kwenye kikao na wanahabari, Msemaji wa Ikulu Manoah Esipisu na Inspekta Mkuu wa Polisi Joseph Boinnet walisema hatua madhubuti zimechukuliwa kumpokea kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani.

“Hili ni tukio muhimu sana, nchi yetu inamkaribisha Papa Francis kwa mara ya kwanza barani Afrika, na ningependa kusema kwamba tuko tayari kumpokea pamoja na msafara wake, usalama umeimarishwa tukiangazia kuanzia kuasili kwake, njia atakazotumia na pia kwa wageni wote watakaomiminika jijini hapa,” alisema Bw Boinnet.

JAMAA ALIYEBADILI JINSIA AJIUA, KISA KAHUKUMIWA KWENDA JELA YA WANAUME

Mwanaume aliyebadili jinsia na kuwa mwanamke aliyetishia kujiua iwapo angepelekwa jela ya wanaume, amekutwa amekufa. Vicky Thompson (PICHANI KULIA), mwenye umbra wa miaka 21, alihukumiwa kifungo cha miezi 12 katika jela ya HMP Leeds baada ya kuvunja makubaliano ya hukumu aliyopewa awali.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mirror la niching Uingereza, Mwanasheria wa Vicky, Mohammed Hussain alimweleza hakimu kuwa Vicky ni mwanamke na kumtaka ampeleke kutumikia kifungo chake katika mahakama ya New Hall kitengo cha wanawake, karibu na Wakefield.


ARUSHA SASA KUFURAHIA INTANETI YA KASI ZAIDI KUTOKA TIGO

Arusha, Novemba 18 2015. Wateja wa Tigo waishio Arusha sasa wanaweza kupata mtandao wa intaneti wenye kasi kubwa zaidi kufuatia upanuzi wa upatikanaji wa huduma ya 4G LTE hadi kufikia jiji hilo lilopo kaskazini mwa Tanzania Teknolojia ya 4G LTE ina kasi mara tano zaidi kuliko teknolojia ya 3G inayopatikana nchini kwa sasa.

‘’Upanuzi huu umetokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika majaribio ya awali ya utoaji huduma ya 4G jijini Dar es Salaam kuanzia mapema mwaka huu’’, amesema Mkuu wa Kitengo cha Internet David Zacharia.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Zacharia amesema: "ni kielelezo cha jinsi ambavyo Tigo imedhamiria kufanikisha kuleta mabadiliko ya dijitali katika maisha ya watanzania na pia kuwa katika msitari wa mbele wa kutumia teknolojia ya kisasa na kibunifu nchini Tanzania."


MILEY CYRUS KAZIDISHA. . ., AMNYONYA DANCER WAKE MATITI JUKWAANI (ANGALIA PICHA)











Tunajua kichaa chake, usiku wa alhamisi iliyopita, Miley Cyrus (KUSHOTO PICHANI) alifanya kituko ambacho hakijawahi kutokea akiwa jukwaani, wakati akifanya onesho la kukata na shoka jijini Chicago.

Aliingia jukwaani katika ukumbi wa Rivera akiwa amevalia vazi la aibu mno ambalo linaonesha maungo yake na uume wa bandia. 

Lakini kama haitoshi alimnyonya mcheza sho wake maziwa akiwa jukwaani. . . 

Bofya uangalie picha chini. . .


KANDA YA KASKAZINI WAZINDUA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA



Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili kanda ya Kaskazini na Meneja Miradi wa Shirika lisilo la kiserikali la NAFGEM,Honorata Nasuwa akizungumza na wanahabari(hawako pichani ) juu ya uzinduzi huo,kushoto kwake ni Afisa Ushawishi na utetezi (KWIECO) na mratibu wa maadhimisho hayo kanda,Hilary Tesha.

Sunday, November 22, 2015

PANONE FC YASONGA MBELE LIGI YA SHIRIKISHO YA AZAM,YAIFUNGA POLISI 2 - 1.


