Showing posts with label SPORTS. Show all posts
Showing posts with label SPORTS. Show all posts

Monday, May 21, 2018

RITTA KABATI CHALLENGE CUP MSIMU 2018 YAANZA RASMI,TIMU ZAOMBWA KUCHUA FOMU KUSHIRIKI


Kulia ni Mwenyekiti wa mashindano ya Ritta Kabati challenge cup 2018 na kushoto ni katibu wa kamati ya mshindano hayo walipokuwa wakiongea na vyombo vya habari kwenye ofisi zao zilizopo manispaa ya Iringa mkoani Iringa mapema hii leo


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Kamati ya ya mshindano ya Ritta Kabati challenge cup 2018 imezindua rasmi kwa kuanza kuzialika timu kwa ajiri ya kuchukua fomu kushiriki na wameweka bayana jinsi mfumo wa mashindano utakavyokuwa pamoja na zawadi kwa washindi wote.

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa mashindano hayo Gerald Malekela alisema kuwa analialika timu mbalimbali za mkoa wa Iringa kuja kuchukua fomu za mashindano kwa gharama ya shilingi elfu thelathini (30,000/=) ambazo zinapatikana katika kituo cha radio cha Nuru Fm.

“Naomba viongozi wa vilabu vinavyotaka kushiriki mashindano haya vinatakuwa kufika katika ofisi za Nuru fm au kumpigia mratibu wa mashindano haya Fredy Mgunda kwa kumpigia simu ya nambari 0714201006 au mnipigie mimi mwenyewe kwa namba hii 0762687732 hapo utakuwa umerahisisha jinsi ya kuzipata hizo fomu na maelezo kwa kina” alisema Malekela



Saturday, April 21, 2018

KIGWANGALA ATUMIA NGORONGORO MARATHON KUWATUMIA SALAMU MAJANGILI

PICHANI: Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamis Kigwangala (fulana nyekundu) akiwa na uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) pamoja na baadhi ya washiriki wa mbio za Ngorongoro Marathon zilizofanyika leo Aprili 21, 2018. Wengine ni Mwenyekiti wa Bodi ya NCAA Profesa Abiud Kaswamila (namba 002), Mhifadhi Mkuu wa NCAA Dkt. Fred Manongi (namba 003) na Meneja Mahusiano wa NCAA Joyce Mgaya (kulia waliosimama). (Picha na Yusuph Mussa Immamatukio Blog).

Na Yusuph Mussa, Karatu
Immamatukio Blog

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamis Kigwangala ametuma salamu kwa majangilli wanaojihusisha na uwindaji haramu wa wanyama kwenye Hifadhi za Taifa ikiwemo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA).

Amesema Serikali na wadau wengine wamejipanga kuhakikisha rasilimali za nchi zinalindwa kwa kudhibiti ujangili wa wanyama na viumbe hai vyote vinavyotokana na maliasili yetu ya asili kwenye hifadhi za Taifa.



Wednesday, April 11, 2018

NCAA YADHAMINI NGORONGORO MARATHON

Mashindano ya Ngorongoro Marathon 2017, ambayo kwa mara ya kwanza yalidhaminiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Mamlaka hiyo inadhamini kwa mara ya pili mwaka huu. (Picha na Yusuph Mussa, Immamatukio Blog).

Na Yusuph Mussa, Tanga
Immamatukio Blog

MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongo (NCAA) imedhamini mashindano ya Ngorongoro Marathon kama sehemu ya njia ya kukuza utalii kwenye eneo hilo lenye vivutio vya pekee duniani.

Akizungumza na waandishi wa habari leo (Aprili 11) jijini Tanga, Naibu Mhifadhi wa NCAA Asangye Bangu, alisema mashindano hayo yatakuwa na faida kubwa kwenye nyanja za utalii na kuwezesha watu wengi ndani na nje ya nchi kuvutiwa na hifadhi hiyo.

"Tumeamua kudhamini mashindano haya ya Ngorongoro Marathon yanayofanyika Aprili 21, mwaka huu. Nia ya kudhamini mashindano haya, kwanza ni kufanikisha mashindano yenyewe na pili ni kuweza kutangaza utalii wetu.

"Tunaamini sisi Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro tuna dhima kubwa kuona watalii wa ndani na nje wanaongezeka. Lakini ili waongezeke ni lazima tutumie njia mbalimbali za kutangaza vivutio vya Hifadhi za Ngorongoro ambavyo ni vya kipekee duniani" alisema Bangu.



