Tuesday, November 24, 2015

RC KILIMANJARO AKUTANA NA MAOFISA WA MANISPAA KUJADILI HOFU YA KIPINDUPINDU



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Amosi Makala akiwa katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi,kuzingumza na watendaji wa Afya na Mazingira.




Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Amosi Makala akifurahia jambo mara baada ya kukutana na watendaji wa Halmashauri kuzungumzia juu ya hofu ya Ugonjwa hatari wa Kipindupindu.kushoto kwake ni kaimu mkurugenzi wa Manispaa hiyo Jeshi Lupembe.







Baadhi ya watendaji.







Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Novatus Makunga akiwa na mmoja wa maofisa wakifuatilia maelelzo yaliyokuwa yakitolewa ofisini hapo.









Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Amos Makala akizungumzia changamoto iliyojitokeza hivi karibuni ya kujaa kwa dampo la kutupa taka hali iliyosababisha mrundikano wa takataka katika maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi,Hapa alikuwa akitoa agizo taizo hilo kushughulikiwa mara moja.







Baada ya agizo hilo mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga alifanya ziara katika dampo lilopo Kaloleni kujinea tatizo lililosabaisha magari ya kubeba taka kushindwa kuendelea na zoezi hilo.









Katapila likijaribu kusawazisha takataka katika eneo hilo la dampo ili kurahisisha utupwaji wa taka katika eneo hilo.









Wakati zoezi la kurekebisha barabara katika eneo la dampo likiendelea,mmoja wa wananchi kkatika eneo hilo alikuwa na shughuli ya kujiokotea vitu ambayo anadhani vitamsadia katika kujipatia kipato.









Mifugo aina ya Mbuzi pia wamekuwa wakifanya eneo hilo la dampo kama sehemu ya kujipatia chakula.









Wafanyakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakizoea taka zilizokuwa zimerundikana katika eneo la jirani kabisa na soko la Manyema mjni hapa.











Shughuli ya uzoaji taka ikiendelea.







Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Novatus Makunga akizungumza namna ambavyo utekelezaji wa agizo la mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro lilivyoanza ikiwa ni njia moja wapo ya kukabiliana na Ugonjwa hatari wa Kipindu pindu.









Hivi ndiyo hali iliyokuwa katika soko la MANYEMA.









DC Makunga akijionea hali halisi.







Moja ya dampo likiwa limejaa taka.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.





No comments:

Post a Comment