Showing posts with label news. Show all posts
Showing posts with label news. Show all posts

Monday, June 11, 2018

KITUO CHA AFYA TAMOTA - BUMBULI VIJIJI 20 KUNUFAIKA


PICHANI: Moja ya majengo ya Kituo cha Afya Tamota, Jimbo la Bumbuli mkoani Tanga, ambapo Mbunge wa Jimbo hilo January Makamba alikagua ujenzi wake jana Juni 10, 2018. (Picha na Yusuph Mussa, Immamatukio Blog).

Na Yusuph Mussa, 
Immamatukio Blog, 
Lushoto

WANANCHI wa vijiji zaidi ya 20 wanatarajiwa kunufaika na ujenzi wa Kituo cha Afya Tamota kilichopo Kijiji cha Tamota, Tarafa ya Bumbuli, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.

Ni baada ya Serikali Kuu kutoa sh. milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa majengo muhimu kwa iliyokuwa Zahanati ya Tamota ili kuwa Kituo cha Afya.

Mbunge wa Jimbo la Bumbuli January Makamba jana Juni 10, 2018 alitembelea Kituo cha Afya Tamota kuona ujenzi unavyoendelea ambapo kwa sasa ujenzi wake umefikia hatua ya linta.

Baadhi ya majengo yanayojengwa ni wodi ya wanawake ikiwemo wazazi, maabara, upasuaji na nyumba ya mtumishi, ambapo hadi sasa ujenzi huo umegharimu sh. milioni 135.6

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Afisa Mtendaji wa Kata ya Tamota Sophia Matogolo alisema kati ya fedha hizo, wananchi wamechangia sh. milioni 10 ikiwa ni pamoja na kuchota maji na kuchimba msingi wa majengo hayo.

Katibu wa Mbunge ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kwamkomole, Hozza Mandia alisema kituo hicho kitamaliza matatizo ya wananchi kupata huduma za afya kwenye kata za Tamota, Mahezangulu na Funta katika Jimbo la Bumbuli.



Sunday, June 10, 2018

WAZIRI AAGIZA KUKAMATWA KIONGOZI ALIYEFUJA MILIONI 23


PICHANI: Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati akizungumza na wakulima wa pamba katika kijiji cha Msai wilaya ya Iramba akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Singida kutembelea vituo na kujionea ununuzi wa pamba, Picha Zote Na Mathias Canal, WK


Na Mathias Canal-WK, Singida

Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba amemuagiza Mrakibu wa polisi Wilaya ya Iramba ASP Magoma Mtani kumkamata aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha ushirika (AMKOS) Msai.

Waziri Tizeba ametoa agizo hilo jana 9 June 2018 Mara baada ya kutembelea kitongoji cha Kati, Msai na Mtoa akiwa katika ziara ya kikazi ya Siku mbili kwa ajili ya kutembelea vituo vya ununuzi wa pamba na kujionea msimu wa ununuzi wa zao hilo katika vijiji hivyo.

Dkt Tizeba amelaani vikali ufujaji huo wa fedha za wakulima huku akimtaja Paul Ramadhan Kurwa kuhusika na ufujaji huo wa shilingi milioni 23 huku akiendelea kuonekana mtaani pasina kuchukuliwa hatua za kisheria.

"Wakati muelekeo wa serikali yetu inayoongozwa na Rais wetu Dkt John Pombe Magufuli ukijipambanua kutaka kuboresha maisha ya watanzania kupitia Kilimo lakini kuna watu wanataka kurudisha nyuma juhudi hizo, hakika tutawapa kibano kweli kweli hakuna utani kwenye fedha za wananchi" Alikaririwa Dkt Tizeba

Mhe Tizeba ametoa siku moja kukamatwa kwa mwizi huyo na kufikishwa mahakamani ili awe mfano kwa wezi wengine wasio kuwa na haya wala soni.

Aidha, amewataka wananchi katika msimu huu wa uuzaji na ununuzi wa Pamba kutouza Pamba zenye uchafu wakidhani wataongeza idadi ya kilo kwani kufanya hivyo ni kufifihisha juhudi zao wenyewe jambo ambalo halina tija.