Saturday, March 24, 2018

BOLT AIBUKIA UJERUMANI, KUCHEZA SOKA BORUSSIA DORTMUND (ANGALIA PICHA)

Na Mwandishi Wetu
Immamatukio Blog

Mshindi wa medali ya dhahabu mara nane katika Olympic, Usain Bolt, ameanza majaribio katika mchezo wa mpira wa miguu nchini Ujerumani katika klabu ya Borussia Dortmund, kwa lengo la kuendeleza kipaji cha soka.

Mjamaika huyo ambaye ni mshindi wa mbio za mita 100 na 200 na hatimaye kuweka rekodi ya dunia kuwa ni mru mwenye mbio Zaidi, alionekana akifanya mazozi katika viwanja vya timu ya Borussia Dortmund mapema ijumaa (jana).

Mwanariadha huyo mkongwe alisikika mara kadhaa akisema moja ya ndoto yake ni kujiunga na kuchezea timu ya Manchester United ya nchini Uingereza.


Tazama picha hapa:-




Friday, March 02, 2018

RATIBA ROBO NA NUSU FINALI KOMBE LA SHIRIKISHO ZAKAMILIKA

Upangaji wa ratiba kwa hatua ya robo fainali na nusu fainali ya mashindano ya Kombe la Shirikisho la Azam umefanyika leo Ijumaa Machi 2, 2018 kwenye Makao Makuu ya Azam Tv.

Droo hiyo imehusisha timu saba za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na timu moja ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.

Timu zilizochezeshwa kwenye droo hiyo ni Young Africans,Azam FC,Singida United,Tanzania Prisons,Njombe Mji,Stand United,JKT Tanzania na Mtibwa Sugar.



Thursday, March 01, 2018

RAIS WA FIFA AIMWAGIA SIFA TANZANIA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA Ndugu Gianni Infantino amemshukuru Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) Ndugu Wallace Karia kwa kazi nzuri ya maandalizi ya mkutano wa FIFA wa maendeleo ya mpira (FIFA Football Executive Summit) uliofanyika Februari 22, 2018 Dar es Salaam,Tanzania.

Infantino amesifia mapokezi na maandalizi yaliyofanywa na TFF katika mkutano huo mkubwa uliofanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini.

Katika barua yake aliyomuandikia Rais wa TFF Ndugu Karia ,Infantino amesema wameondoka na kumbukumbu zisizosahaulika kuhusu Tanzania ikiwemo urafiki uliojengeka wakati wote waliokuwepo Tanzania.

Aidha Infantino ameshukuru kwa chakula cha usiku kilichoandaliwa kwenye mgahawa wa Cape Town Fish Market lakini pia kwa kukutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Kassim Majaliwa.



Tuesday, February 27, 2018

TFF YAWATAJA WATAKAOCHEZESHA MECHI YA SIMBA NA YA YANGA

SIMBA YAPANGIWA WAAMUZI WA AFRICA KUSINI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Africa (CAF) imewapanga waamuzi kutoka nchini Africa Kusini kuchezesha mchezo wa Kombe la Shirikisho Barani Africa Simba ya Tanzania itakapocheza na El Masry ya Misri Machi 7,2018 Uwanja wa Taifa saa 10 kamili jioni.

Mwamuzi wa kati atakuwa Thando Helpus Ndzandzeka akisaidiwa na Zakhele Thusi Siwena mwamuzi msaidizi namba moja na Athenkosi Ndongeni mwamuzi msaidizi namba mbili wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Christopher Harrison na kamishna wa mchezo huo Tuccu Guish Chrbremedhin kutoka Eritrea.

Mchezo wa marudiano utachezwa huko Port Said Machi 17, 2018 utachezeshwa na waamuzi kutoka Eritrea .

Mwamuzi wa kati kati atakuwa Yonas Zekarias Ghetre akisaidiwa na Angesom Ogbamarian mwamuzi msaidizi namba moja na Yohannes Tewelde Ghebreslase mwamuzi msaidizi namba mbili wakati mwamuzi wa akiba atakuwa Yemane Asfaha Gebremedhin na kamishna wa mechi hiyo anatoka Libya Gamal Salem Embaia.

YANGA KUCHEZESHWA NA WAAMUZI KUTOKA BURUNDI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Africa(CAF) limewataja waamuzi kutoka Burundi kuwa ndio watachezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Africa kati ya Yanga ya Tanzania na Township Rollers FC ya Botswana utakaochezwa Machi 6,2018 kwenye Uwanja wa Taifa saa 10.30 jioni.

