Wednesday, July 31, 2013

YANGA YAITOSA AZAM MEDIA

 Uongozi wa timu ya Yanga ukizungumza na waandishi wa habari pamoja na wanachama (hawapo pichani) juu ya tamko la yanga kukataa mechi zao zisirushwe na Azam Media
Wanachama wa timu ya Yanga wakishangilia tamko hilo la kukataza mechi zao kurushwa kwenye Azam Media

ZIMBAMBWE WAPIGA KURA LEO



Raia wa Zimbabwe wanapiga kura katika uchaguzi wa Urais unaotajwa kuwa na ushindani mkali huku kukiwa na madai ya udanganyifu. Rais Robert Mugabe wa miaka 89 amesema atang'atuka ikiwa yeye na chama chake cha Zanu-PF watashindwa.

Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai na chama chake cha Movement for Democratic Change (MDC) wamelalamikia Zanu-PF kwa kuhitilafiana na utaratibu wa uchaguzi ili kunyakua ushindi, lakini chama tawala kimekanusha madai hayo.Shughuli za kampeini zimekua ghasia zozote huku kukiwa na visa vichache sana vya kuwatisha wapiga kura.

ANGELINA JOLIE ATAJWA KULIPWA ZAIDI DUNIANI


Ingawa hajatoa filamu tangu mwaka 2010 iliyokuwa inajulikana kwa jina la 'The Tourist' muigizaji wa kimataifa Angelina Jolie ametajwa kuwa mwigizaji wa kike anayelipwa fedha nyingi zaidi duniani.

Jolie ametajwa na mtandao wa Forbes kupitia ripoti yake kuwa katika kipindi cha mwezi June mwaka jana na june mwaka huu ameingiza kiasi cha dola milioni 33 ambazo ni zaidi ya sh. bilioni 48 za kitanzania.


MAGAZETI LEO





Tuesday, July 30, 2013

KIKONGWE CHAMBAKA MWANAFUNZI DARASA LA TANO

MWANAFUNZI wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 11 katika Shule ya Msingi Mjini Musoma, anadaiwa kufanyiwa  kitendo cha kinyama kwa kubakwa na kujeruhiwa vibaya katika sehemu zake za siri na babu wa miaka 65 mkazi wa mtaa wa Kawawa katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara.

Wakizungumza wakiwa nje ya Hospitali ya Mkoa wa Mara, baada ya kumpeleka mtoto huyo kupata matibabu, wazazi wa mtoto huyo majina yanahifadhiwa  wakiwemo majirani na viongozi  wa Kataya Mwigobero, walisema mtoto huyo amefanyiwa kitendo hicho cha kikatili kwakudanganywa kupewa sh. 1,000 kila siku na mzee huyo kabla ya kufumaniwa na mmoja wa Askari Polisi wa Kituo Kikuu cha mjini Musoma.


PINGA KORTINI ALHAMISI


KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimetangaza kumburuta Mahakamani siku ya Alhamisi asubuhi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwa kile kinachodaiwa amekaidi kufuta kauli yake ya kuruhusu vyombo vya usalama kupiga wananchi wanaokaidi amri za vyombo hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi na mwanasheria wa LHRC , Harold Sungusia, alisema wanamfungulia shtaka Waziri Mkuu Pinda, kesi ya kimkakati inayomlazimu ajibu mbele ya mahakama msimamo wa serikali unaomsababisha atoe kauli hiyo.


NANDO AWASILI TANZANIA


Aliyekuwa mshiriki wa shindano la Big Brother Nando amewasili leo nchini baada ya kutolewa kwenye shindano hilo kwa kuonekana hastahili kuendelea kukaa ndani ya jumba hilo baada ya kukiuka baadhi ya sheria.

MWISHO MWAMPAMBA AGEUKIA CLOUDS FM?





KESI YA JAYDEE YAPIGWA KALENDA TENA

 MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, leo imeiaharisha kesi inayomkabili msanii wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura 'Lady Jaydee' a.k.a Annaconda dhidi ya uongozi wa Clouds Media Group hadi Agosti 2, mwaka huu.