Sunday, June 03, 2018

MAPACHA WALIOUNGANA CONSOLATA NA MARIA WAFARIKI DUNIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwajulia hali watoto wawili Mapacha walioungana Maria na Consolata ambao wamelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)kwa ajili ya Matibabu.


Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa familia, Masista wa Maria Consolata na wote walioguswa na kifo cha mabinti mapacha walioungana Maria na Consolata Mwakikuti waliofariki dunia jana jioni katika hospitali ya Mkoa wa Iringa.

Mhe. Rais Magufuliwa aliwatembelea Maria na Consolata walipokuwa wakipata matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Jijini Dar es salaam tarehe 06 Januari, 2018.

Pamoja na kuwapa pole Maria na Consolata waliongoza sala ya kuliombea Taifa na Viongozi wake.



Saturday, June 02, 2018

MTAJI WA BENKI YA TPB UMEKUWA KUTOKA BILIONI 8 HADI BILIONI 60

 
Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki hiyo,Proffesa Lettice Rutoshobya akifungua tawi jipya la TPB mkoani Tanga kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Sabasaba Moshingi akishuhudia


Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki hiyo,Proffesa Lettice Rutoshobya akikata utepe kushiria ufunguzi wa tawi la TPB Tanga kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Sabasaba Moshingi na kulia ni Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Wakurugenzi wa TPB Dkt Edmund Mndolwa


MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB Dkt Edmund Mndolwa amesema mtaji wa benki hiyo hivi sasa umekuwa kutoka Bilioni 8 hadi kufikia Bilioni 60 hatua inayoonyesha utendaji mzuri wa wafanyakazi kutokana na kutoa huduma bora zinazowafanya wateja kuvutiwa na kujiunga nao.

Dkt Mndolwa aliyasema hayo leo wakati wa ufunguzi wa tawi la Tanga la Benki hiyo lililopo eneo la Chumbageni Jijini Tanga ambao ulifanywa na Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Proffesa Lettice Rutashobya kwenye halfa iliyofanyika mjini hapa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wajumbe wa bodi ya wakurugenzi na wafanyakazi.

Alisema hatua hiyo inatokana na huduma nzuri inayotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo na hivyo kusaidia kuwepo kwa ongezeko kubwa la wateja jambo ambalo limepelekea kuongezeka matawi nchini kutoka 32 mpaka 74 kwa sasa.

“Niwapongeze sana TPB kwa kasi kubwa ya utendaji mzuri mliokuwa nayo na kupelekea kuwezesha kupanua wigo wa matawi kwa wateja wenu ambapo awali kulikuwa na matawi 32 lakini hivi sasa yamefikia 74 hii ni hatua nzuri sana hivyo kuwatake muendelee nayo “Alisema.

“Lakini pia nimpongeze Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi anayemaliza muda wake Proffesa Lettice kwa kazi nzuri aliyoifanya jambo ambalo limewezesha kufikia mafanikio yaliyopo hivi sasa ndani ya benki hii nitaendelea kushirikiana na wafanyakazi “Alisema.



RC AAGIZA KOROGWE KUWA NA STENDI MOJA YA MABASI


PICHANI: Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela (kulia) akiteta jambo na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Godwin Gondwe kwenye kikao na wadau wa Korogwe juu ya hatma ya matumizi ya stendi mbili katika Mji wa Korogwe. Kikao hicho kilifanyika jana Juni mosi, 2018 kwenye Ukumbi wa Halmashsuri ya Mji Korogwe (Picha na Yusuph Mussa).

Na Yusuph Mussa, Korogwe

MKUU wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela ametengua maamuzi ya Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji Korogwe ya kuruhusu kutumika kwa stendi mbili katika Mji wa Korogwe.

Na badala yake, ameagiza stendi itakayotumika ni ile ya Kilole ambayo Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli aliifungua Agosti 7, 2017, na kuachana na stendi ya zamani ya Manundu.

Aliyasema hayo jana Juni mosi, 2018 kwenye Mkutano uliofanyika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Korogwe na kuwashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo madiwani, wakata tiketi za mabasi, wafanyabiashara, watumishi na kamati za ulinzi na usalama za wilaya ya Korogwe na mkoa wa Tanga, na kufanya mikutano ya hadhara kwenye stendi hizo.