Wachezaji wa timu ya soka ya Panone fc wakipasha misuli moto kabla ya kuanza kwa mchezo wa ligi ya shirikisho inayodhaminiwana Azam.


Friday, November 20, 2015

BREAKING NEWS: MAGUFULI AHAMISHIA MIL 235 ZA SHEREHE YA WABUNGE KUNUNUA VITANDA MUHIMBILI (VIDEO)

RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI AMEMUAMBIA SPIKA WA BUNGE AHAMISHIE SHILINGI ZAIDI YA MILIONI 235 ZILIZOTOEWA NA WAFADHILI KWAAJILI YA SHEREHE YA KUFUNGUA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA KWAAJILI YA KUNUNUA VITANDA KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI. . . ANGALIA VIDEO CHINI 

VIDEO HII NI KWA HISANI YA MUHIDINI MICHUZI

Baada ya kulihutubia na kulizindua bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt JOHN POMBE MAGUFULI amehudhuria hafla fupi iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma na kuagiza fedha zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla hiyo zipelekwe Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kununulia vitanda vya wagonjwa.

HOTUBA YA RAIS MAGUFULI HAPA WAKATI AKIFUNGUA BUNGE JIJINI DODOMA

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, AKIFUNGUA RASMI BUNGE JIPYA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA,
20 NOVEMBA 2015


Mheshimiwa Spika;
Niko hapa leo kutimiza matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 91 Ibara ndogo ya kwanza inayonitaka kulihutubia na kulifungua rasmi Bunge hili. Naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya njema, na kutuwezesha kuwepo hapa siku ya leo. Aidha nitumie fursa hii kuwakumbuka wenzetu ambao, kwa namna na nafasi mbalimbali, walishiriki katika mchakato wa uchaguzi huu na kwa bahati mbaya walipoteza maisha yao kabla ya mchakato haujakamilika. Kwa hao wote waliotangulia mbele za haki ninamuomba Mwenyezi Mungu azirehemu roho zao na awape pumziko la amani. Nitumie nafasi hii kuwapa pole ndugu na jamaa ambao ndugu zao walifariki na wengine kupata ulemavu wakati wa mchakato wa uchaguzi huu.


SASA UNAWEZA ANGALIA TELEVISION KWA SIMU ZA MKONONI

Dar es Salaam, Tanzania 19 Novemba 2015, kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua huduma ya ziada itakayowawezesha wateja wake nchi nzima kuangalia vipindi vya televisheni katika vituo vya ndani na nje ya nchi kupitia simu zao za mkononi.

Huduma hii mpya ijulikanayo kama "Airtel TV" imeunganishwa na vituo 8 vya televisheni vya ndani na nje ya nchi na kuwawezesha wateja wa Airtel kuangalia vipindi vilivyopita katika tamsilia wanazozipenda, kuangalia sinema na video wanazohitaji kupitia simu zao.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa "Airtel TV" Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw Jackson Mmbando (PICHANI JUU)alisema "kwa kawaida mara nyingi watanzania wanaangalia vipindi vya televisheni wakiwa nyumbani wakati wa jioni baada ya kutoka katika kazi zao.

PONGEZI ZAMIMINIKA KUTOKA KWA MARAIS DUNIANI AKIWEMO MUGABE



ANGALIA ZAIDI. . .


BUSU LA SINEMA MPYA YA JAMES BOND LAZUA UTATA NCHINI INDIA

Bodi ya Filamu nchini India imeficha baadhi ya vipande vya filamu mpya ya James Bond “007” ijulikanayo kama “SPECTRE” vinavyoonesha akipiga mabusu, hatua hiyo ni kuendana na maadili na kulinda tamaduni na mila za nchi hiyo.

Kwa mujibu wa shirika la habari la CNN, Kiongozi wa Bodi hiyo, Pahlaj Nihalani ameliambia shirika la habari kuwa wamepunguza sehemu mbili zinazoonesha Daniel Craig(007) akimbusu Monica Bellucci pamoja na Lea Seydoux

“Kazi yetu ni kuziba maeneo yasiyofaa kutokana na daraja la sinema, kwa hiyo tumetekeleza hilo” Nihalani aliiambia AFP. Matusi mawili pia yameondolewa.