Kesi hiyo ya madai iliyopo mbele ya Hakimu Athumani Nyamlani, leo ililetwa kwa ajili ya kusikilizwa lakini ilishindikana kutokana na wakili anayemtetea, Jaydee kutotokea mahakamani hapo na kumtuma mwakilishi wake.


Monday, July 29, 2013

MBUNGE AJISALIMISHA POLISI


MBUNGE wa Jimbo la Kinondoni, jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya CCM, Idi Azzan, amejilisalimisha' polisi na kutaka jeshi hilo, kufanyia uchunguzi tuhuma za kuhusishwa na biashara za dawa za kulevya na iwapo itabainika anahusika, hatua za kisheria zichukue mkondo wake.

Mbunge huyo alifikia hatua hiyo jijini Dar es Salaam jana baada ya barua zilizoandikwa na watu wanaodai ni wafungwa wa Tanzania wanaotukia adhabu zao mjini Hong Khong, nchini China, kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimhusisha yeye (Azzan) kuwa amekuwa akifanya biashara hiyo akiwatumia vijana hao. Wafungwa hao wanadaiwa kuwa wanatumikia adhabu zao baada ya kupatikana na makosa ya dawa za kulevya.


TRUST - UPCOMMING ARTIST ON HIPHOP


STAY TUNED FOR MORE INFO

MBUNIFU DIANA MAGESA ALIPOFANYA SHOW PARIS

Sehemu ya show ya mbunifu maarufu kutoka Tanzania, Diana Magesa iliyofanyika Paris, Ufaransa hivi karibuni. Imma Matukio itaendelea kukuletea designs mbalimbali za show hiyo, keep it locked

AIRTEL YAFTURISHA WATEJA








Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (kushoto) akimkaribisha Ofisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya NMB, Waziri Barnabas katika hafla ya futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja wao jijini Dar es Salaam jana.
 






Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa pili kushoto) akiwakaribisha baadhi  ya wateja wao katika hafla ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Mallya.



MOXIE ASAFIRISHA ABIRIA BURE JIJINI


MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, anayeunda kundi la Wateule, Taikuni Ally 'Moxie' jana amejitolea kuwasafirisha abiria bure kwenye maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Moxie amejikuta akisukumwa kuwasafirisha abiria maeneo mbalimbali ikiwa ni sehemu moja wapo ya kurudisha kwa jamii, kutokana na kile anachokifanya.



DIAMOND AENDA KUSOMA AFRIKA KUSINI

Hatimaye msanii anayetamba kwenye gemu la muziki wa kizazi kipya nchi, anayeongoza kwa shoo Diamond Platinum amua kujikita darasani kwa kuongeza elimu.

Kupitia ukurasa wake wa FB msanii huyo alijalibu kutupia swali kwa mashabiki wake kuwa wahisi ameenda kusomea fani gani?


AJALI YA BASI YAUWA 38 ITALY



Waokoaji kusini mwa Italy wamesema kuwa takriban watu 38 wameuawa baada ya basi moja waliokuwa wakisafria kutumbukia mita thelathini ndani ya mtaro.Abiria wengine walipelekwa hospitalini wakiwa na majeraha mabaya.

Hatahivyo haijabainika kiini cha ajali hiyo iliohusisha magari kadhaa.Basi hilo lilikuwa limebeba abiria waliokuwa wakirudi mjini Napoli kutoka jimbo la kusini la Campania.Basi hilo liligonga magari kadhaa kabla ya kuanguka ndani ya mtaro mjini Avellino.

Takriban watu 10 wamejeruhiwa baadhi wakipata majeraha mabaya sana, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Italia.Basi hilo liliwa limewababa abiria hamsini ikiwemo watoto waliokuwa wanarejea Naples baada ya kufanya hija.