Pamoja na marufuku hiyo ya stendi ya zamani, pia ameagiza vituo vya maegesho ya magari kwenye barabara kuu ya Dar es Salaam kwenda Arusha kuanzia Mtonga, Mwembeni, Uwanja wa Sokoni, CRDB, Majengo na Kilole viondolewe.

"Kuanzia tarehe ya leo (Juni mosi) stendi ya mabasi itakuwa moja nayo ni Kilole. Na hiyo ni kutokana na kuongeza mapato ya Halmashauri ya Mji Korogwe. Lakini ni lazima turejee kwenye makusudio yetu ya kujenga stendi mpya, nayo ni kukidhi mahitaji ya wananchi kuweza kupata eneo nzuri na la kisasa katika kutoa huduma.

"Uwepo wa stendi ya zamani (Manundu) kufanya kazi, kunaharibu utaratibu tuliojiwekea, kwani badala ya mabasi kuingia Stendi ya Kilole, yanabaki stendi ya zamani, hivyo kuathiri ufanyaji wa shughuli kwenye stendi mpya. Lakini pia stendi zote zilizopo pembeni ya barabara kuu ziondolewe, zinachangia abiria na mabasi kutoingia stendi mpya" alisema Shigela.

Shigela alisema Stendi ya Manundu itumike kama daladala kwa magari yanayotoka kwenye kata za Halmashauri ya Mji Korogwe, bodaboda na bajaj na si vinginevyo, kwani hata idadi ya magari yanayoingia stendi ya zamani iliyoelezwa na madiwani kuwa hayazidi 10, siyo ya kweli, kwani zaidi ya magari makubwa 40 yanaingia stendi ya zamani kwa siku.



DKT. KIGWANGALLA ASHIRIKI MAZISHI YA MAMA MZAZI WA HUSSEIN BASHE NZEGA


Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Vijijini, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimfariji mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe kufuatia kifo cha mama yake mzazi aliyezikwa leo wilayani Nzega. Kulia ni mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye. Wabunge mbalimbali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiongozwa na Abdallah Bulembo wameshiriki msiba huo pamoja na viongozi mbalimbali wa vyama na Serikali.


Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Nzega Vijijini, Dkt. Hamisi Kigwangalla (kulia) akimfariji mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe kufuatia kifo cha mama yake aliyezikwa leo wilayani Nzega. Kulia ni mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye na mbunge wa Kigoma Vijijini, Peter Selukamba. Wabunge mbalimbali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiongozwa na Abdallah Bulembo wameshiriki msiba huo pamoja na viongozi mbalimbali wa vyama na Serikali.



Thursday, May 31, 2018

KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO AONGOZA WAJUMBE WA KAMATI YA MAAFA KUTEMBELEA BWAWA LA NYUMBA YA MUNGU

Eneo la Kitongoji cha Mferejini lililotengwa na Serikali kwa ajili ya kuanzisha kambi kwa ajili ya Wahanga wa Mafuriko .

Wahanga wa Mafuriko wakianza ujenzi wa nyumba za Miti kwa ajili ya kujisitiri katika eneo la Ruvu Mferejini.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

SERIKALI imetoa siku mbili kwa wananchi waliosalia katika Vijiji vya Ruvu Mferejini na Ruvu Marwa wilayani Same ,Mkoani Kilimanjaro vilivyozingirwa na maji kuondoka mara moja na kwamba watakao kaidi wataondolewa kwa kutumia nguvu na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Zaidi ya watu wapatao 2000 wamelazimika kuyahama makazi yao baada ya kufikwa mafuriko kutokana na mvua kubwa za masika zinazoendelea kunyesha huku eneo lililoathirika zaidi na mvua hizo ni ukanda wa tambarare wa wilaya ya Same unaopakana na Bwawa la Nyumba ya Mungu.

Licha ya Idadi hiyo ya watu kuyahama makazi yao lakini bado wapo waliokaidi kuondokana na hapa Serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Same ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Wilaya hiyo ,Rosemerry Senyamule ,ikatoa agizo.