Mwamuzi wa kati atakuwa Pacifique Ndabihawenimana akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Willy Habimana na mwamuzi msaidizi namba mbili Pascal Ndimunzigo wakati Kamishna wa mchezo huo anatoka Swaziland Mangaluso Jabulani Langwenya

Mechi ya marudiano itachezwa Machin 17,2018 nchini Botswana na itachezeshwa na waamuzi kutoka Morocco.

Mwamuzi wa kati kati atakuwa Redouane Jiyed akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Youssef Mabrouk na mwamuzi msaidizi namba mbili Hicham Ait Abou ,mwamuzi wa akiba Samir Guezzaz na kamishna wa mchezo huo anatoka Africa Kusini Gay Makoena.




Tuesday, February 13, 2018

SERIKALI, TFF NA WAHARIRI WA MICHEZO WAJADILI UJIO WA MARAIS WA FIFA NA CAF


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe (kushoto) akizungumza na Wahariri wa Habari za Michezo kutoka vyombo mbalimbali nchini (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu utaratibu wa ujio wa Rais FIFA na CAF nchini mwezi huu kwa ajili ya kufanya mkutano wa kujalili agenda za mkutano mkuu wa FIFA,na Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw.Yusuph Singo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.


 Mjumbe wa CAF na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa Bw.Leodger Tenga (katikati) akizungumza na Wahariri wa Habari za Michezo kutoka vyombo mbalimbali nchini (hawapo pichani) kuhusu mambo ambayo uongozi wa FIFA utapenda kujua katika soka la Tanzania ambapo moja wapo ni Maendeleo ya Soka la Wanawake,Kushoto ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe na Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw.Yusuph Singo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo.


MAAMUZI KAMATI YA SAA 72 LIGI KUU YA VODACOM, JUMLA YA FAINI MILIONI 3.6


Mechi namba 122 (Lipuli 0 vs Yanga 2). Klabu za Lipuli na Yanga kila moja imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kutumia milango isiyo rasmi kuingia uwanjani, kitendo ambacho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(14) ya Ligi Kuu. Adhabu dhidi yao imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. 

Pia klabu ya Yanga imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kutoingia vyumbani, hivyo kwenda kinyume na Kanuni ya 14(13) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo. Adhabu hiyo ni uzingativu wa Kanuni ya 14(49) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Mechi namba 123 (Singida United 3 vs Mwadui 2). Kocha wa makipa wa Mwadui, Lucheke Gaga amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) baada ya kuondolewa kwenye benchi (ordered off) na Mwamuzi kwa kutoa lugha ya matusi katika mechi hiyo iliyofanyika Februari 3, 2018 kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 40(11) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.

Mechi namba 128 (Ruvu Shooting 0 vs Simba 4). Mchezaji wa Ruvu Shooting, Mau Bofu amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kumpiga kiwiko Emmanuel Okwi wa Simba katika mechi hiyo iliyofanyika Februari 4, 2018 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 37(3) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Wachezaji.

LIGI DARAJA LA KWANZA

Mechi namba 53 Kundi A (Kiluvya United 0 vs African Lyon 1). Klabu ya African Lyon imepigwa faini ya sh. 200,000 (laki mbili) kutokana na timu yake kutoingia vyumbani katika mechi hiyo iliyofanyika Februari 5, 2018 kwenye Uwanja wa Filbert Bayi mkoani Pwani.

KAMATI YA NIDHAMU YAMFUNGIA JUMA NYOSO

Kamati ya Nidhamu iliyokutana Jumamosi Februari 10, 2018 pamoja na mambo mengine pia ilipitia shauri la mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyoso lililofikishwa kwenye kamati akituhumiwa kwa utovu wa nidhamu kwenye mechi namba 112 ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Kagera Sugar dhidi ya Simba Sports Club iliyochezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba.

Juma Nyoso alituhumiwa kumpiga shabiki baada ya kumalizika mchezo huo kinyume cha kanuni ya 36 ya ligi Kuu inayozungumzia uchezaji wa kiungwana pamoja na Ibara 50(1)(2) na (5) ya katiba ya TFF toleo la 2015.

Kamati ilipitia ripoti ya kamishna wa mechi ambayo imeeleza tukio hilo la Juma Nyoso kupishana na shabiki aliyekuwa amebeba vuvuzela na ndipo Nyoso aliposimama na kuanza kumpiga na kiatu na kutumia goti mpaka askari wa jeshi la Polisi walipoingilia kumuokoa na kumshikilia mchezaji huyo wakati shabiki akipatiwa huduma kwenye gari la huduma ya kwanza.