Sunday, July 28, 2013

WATANZANIA WALIOFUNGWA HONGKHONG WATAJA VIGOGO KUHUSIKA




WATANZANIA WAKAMATWA NA DAWA ZA KULEVA HONG KONG


WATANZANIA watatu wanadaiwa kukamatwa nchini mjini Hong Kong nchini China  wakisafirisha dawa za kulevya zenye thamani ya sh. bilioni moja. Dawa hizo zimetipotiwa kuhifadhiwa katika kitengo cha madawa ya kulevya nchini humo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao wa serikali ya Hong Kong, maofisa wa ushuru wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Hong Kong(HKIA) walimkamata kijana wa miaka 26 ambaye ni abiria kutoka Tanzania juzi mchana akiwa amebeba kilo 1.6 za dawa aina ya heroine zikiwa kwenye sanduku lake la mkononi (briefcase).


Saturday, July 27, 2013

JENGO PACHA HALIVUNJWI KWA SASA

 JENGO LILIAMRIWA KUVUNJWA LILOKO KARIBU NA JENGO LILIPOROMOKA NA KUUA KUTOVUNJWA

 Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imesema hatma ya jengo la ghorofa 16 (pichani) lililoko mtaa wa Indira Gandhi na Asia lililoamriwa kuvunjwa na Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, haijaeleweka kwa sababu Mahakama imeweka zuio la kuvunjwa kwa jengo hilo.

Kwa mujibu wa Afisa Uhusiano wa Manispaa ya Ilala Tabu Shaibu " haitawezekana kuvunjwa jengo hilo kwa sasa kwa sababu mmiliki wa jengo hilo, Bw. Rada Damji amefungua kesi ya kupinga amri hiyo"

"Kwa sasa kesi iko mahakamani, mmiliki kapewa zuio la kuvunja," aliongeza Shaibu.


JAY Z 'AMDATISHA' BEYONCE


Rapa wa kimataifa Jay Z adhihirisha jinsi gani anavyompenda mke wake Beyonce, baada ya kushindwa kuvumilia na kumvamia juu ya stage ya Philadelphian Alhamisi usiku na kumkumbatia

KALA AMPIGIA DEBE LOWASA


Mimi Kala Jeremiah nilikuwa msanii wa kwanza tanzania kumsema mheshimiwa Edward Lowasa kupitia wimbo wangu uitwao wimbo wa taifa baada ya mheshimiwa kukumbwa na kashfa ya ufisadi wa Richmond.
Kwa kipindi kile kila mmoja wetu alihamaki sana na kuona kweli mzee wa watu ni fisadi. Kwenye wimbo huo kuna mistari nilisema. Mi siyo mwana siasa sisubiri tume ichunguze nistaafu ka Lowasa.

Kwa kuwa mimi ni mzuri sana kwenye kufanya uchunguzi binafsi nilitumia muda mwingi sana kulichunguza swala hili la kashfa hii na baadae niligundua kuwa ni swala la kisiasa.

Na yalikuwa ni mapito ambayo mwanadamu yoyote hupewa muda wa kupitia magumu ili kupimwa imani yake kwa mungu.

Baada ya kugundua hayo mwaka jana nilitengeneza wimbo unaoitwa azimio la arusha ambao upo kwenye album yangu ya pasaka ambayo iko sokoni tokea mwaka jana. Katika wimbo huo wa azimio la arusha niliandika mistari ifuatayo.
Walipiga dili waka msakizia Lowasa ili kuficha siri kali.niliandika mstari huu baada ya kufanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa mheshimiwa ni kiongozi bora sana na hasa kwa uamuzi wake wa kujiuzulu bila shinikizo kubwa na wakati kwa nafasi aliyokuwa nayo ya uwaziri mkuu alikuwa na uwezo wa kugoma kujiuzulu na hasa kwa kuwa hakuwa fisadi kama ilivyosemwa.

Mwezi wa tatu mwishoni mwaka huu nilitoa wimbo unaokwenda kwa jina la karibu Dar ambako nilisema Dar Es Salam ingekuwa nchi rais angekuwa Lowasa huku watu washashtukia kuna mchezo kwenye siasa hapa nilikuwa namaanisha kuwa watu wengi wanaoishi dar wanawahi kujua mambo ya wanasiasa kwa kuwa wanasiasa wanaishi huku lakini pia watafiti wengi wa mambo ya kisiasa wanaishi huku kwa hiyo ni rahisi zaidi kuujua ukweli mapema.