MAFURIKO SAME YAKATA MAWASILIANO YA MIOUNDO MBINU ,WANACHI WATUMIA MITUMBWI NA TREKTA KUSAFIRISHA MALI ZAO.



Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro,Aisha Amour (aliyenyoosha mkono) akiwa na baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Maafa ya mkoa wakiwa eneo la Ruvu Darajani ambako magari yanaishia baada ya miuondo mbinu ya barabara kujaa maji .

Moja ya barabara ambayo ilikuwa ikitumiwa na wakazi wa maeneo ya Ruvu Muungano na Darajani ikiwa imejaa maji na kusababisha adha kwa wasafiri.



Tuesday, May 29, 2018

HUU NDIO MSINGI NA WAJIBU WA VYOMBO VYA HABARI KATIKA TAIFA



TPA TANGA YAJIVUNIA KASI YA UTOAJI HUDUMA


PICHANI: Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage akisalimia na Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga alipokwenda kufungua maonyesho ya sita ya biashara ya kimataifa

Na Mwandishi Wetu

MENEJA wa Bandari ya Tanga (TPA) Percival Salama amesema wanajivunia kuboreshwa huduma zao kwa kiwango kikubwa ikiwemo uandaaji wa nyaraka kwa kasi na usalama wa kutosha kwa wateja na hivyo kutumia muda mfupi kutokana na taasisi zinazohusika kuwepo sehemu moja hivyo kuwawia rahisi kuweza kufanya shughuli zao kwa wakati mmoja.

Salama aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya kimataifa ya sita ya biashara ambapo alisema kutokana na hali hiyo hakuna sehemu ambayo mteja anaweza kupita akikwama bila wao kujua mara kila hatua wanazokuwa wakipitia wanatambua mara moja.

Alisema kuwa sehemu ambazo mteja anaingia kwenye bandari hiyo anapata taarifa moja kwa moja hiyo ikiwa wanakumbana na vikwazo vya namna yoyote zikijitokeza inawawia rahisi kuweza kuona na kuvishughulia kwa muda mfupi ili kuweza kuondoa usumbufu ambazo unaweza kuwakabili wafanyabiashara.



Monday, May 28, 2018

WAZIRI UMMY AMWAGA FUTARI KWA TAASISI 10 ZA KIDINI NA MAGEREZA, TANGA




PICHANI: Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) kushoto akimkabidhi futari Mkurugenzi wa Taasisi ya kulea watoto wanaoishi kwenye Mazingira magumu ya Goodwill Sayyed Muhdhar Idarus ambapo futari hiyo ambapo taasisi 10 zilipewa futari hiyo kwa kila taasisi ni Unga wa ngano kg 50, mchele kg 100,unga wa ngano kg 50,Sukari Kg 25,Tambi Mfuko miwili,Mafuta ya kula lita 20na majani ya chai kilo 3,Maharage Kg 100 na Unga wa Dona Kg 25 vyote vikiwa na thamani y ash.milioni 6.8

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kupitia Taasisi yake ya Odo Ummy Foundation leo amegawa futari kwa taasisi za kiislamu na magereza zilizopo Jijini Tanga vyakula mbalimbali ili viweze kuwasaidia wakati wa mwezi mtukufu wa ramadhani.

V yakula ambavyo vimetolewa na Waziri Ummy ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) kwa kila taasisi ni Unga wa Ngano Kg 50, mchele kg 100,Sukari Kg 25,Tambi Mfuko miwili,Mafuta ya kula lita 20,Maharage kg 100, unga wa dona kg 25,na majani ya chai kilo 3 vyote vikiwa na thamani y ash.milioni 6.8

Akizungumza mara baada ya kukabidhi futari hizo mapema leo taasisi zenye wanafunzi waliotika maeneo mbalimbali na wakati mwengine wanakuwa hawana uhakika wa kufutari,watu wengine wajitoleza kulea taasisi hizo pamoja na

Alisema ameona atoe futari hiyo kwa kila taasisi badala ya kuwaita pamoja kufuturu nao maana wengine wanaweza kushindwa kupata fursa ya kuhudhuria lakini wakikabidhiwa wanaweza kuona namna nzuri ya kuweza kuitumia wakati wa mfungo mtukufu wa ramadhani.