Monday, November 06, 2017

MAKAMU WA RAIS AVUTIWA NA MATEMBEZI YA HISANI JIJINI DSM








Lengo la matembezi hayo ni kusaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kugharamia mafunzo ya wauguzi wakunga nchini.



Saturday, October 21, 2017

MWALIMU COMMERCIAL BANK, YASHIRIKI BONANZA YA WALIMU WA MICHEZO


NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

TIMU ya soka ya wafanyakazi wa Mwalimu Commercial Bank,(MCB), plc, imefungwa mabao 3-1 na kikosi mchanganyiko cha walimu wa jijini dar es salaam, katika pambano la kirafiki ikiwa ni sehemu ya mafunzo ya wiki moja ya walimu wa michezo yaliyofanyika chuo kikuu cha dar es salaam.

Pambano hilo lililopigwa kwenye uwanja wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, leo Oktoba 21, 2017, haikuwa kazi rahisi kwa kombaini ya walimu kushinda mchezo huo dhidi ya “mabenker” hao wa MCB, kwani hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, timu zote zilitoka sare ya bao 1-1.

Katika kipindi cha pili tena dakika za lala salama, wafanyakazi wa MCB walielemewa na kujikuta wanatundikwa mabao mawili ya haraka haraka.

Hata hivyo kocha wa MCB, Lufingo Mwakilasa, aliwasifu wachezaji wake kuwa wamejitahidi kucheza vizuri licha ya hali ya hewa kuwa mbaya (joto kali), lakini pia asili ya kazi yao ambayo muda mwingi huwa wanautumia wakiwa maofisini kuhudumia wateja ukilinganisha na wenzao ambao ni walimu wa michezo na muda mwingi huwa wanafanya mazoezi.



Saturday, October 14, 2017

MECHI KATI YA EFM SPORT NA MWANZA VETERANS, NI MAGOLI MENGI TU

Ni kwenye mchezo wa kirafiki baina ya EFM Vs Mwanza Veterans!

BMG


TAMASHA LA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA ARUSHA KUFANYIKA KESHO

PICHANI: Kulia ni Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma katikati ni Mwenyekiti wa TASWA Arusha, Jamila Omar akioongea na waandishi wa habari

Na Woinde Shizza,Arusha

Tamasha la waandishi wa habari, kanda ya kaskazini, linatarajiwa kufanyika jumapili, octobar 15 katika uwanja wa General Tyre ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Katika tamasha hilo, ambalo litashirikisha wanahabari zaidi ya 500, kutoka mikoa ya Arusha, Tanga, Manyara na Kilimanjaro,limedhaminiwa na shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA) Mifuko ya hifadhi ya Jamii ya LAPF na PSPF, Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, kampuni ya vinywaji baridi ya Coca cola na kampuni ya ya vinywaji baridi ya SBC (T) Limited na Palace Hoteli.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma, alisema tamasha hilo, limeandaliwa na TASWA kwa kushirikiana na kampuni ya Arusha media na maandalizi yote yamekamilika.


Thursday, September 28, 2017

RAIS WA TFF ATEMBELEA KIWANDA CHA BIA CHA SERENGETI BREWERIES


Rais wa TFF ,Wallace Karia akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani alipofanya ziara katika Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars.pembeni yake kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Helene Weesie na kulia ni Mkurungezi wa masoko wa SBL Ceaser Mloka na mwishoni ni Kocha mkuu wa Taifa stars Salum Manyanga,Mapema jana katika ofisi za makao makuu ya SBL Temeke Jijini Dar es salaam.


Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Helene Weesie akifurahia jambo na Rais wa TFF ,Wallace Karia na Mkurungezi wa masoko wa SBL Ceaser Mloka wakati uongozi wa TFF ulipotembelea kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars. 

Dar es Salaam, Septemba 27, 2017. 

Uongozi mpya wa Shirikisho la Soko Tanzania (TFF) ukiongozwa na Rais wake Wallace Karia, leo umetembelea Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars. 

Ziara hii imefanywa na uongozi mpya wa TFF ikiwa ni wiki moja kabla ya mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayozikutanisha Taifa Stars na Malawi, mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam. Tangu imepata udhamini wa SBL mwezi Mei mwaka huu, Taifa Stars imecheza mechi nne za kimataifa na kufanikiwa kuweka rekodi nzuri kwenye mechi zote ilizocheza. 