Thursday, November 19, 2015

ISIS YATOA PICHA YA BOMU LILILOLIPUA NDEGE YA URUSI NA KUUA ABIRIA 224

Kundi la kigaidi la Kiislam, maarufu kama ISIS limetoa picha ya bomu na kudai ndilo lililotumika kulipua ndege ya Urusi katika anga ya Misri eneo la rasi ya Sinai mwezi uliopita na kuua abiria 224 waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.

Picha hiyo (KULIA) ilichapishwa katika jarida lenye msimamo mkali la kiingereza likionesha neno “EXCLUSIVE - picha ya IED iliyotumika kushusha ndege ya shirika la Urusi” 

Picha hiyo ilionesha kikopo cha kinywaji cha soda aina ya Schweppes Gold na kuambatanishwa na vitu ambayvo ni sehemu ya vilipuzi.

Taarifa hiyo iliandika “ Tarehe 30, Septemba, 2015, baada ya kuunga mkono Nusayrī tāghūt kwa miaka mingi katika vita dhidi ya Uislamu wa Shām, Urusi imeamua kushiriki moja kwa moja kwa kutumia ndege zao katika vita hiyo.


RIHANNA KUFUNGUA BIASHARA YA BANGI, KUITWA "MaRihanna"

Mwanamuziki maarufu wa kimataifa wa nchini Marekani, Rihanna anajiandaa kuzindua biashara ya Bangi itakayoitwa “MaRihanna”

Kwa mujibu wa mtandao wa Celeb Stoner wa nchini humo, Rihanna atazindua biashara yake mpya itakayojulikana kama MaRihanna. 

Imeripotiwa kuwa Rihanna ametangaza jijini Jamaica pamoja na kwamba hapajakuwa na taarfa rasmi kutoka katika kambi yake.

Rihanna alisikika akisema “MaRihanna ya Rihanna kwa kweli itakuwa ni kanabis mpya duniani na ni fahari kubwa kuwa mkongwe. MaRihanna inakuja kuliwasha soko”






KINYANG'ANYIRO CHA UNAIBU SPIKA, DK TULIA ACKSON APITA KWA KISHINDO

Dkt TULIA ACKSON MWANSASU

Matokeo ya zoezi la kura za Naibu Spika
Idadi ya wabunge halali kikatiba ni 394 
Webunge waliosajiliwa ni webbing 369
Akidhi ni 184

Waliopiga kura ni Wabunge 351, hakuna kura zilizoharibika 
Mh. Magdalena Sakaya amepata kura 101 sawa na 28.8%
Mh. Dk. Tulia Ackson Mwansasu amepata kura 250 sawa na 71.2%

Naibu Spika ametangazwa na kudhibitishwa rasmi na Spika wa Bunge, Mh. Job Ndugai. 

Dkt Tulia Ackson apishwa rasmi kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania


BREAKING NEWS: WAZIRI MKUU RASMI NI KASSIM MAJALIWA, ASHINDA KWA 73.5%

Mh. Nassim Majaliwa
Matokeo ya zoezi la kura za Waziri Mkuu
Idadi ya wabunge ni 394 
Waliopiga kura ni 351 
Zilizoharibika ni kura 2 sawa na 0.06%,
Kura za Hapana ni 91 sawa na 25.9%
Kura za Ndio ni 248 sawa na 73.5%

Waziri Mkuu ametangazwa na kudhibitishwa rasmi na Spika wa Bunge, Mh. Job Ndugai na kuita ni ushindi wa Kimbunga.

