Inaaminika kuwa Sabina alifariki mwezi disemba mwaka jana wakati wa kipindi cha mapigano makali. Wasichana hao wawili walionekana katika video ya propaganda za ISIS mda mfupi baada ya kuwasili nchini Syria. Rafiki yake ambaye waliambatana aliuwawa miezi michache kabla yake.
Samra Kesinovic na rafiki yake Sabina Selimovic(kulia) wakiwa katika picha iliyopigwa na kundi la magaidi wa ISIS mda mfupi baada ya kuwasili nchini Syria mwezi aprili 2014.

Pamoja na kwamba maafisa wa serikali wamegoma kuongelea suala hilo.
Wasichana hao wawili wenye asili ya Viena wakiwa na umri wa miaka 17,16 ambao wazazi wao wote wawili ni wakimbizi wa Bosnia, walipotea mwezi aprili mwaka jana, kwa madai kuwa wanataka kwenda kupigana vita nchini Syria.

Mapema mwaka huu, maafisa wa Umoja wa Mataifa waliripoti kuwa wasichana wawili wenye asili ya Austria wenye makazi yao Vienna wamedhibitishwa kufa katika mapigano.
Kwanza walikwenda katika mji mkuu wa Uturuki, Ankara kwa ndege, baadae walielekea kusini mwa Uturuki katika mji wa Adana. Baada ya hapo walipotelea kusiko julikana.
Badala yake walionekana katika mitandao ya kijamii wakionekana na mabunduki huku wamezungukwa na watu wenye silaa, picha zilizoonesha kutumiwa kwaajili ya kuvutia utafuta wasichana ambao wangejiunga na kundi hilo.
No comments:
Post a Comment