“Nimeona ni bora nitoe futari hii badala ya kwenda kufuturu kila mahali kwani tutakapofanya hivyo wanaweza kuja wachache na mimi kutokana na kuwa nimetoka kwenye familia ya watu wa kawaida maskini nimeona angalu hicho kidogo ambacho nimejaliwa nitoa kwa taasisi za dini na watoto kwenye mazingira magumu”Alisema.



NHIF TANGA YAHAMASISHA WAFANYABIASHARA KUJIUNGA NA MPANGO WA BIMA YA AFYA



MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) umesema watatumia maonyesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea Jijini Tanga kuwahamasisha wafanyabiashara kujiunga nao ili waweze kunifaika na huduma za matibabu pindi wanakuwa wakikumbana na magonjwa mbalimbali.

Hayo yalisemwa jana na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Sophia Kaku wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda lao kwenye ufunguzi wa maonyesho ya sita ya biashara ya kimataifa yanayofanyika eneo la Mwahako mjini hapa.

Alisema watakapojiunga nao wataweza kuwa na uhakika wa matibabu wakati wanapougua lakini pia itawawezesha kuepukana na kutumia fedha nyingi pindi wanapokuwa wakiugua zinazotokana na kupanda kwa gharama.

“Ndugu zangu maradhi yanakuja bila taarifa hivyo iwapo tutawekeza kujiunga na mpango wa Mfuko huu unaweza kufaidika na matibabu lakini pia utaepukana na gharama kubwa za matibabu utakazopaswa kulipia wakati unapokumbana na magonjwa mbalimbali “Alisema.



KINANA, MBUYU KWENYE MSITU WA SIASA

Image may contain: 2 people, people smiling, people standing
Na Emmanuel J. Shilatu

Kanali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Abdulrahman Omar Kinana anatajwa kuwa katika orodha ya safu za viongozi mibuyu na migude kwenye misitu minene ya siasa yenye kuhimili tufani za kila aina pia Mwanasiasa anayependa kuheshimu utamaduni, utaratibu na mwenye kuishi kwa misingi ya nidhamu .

Kinana anatajwa kama zao miongoni mwa kunga zitokanazo na mazao katika medani za siasa, utawala, uongozi na aliyeshiba ujuzi toshelezi wa masuala ya diplomasia ya siasa pia anayejua mahusiano yatokanayo na historia, harakati za ukombozi na umoja wa Afrika.

Sauti yake aghalabu huwa na mvumo wa mawimbi ya busara, fikara njema na hekima zenye wito pele aamuapo kusema, kukosoa, kutetea, kukumbusha, kushauri au kuonya kutokana na tabia yake ya kufanya yote hayo kwa hali ya kujiamini akiwa na nguvu ya hoja.

Ukimya wa Mwanasiasa huyo siku zote ni kama mfano wa Simba hodari awindae nyikani au mbugani akiwa hana pupa wala kiherehere. Huyafanya yote kwa utulivu na umakini mkubwa ambao baadae haumletei majuto, athari wala taathira.

Ni Mwanasiasa wa aina yake aliyewahi kuhitajiwa na Marais (Wenyeviti) watatu awe katibu mkuu wa CCM akakataa huku akitoa madai mazito yenye msingi, nguvu ya hoja na maana.



Sunday, May 27, 2018

MAKAMU WA RAIS AKIPONGEZA CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE TANZANIA (TAWLA) KWA KUTOYUMBA



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassanakisalima iana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndungulile wakati walipowasili kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam kwa ajili yakufungua mkutano wa Chama cha Wanzsheria wanawake Tanzania TAWLA.

Amesema “Nawapongeza TAWLA kwa namna ya kipekee sana kwa kutimiza miaka 28 ya uhai wake. Ni miaka 28 ya mafanikio makubwa sana. Nawapongeza kwa sababu, katika miaka 28 ya uhai wenu, hamjawahi kuyumba wala kutoka nje ya lengo la kuanzishwa kwenu, ambalo ni kutumia taaluma ya sheria kuwasaidia wanawake wasio na uwezo kupata msaada wa kisheria na haki zao.” alisema Makamu wa Rais.