Ataapishwa kesho tarehe 20/11/2015, katika Ikulu ndogo ya Chamwino, jijini Dodoma


LOADING. . . KITI CHA NAIBU SPIKA KINAPIGIWA KURA SASA

DKT. TULIA ACKSON (CCM)                                    MAGDALENA SAKAYA (CUF)



TOA MAONI YAKO SASA HAPA CHINI 


MSAADA WA WASAMARIA WEMA WA MATIBABU UNAHITAJIKA KWA DADA HUYU


Ndugu Wasamaria wema
Napenda kutumia fursa hii kukushirikisha habari ya kusikitisha kuhusu dada Joyce Mwambepo (pichani akiwa na mwanaye, na migu yake iliyopooza) mkaazi wa Sinde jijini Mbeya. Dada huyu mwenye umri wa miaka 27 anaishi na bibi yake mwenye umri wa miaka 80 pamoja na mwanaye mwenye umri wa miaka 4.


BREAKING NEWS: NAFASI YA KUTEULIWA WAZIRI MKUU NI KASSIM MAJALIWA


Jina la Ukoo:     Majaliwa
Jina la Kwanza:     Kassim
Jina la Kati:     Majaliwa
Tarehe ya Kuzaliwa:     1960-12-22
Mahali Alipozaliwa:
Hali ya Ndoa:     Nimeoa
Kundi:     Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
Jinsia:     M
Simu ya Ofisi:     -
Simu ya mkononi:     0785205910
Barua pepe:     majaliwa.kasimu@yahoo.com
Anuani: P.O.Box 51,Ruangwa



Wednesday, November 18, 2015

KILIMANJARO MARATHON 2016 YAPIGWA TAFU ZAIDI YA MILIONI 200




Meneja Mawasiliano ya Umma wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, John Wanyancha akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika hafla ya kuzindua msimu mpya wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2016, ambapo Tigo wametoa zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya mbio hizo. Hafla hiyo imefanyika leo asubuhi jijini Dar es Salaam.


HAPA KAZI TU: KAMA ULINUNUA KIWANDA NA MASHIRIKA YA SERIKALI HII INAKUHUSU

Na Mwandishi Wetu
Serikali imetoa tamko kuwa baada ya siku 30 kuanzia sasa itarejesha mashamba na viwanda vyote vilivyobinafsishwa na wamiliki wake kukiuka masharti na kushindwa kuviendeleza.

Kauli hiyo imetolewa na ofisi ya msajili wa Hazina na kusainiwa na Lawrence Mafuru ambayo ndiyo imepewa majukumu ya kusimamia mali za serikali “ninawaagiza wawekezaji wote walionunua viwanda na mashamba yaliyokuwa yakimilikiwa na serikali kuwa wawakilishe taarifa zao za utekelezaji wa mkataba wa mauzo kwenye ofisi ya hazina”taarifa hiyo ilieleza.

Ofisi ya hazina imepewa mamlaka hayo kupitia tamko la serikali namba 203 na kuchapishwa juni 27,2014 pia kupitia sheria yake ya Treasury Registrar(power and function)Act,sura ya 370 na kurekebishwa mwaka 2010 imempa mamlaka ofisi ya Hazina kusimamia mashamba,viwanda na mali nyingine za serikali .

Taarifa hiyo inasema kuwa ofisi ya msajili wa Hazina kwa sasa inarejea mikataba yote ya mauzo ya viwanda na mashamba iliyoingiwa kupitia mpango wa ubinafsishaji na lueleza kuwa iwapo mikataba haijafuatwa hatua zitachukuliwa kwa wahusika. 

MAMA ADAI MZIMU WA MICHAEL JACKSON UMEMPA MIMBA, AFUNGUA KESI

Mwanamke mmoja ameibuka na madai kuwa amejifungua mtoto wa mzimu wa Michael Jackson. Mwanamke huyo amefungua kesi kuishitaki wamiliki wa mali za mkongwe huyo wa muziki wa Pop ili kupata fidia ya matunzo ya mtoto.