Monday, August 28, 2017

HIZI NDIO MECHI KUBWA ZA WATANI WA JADI BARANI AFRIKA


Na Jumia Travel Tanzania

Miongoni mwa matukio yanayosisimua zaidi kwenye mchezo wa soka ni mipambano ya watani wa jadi. Katika nchi nyingi barani Afrika ukiwauliza kwa harakaharaka mashabiki wengi wa soka ni mechi zipi huwa wanazisubiria sana utawasikia wanakutajia michezo kama vile Real Madrid na Barcelona, Manchester United na Manchester City, Inter Milan na AC Milan, Liverpool na Manchester United, Chelsea na Arsenal au Bayern Munich na Borussia Dortmund.

Kutokana na umaarufu wa soka la nchi za Ulaya imekuwa ni rahisi kwa mechi zao kufuatiliwa kwa urahisi ukilinganisha na huku Afrika. Lakini hiyo haimaanishi kwamba bara la Afrika nalo halina michezo ya namna hiyo ambayo ikiwa inakaribia homa miongoni mwa mashabiki huwa juu kuliko kawaida.

Wednesday, August 23, 2017

MSHINDI WA MZUKA JACKPOT AKABIDHIWA MILIONI 80 DAR ES SALAAM LEO


PICHANI: Balozi wa Mchezo wa Bahati Nasibu wa Tatu Mzuka, Mussa Hussein (kulia), akimkabidhi mfano wa hundi ya thamani ya shilingi milioni 80 Mshimdi Mkuu wa Mchezo huo, Rashid Ally katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Regence Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mwakilishi kutoka Baraza la Michezo ya Bahati Nasibu Tanzania, Abdallah Hemed.

Na Dotto Mwaibale

MSHINDI Mkuu wa mchezo wa bahati nasibu ya Tatu Mzuka , Rashid Ally, leo amekabidhiwa sh.milinoni 80 alizojishindia katika droo kubwa iliyochezwa Jumapili.

Rashid ambaye alijishindia kiasi hicho cha fedha katika mchezo huo wa Tatu Mzuka, alionyesha kutoamini, huku akiwa na furaha na shukrani baada ya ushindi huo wa kihistoria. Rashid, ambaye ana umri wa miaka 21 tu, anaishi na familia yake maeneo ya Temeke, Dar es Salaam.

Akizungumzia ushindi wake, Rashid ambaye amemaliza kidato cha nne hivi karibuni, alisema kuwa alikuwa anacheza angalau mara 4 hadi 6 kwa wiki kwa kutumia pesa aliyokuwa anaipata katika shughuli zake za kila siku.

'Ndoto yangu ni kujenga nyumba, na kuwekeza katika kilimo, kitu ambacho nitafanya kwa kushirikiana na mama pamoja na Baba yangu. Nia yangu ni kuikuza iwe ni biashara kubwa ' alisema Rashid.


Tuesday, August 22, 2017

RIDHIWANI KIKWETE AKABIDHI ZAWADI ZA WACHEZAJI BORA NDONDO CUP

 Mbunge wa Chalinze Ridhiwani  Kikwete akizungumza na familia ya Wanamichezo wakati wautoaji wa Tunzo za Mchezaji borawa michuano ya Ndondo Cup inayoandaliw ana kampuni ya CloudsMedia Group kupitia kipindi chake cha Sports Extra
  Mbunge wa Chalinze Ridhiwani  Kikwete, akikabidhi tunzo ya Mchezaji bora kwa kocha wa timu ya Misosi FcYenye maskani  yake Manzese


Thursday, August 10, 2017

KAMPUNI YA NETWORK LTD YAZINDUA DROO KUBWA YA MILIONI 60


PICHANI:Mratibu wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Sebastian Maganga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo Pichani) kuhusiana na mchezo wa bahati nasibu ya Tatu Mzuka, wakati wa uzinduzi wa mchezo huo wa kubahatisha nchini mapema jijini Dar es salaam (picha na ImmaMatukio Blog)

Na Mwandishi Wetu

Tatu Mzuka ni mchezo mpya wa jackpot uliobuniwa mahsusi kubadilisha maisha ya watu. Tatu Mzuka ni rahisi kucheza kwa kutumia simu ya mkononi, na kushinda ni baada ya kila lisaa limoja baada ya kucheza.

Kucheza Tatu Mzuka unahitaji kuchagua namba zako tatu za bahati, kati ya 0 na 9 kwa kufanya muhamala kwenye simu ya mkononi, linganisha namba mbili ili kujiongezea nafasi ya kushinda mara mbili, au linganisha namba tatu na ushinde mara 200.