Thursday, November 26, 2015

RIPOTI YA RUSHWA BARANI AFRIKA KUZINDULIWA, TANZANIA PIA IPO

Transparancy International, inategemea kuchapisha utafiti unaoangalia maoni ya watu uzoefu na mtazamo wao kuhusu masuala ya rushwa katika nchi 28 barani Afrika.

Maandalizi ya ripoti hiyo iitwayo People and Corruption, Africa Survey 2015 Global Corruption Barometer Transparency International imeungana na Afrobarometer, walioongea na watu wasiopungua 43,143, katika nchi 28 katika nchi zilizoko pembezoni mwa jangwa la Sahara.

Kwa mujibu wa African Press Organisation, shirika la Transparency International litachapisha utafiti huo tarehe 1/12/2015, unafuatia ule uliopita uliojulikana kama Global Curruption Barometer, uliochapishwa mwaka 2013

No comments:

Post a Comment