Kwa mujibu wa chaneli ya televisheni ya shirika la Now8News nchini Marekani, Kiera Johnson (Pichani Kushoto) alidai kuwa wakati anaangalia dvd ya saa mbili ya toleo maalumu la miaka 30 ya Michael Jackson (Michael Jackson 30 Year Anniversary Special), lipofikia sehemu ya muziki wa Thriller, macho yake yakawa mazito akasinzia. Na ndio hapo sasa maajabu yalipotokea…


HANDING OVER OF EQUIPMENT’S TO THE TANZANIAN POLICE FORCE (TPF)

Speech by the German Ambassador to Tanzania Honorable Egon Kochanke
Handing over of Equipment’s from German Bundeskriminalamt (BKA) to the Tanzanian Police Force (TPF) on 18.11.2015


Honorable Inspector General of Police Mr. Mangu,
Deputy Commissioner of Police Ally Lugendo,
Detective Chief Superintendant Sven Radke,
Detective Chief Inspector Rainer Harms,
Distinguished Participants of the Police Academy Dar es Salaam,

It is my privilege and great pleasure to address you today on the occasion of this handing-over ceremony of equipment from the German Bundeskriminalamt to the Tanzania Police Force.

Germany and Tanzania are good development partners. Germany is one of the top donors. Sometimes we forget some of the other areas where we work together – be it TPDF or the police.


Tuesday, November 17, 2015

KIPINDUPINDU CHANYEMELEA JIJI LA MBEYA


Na Mwandishi wetu,Mbeya

Halmashauri ya jiji la Mbeya limewataka wafanyabiashara ndogondogo hususani wa chakula kujijengea tabia ya kuchoma taka nyakati za jioni mara wamalizapo kuuza biashara zao na si kusubili gari ya taka kuja kuzoa.

Aidha imewataka wakazi hao kuondokana na fikra duni ya kuamini kuwa kazi ya uzoaji wa taka na kusafisha mazingira ni ya halmashauri ya Jiji na sio mali ya mtu.
( Picha Kushoto:Wafanyabiashara ndogo ndogo katika eneo la Makunguru jijini Mbeya wakiendelea na shughuli zao kama kawaida . )

Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Jiji la Mbeya, Dkt. Samweli Lazaro, amesema, wananchi wanatakiwa kujenga tabia ya usafi na sio kusubili kupigizana kelele na serikali kwa kuwahimiza kufanya usafi kwani adui mkubwa wa afya ni uchafu hivyo kila mmoja anapaswa kuwa mlinzi wa mwezake katika kutunza mazingira.


MKUTANO WA UMEME AFRIKA KUFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Mkutano wa mwaka maarufu kama POWERING AFRICA: Tanzania Investment Conference (www.PoweringAfrica-Tanzania.com) unatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam, katika hoteli ya Hyatt Regency, Kilimanjaro Hotel kwa siku mbili kuanzia tarehe 3 mwezi Disemba 2015.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kusambazwa na mtandao wa African Press Organisation mapema leo, mkutano huo utaangazia masuala ya umeme wa Tanzania baada ya uchaguzi, fursa za uwekezaji pamoja na kujenga mahusiano baina ya serikali na sekta binafsi katika soko la umeme.


BREAKING NEWS: MAKOPO YA BIA 48,000 ZA PEPSI ZAKAMATWA

Jamaa mmoja amenaswa nchini Saudi Arabia, wakati akijaribu kuingiza nchini humo zaidi ya makopo 48,000 ya bia aina ya Heineken, yaliyozibwa na kufanana na soda aina ya Pepsi (PICHANI KULIA), katika taifa hilo la kiislam lililoko Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu.

Pamoja na kuwa adhabu za makosa kama hayo hutofautiana ni kinyume cha sheria kukutwa na pombe katika Ufalme wa Saudi Arabia.

Kwa mujibu wa Mtandao wa LBC America, maafisa ushuru katika mpaka wa Al Batha walikamata shehena hiyo ilipokuwa ikijaribu kupenya na kuingia nchini humo.