MPINA AMWAGA PIKIPIKI KWENYE MINADA YA MIPAKANI


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina(mwenye miwani) akikagua moja kati ya pikipiki kumi kabla ya kuzikabidhi ili zitumike kwenye minada ya mipakani na upili.Picha na John Mapepele


Na John Mapepele

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina ameagiza maeneo yote ya minada ya awali na upili yapimwe na kuwekwa alama za mipaka katika mwaka wa fedha 2018/19 ili kuepuka uvamizi unaofanywa na watumiaji wengine wa ardhi.

Maelekezo hayo ameyatoa leo kwenye hafla ya iliyofanyika kwenye Ofisi ya Dar es Salaam wakati akikabidhi pikipiki kumi ili zitumike kwenye mipaka na minada ya upili kwa lengo la kudhibiti utoroshaji wa mifugo na mazao yake nje ya nchi.

Alisema Serikali inakusudia kuifunga minada yote iliyoanzishwa kiholela kwa nia ovu ambapo amesema kuendelea kubaki kwa minada hiyo kunadhoofisha minada ambayo imeanzishwa kwa kufuata taratibu za Serikali.



NAIBU WAZIRI MAVUNDE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA WCF KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI JIJINI MBEYA


 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, akipeana mikono na mama mjane, Atulehemu Kiduko, ambaye analipwa fidia ya kila mwezi kufuatia kifo cha mumewe wakati akiwa kazini kwenye kiwanda cha karatasi Mgololo kilichoko Mufindi mjini Iringa. mama huyo alitoa ushuhuda wa huduma anayopata kutoka WCF wakati wa kutano baina ya Serikali na wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini uliofanyika jijini Mbeya Mei 26, 2018 kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa WCF Bw. Masha Mshomba.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, akifungua mkutano baina ya Serikali na wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini uliofanyika jijinmi Mneya Mei 26, 2018 kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi.

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mbeya

SERIKALI ilianzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kwa lengo la kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanapata mafao bora na stahiki ya fidia tofauti na sheria ya zamani iliyotoa viwango vya chini vya fidia, lakini pia kuwawezesha waajiri kupata muda zaidi kushughulikia masuala yao ya uzalishaji na uendeshaji.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde, jijini Mbeya leo Mei 26, 2018 wakati akifungua mkutano baina ya Serikali na wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi.

Mhe. Mvunde alisema viwango vya juu vya malipo ya fidia kwa wafanyakazi walipokuwa wanaumia kazini kabla ya sheria ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, ilikuwa ni shilingi 108,000/=kwa mfanyakazi aliyepata ajali au kuumia kazini, lakini pia sheria inasema kulikuwa na malipo mengine ya shilingi 83,000/= kwa mfanyakzi aliyefariki kwa ajali au ugonjwa kutokana na kazi aliyokuwa akifanya na malipo hayo yalitegemea pia mkataba wa ajira yake unasemaje.



Friday, May 25, 2018

MAKAO MAKUU HALMASHAURI YA BUMBULIKUJENGWA KWEHANGALA


PICHANI: Ramani ya jengo la Halmashauri ya Bumbuli litakavyokuwa. (Picha na Yusuph Mussa, Immamatukio Blog).

Na Yusuph Mussa, Bumbuli
Immamatukio Blog

HATIMAYE Jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Bumbuli katika Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga ujenzi wake unatarajiwa kuanza mapema Juni, mwaka huu kwenye Kijiji cha Kwehangala katika kata ya Dule B.

Hafla ya utiaji saini kwa ajili ya ujenzi huo umefanyika leo Mei 25, 2018 Ofisi za Halmashauri mjini Bumbuli na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bumbuli Ameir Shehiza, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bumbuli Peter Nyalali, baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo, watendaji na wananchi pamoja na mkandarasi.

Nyalali alisema siku hiyo ni ya aina yake, kwani ni Mungu pekee amewezesha kufikia muafaka baada ya vikwazo vingi.