Monday, November 16, 2015

BREAKING NEWS: RAIS AMTEUA DK TULIA ACKSON KUWA MBUNGE




MWANAMKE AUA MJAMZITO KISHA AMPASUA NA KUTOA MTOTO

Mwanamke mmoja amekamatwa na polisi nchini Mexico, baada ya kumshawishi mwanamke mjamzito kwenda nyumbani kwake kabla ya kumuua na kumpasua kisha kutoa mtoto ndani ya tumbo lake.

Nancy Carrasco (PICHANI KULIA), 34, ambaye pia alikuwa mjamzito na kisha mimba yake kuharibika miezi mitatu kabla ya kujifungua, lakini badala ya kuitaarifu familia yake, alidanganya kuwa bado ni mjamzito, linaarifu gazeti la Daily Mirror.

Licha ya uongo wake aliendelea kuhudhuria kliniki ya wajawazito kama kawaida na ndipo alikutana na mjamzito mwingine, Luviniydi Yasmin Velazques Thomas mwenye umri wa miaka 23, na kuanza urafiki naye.

SOMA ZAIDI. . .


Sunday, November 15, 2015

AFYA BORA INAANZA NA KIFUNGUA KINYWA BORA - SIKU YA KISUKARI DUNIANI

Dk. Bhuvaneshwari Shankar, Mkuu wa idara ya lishe kutoka hospitali za Apollo. (KUSHOTO
 PICHANI)

Na Mwandishi Wetu,
Novemba 14 kila mwaka tunaadhimisha siku ya kisukari duniani ili kuongeza uelewa kuhusu madhara ya kisukari, matatizo yanayoletwa na huu ugonjwa na taarifa muhimu kuhusu kisukari.

Siku hii inabeba ujumbe mahususi kwa watu wote ulimwenguni. Kauli mbiu katika siku hii tokea 2014 hadi 2016 ni maisha bora na kisukari(healthy living and diabetes) na mwaka huu kuna mtazamo zaidi katika kuzingatia mlo kamili na kuanza kila siku na kifungua kinywa bora.

Kutoka katika shirika la kisukari Africa, Tanzania ni kati ya nchi 32 katika shirikisho hilo kwa viwango vya nchi zenye viwango vya kisukari duniani. Kulikuwepo na zaidi ya kesi milioni 1.7 za kisukari hapa Tanzania kwa mwaka 2014. Shirika la afya duniani (WHO) linakadiria zaidi ya watu milioni 180 ulimwenguni wana kisukari, na hiyo takwimu inatarajiwa kuongezeka ifikapo mwaka 2030 kama hamna hatua yoyote itakayochukuliwa.


Friday, November 13, 2015

WATANZANIA WAPEWA SOMO KUHUSU DIPLOMASIA YA UCHUM (ECONOMIC DIPLOMACY)

Kutoka kushoto ni Balozi mstaafu Ahmed Kiwanuka,Nduwayo Mzonya,Hussein Melele,na Rashid Njenga wakiwasikiliza wachangaji mbalimbali katka kongamano hilo lijulikanalo Epowerment of Economic Diplomacy in Tanzania .


UZINDUZI WA USHIRIKA WA MAMA NA BABA LISHE KUFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Mratibu na Msimamizi Mkuu wa Jumuiya Ya Mama na Baba Lishe Mkoa wa Dar es Salaam, Said Said (wa pili toka kulia), akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idata Maleleo kuelezea kuhusu Uzinduzi wa Ushirika wa Mama na Baba Lishe unaotarajia kufanyika Novemba 15, 2015 ukumbi wa SabaSaba jijini Dar es Salaam. Lengo la jumuiya hiyo kuunganisha kwa pamoja wadau mbalimbali, kutoa fursa kulinda haki za ajira na kuzitafutia ufumbuzi na kuondoa tatizo la ajira kupitia tasnia hii ikiwa ni kumtambua mama na baba lishe kama sehemu ya maisha ya kila mmoja wetu, kwani kila mtanzania anaufahamu umuhimu wa mama na baba lishe na takwimu zinaonyesha asilimia 50% ya wanzania waishio mijini hupata huduma ya chakula. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.