"Ni Mungu pekee aliyewezesha siku ya leo kufikia hapa na kushuhudia utiaji saini kwa ajili ya ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Bumbuli, Kwehangala. Lakini kama sio yeye (Mungu), wengine sisi tungekuwa gerezani. Mtu wa pili kumshukuru ni Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli. Yeye baada ya kubaini hali halisi, aliamua kuturudishia fedha tuendelee na ujenzi.

"Shukrani pia zimuendee Mwenyekiti wa Halmashauri, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, watendaji na wananchi kwa kusaidia jambo hili kufanikiwa" alisema Nyalali.

Awali, Shehiza alimtaka Mkurugenzi Nyalali awathibitishie maslahi ya mkandarasi anaejenga jengo hilo Kampuni ya Advent Construction Ltd ya jijini Dar es Salaam kuwa yatalindwa na kufanya kazi yake kwa wakati. Lakini pia kujua ataanza lini kazi hiyo.



Thursday, May 24, 2018

MAPORI MATANO YA AKIBA MKOANI KAGERA NA GEITA KUPANDISHWA HADHI YA KUWA HIFADHI ZA TAIFA


PICHANI: Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamisi Kigwangalla akizungumza bungeni alipokuwa akijibu hoja wa wabunge waliochangia mjadala wa bajeti wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019, jijini Dodoma juzi.

Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Maliasili na Utalii imetangaza kuanza mchakato wa kuyapandisha hadhi Mapori ya Akiba ya Burigi, Kimisi, Biharamulo, Ibanda na Rumanyika kuwa Hifadhi za Taifa. Mchakato huo tayari umeungwa mkono na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Hayo yameelezwa juzi bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akihitimisha mjadala wa bajeti wa makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

“Mheshimiwa Spika, ninaomba kulitaarifu Bunge lako tukufu kuwa Mhe. Rais ameridhia ombi letu la kupandisha hadhi Mapori ya Akiba ya Burigi, Kimisi, Biharamulo, Ibanda na Chief Rumanyika kuwa Hifadhi za Taifa, kipekee namshukuru sana Mhe. Rais kwa kuridhia ombi letu hilo” amesema Dkt. Kigwangalla.

Amesema kufuatia hatua hiyo, wizara yake inaanzisha mchakato rasmi wa kukamilisha taratibu za kupandisha hadhi mapori hayo ili kupanua wigo wa vivutio vya utalii katika kanda ya Kaskazini Magharibi na hivyo kufikia azma ya Serikali kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni 8 na mapato ya dola za kimarekani bilioni 16 katika kipindi cha miaka 7 ijayo.

Inaelezwa kuwa mchakato huo utapitia hatua mbalimbali ikiwemo kuwashirikisha wadau husika kupata maoni yao, mapendekezo kuwasilishwa baraza la mawaziri kabla ya kujadiliwa bungeni na hatimaye kuwasilishwa kwa Mhe. Rais kwa ajili ya kuidhinishwa kuwa Sheria kamili ya kupandisha hadhi mapori hayo.



Wednesday, May 23, 2018

ZAWADI YA KUWAPA WATOTO KIPINDI CHA SIKUKUU NI TOTO AFYA KADI



WAZAZI na Walezi mkoani Tanga wametakiwa kuhakikisha wanawapa watoto wao zawadi kwenye kpindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani kwa kuwaingiza kwenye mpango wa Toto Afya Kadi ili waweze kunufaika na matibabu wakati wanapougua.

Hayo yalisemwa na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Macrina Clemens (Pichani Juu) ambapo alisema zawadi hiyo ni muhimu sana katika ukuaji wao badala ya kuwanunulia nguo ambazo wanavaa kwa wakati Fulani na baaadae kwisha.

Alisema mpango huo ni muhimu kwa watoto wao kutokana na kuwahakikishia kupata huduma za matibabu wakati wote wanapokumbana na magonjwa mbalimbali ambayo yanaweza kuathiri.

“Ndugu zangu wazazi na walezi kwenye kipindi hiki cha mwezi wa ramadhani zawadi mzuri ambayo mnaweza kuwapatia watoto wenu ni kuwaingiza kwenye mpango huu wa Toto Afya Kadi kwani malipo yake yana muwezesha mtoto kupata huduma za matibabu mwaka mzima kwa kiasi cha sh.50400”Alisema.