Friday, July 26, 2013

PAPISS CISSE KIMEELEWEKA

Mzozo kati ya Cisse na klabu yake umetatuliwa


Papiss Cisse
Papiss Cisse na wasimamizi wa klabu ya Newcastle hatimaye wameafikiana na sasa mchezaji huyo ataanza kuvalia sare rasmi ya klabu hiyo iliyo na nembo ya kampuni ya Wonga, licha ya msimamo wake wa kidini.
Cisse, ambaye ni Muislamu, alijiondoa kutoka kwa kikosi cha Newcastle kilichokwenda ngambo kwa mazoezi yake ya klaby ya msimu kuanza, baada ya kuwafahamisha wasimamizi wa klabu hiyo kuwa hakuwa tayari kuvalia sare ambayo inaendeleza kampuni ya kutoa mikopo.
Lakini baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa muda wa wiki moja, pande hizo mbili zimeafikiana na Cisse sasa ataendelea kuichezea klabu hiyo.



MAAFISA WA SOKA KENYA 'UFISADI'


Bendera ya Kenya
Wakuu wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Kenya FKF, wanachunguzwa na maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi kuhusiana na madai ya kutoweka kwa mamia ya maelfu ya dola pesa za shirikisha hilo.

Kwa mujibu wa maafisa hao, fedha zilizo zilitolewa na shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA na mashirika mengine.

Afisa mkuu wa uhusiano mwema wa tume hiyo, Yasin Ayila, amesema, tume hiyo imepokea malalamishi kuwa maafisa hao wametumia vibaya zaidi ya dola laki nne, mali ya FKF.


MBAKAJI SUGU AFRIKA KUSINI AFARIKI

Mwanamume anayetuhumiwa kuwa mbakaji sugu nchini Afrika Kusini ,Sifiso Makhubo, amepatikana akiwa amefariki katika chumba chake gerezani.

Sifiso Makhubo, aliyekuwa anakabiliwa na mashtaka 122 ikiwemo mauaji na ubakaji alipatikana akiwa amejinyonga kwa blanketi.

Baadhi ya makosa aliyoshtakiwa nayo ni pamoja na kuwaambukiza wasichana  virusi vya HIV

Afrika Kusini ina moja ya visa vingi zaidi vya ubakaji duniani, huku polisi wakionyesha kuwa ni visa 64,000 pekee ambavyo viliripotiwa mwaka jana.

Maafisa wanasema kuwa alikuwa peke yake katika selo yake , lakini wanachunguza kilichosababisha kifo chake.

Bwana Makhubo anatuhumiwa kwa kuwabaka watoto 35 na wanawake wawili, kati ya Januari mwaka 2006 na Februari 2011. Hadi sasa uchunguzi uliofanywa wa DNA katika waathiriwa waliodai kubakwa naye, ulithibitisha kuwa yeye ndiye alikuwa mbakaji.

HALI YA MMILIKI WA HOME SHOPING CENTER

Mfanyabiashara Mmiliki wa Home Shopping Center (HSC), Said Mohamed Saad (Pichani), aliyemwagiwa tindikali wiki iliyopita katika shopping mall mpya ijulikanayo kama Msasani City Mall, jijini Dar es Salaam, yuko katika matibabu Afrika Kusini.

Bw. Saad alimwagiwa tindikali ikiwa ni kiasi cha wiki mbili tangu Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Said Juma Makamba naye ajeruhiwe vibaya usoni kwa kumwagiwa tindikali usiku nyumbani kwake.

Kumwagiwa tindikali sio jambo jipya nchini kwani ndani ya miaka miwili pekee, watu zaidi ya watano wameshamwagiwa tindikali nchini.

Vyombo vya habari nchini viliripoti wiki iliyopita tukio la mfanyabiashara huyo kumwagiwa tindikali ikiwa ni tukio lililotokea ijumaa tarehe 19 julai, ambapo saa moja jioni, mfanyabiashara Said Mohammed Saad alimwagiwa tindikali na mtu mmoja ambaye hakufahamika na mara,

Mhusika alikimbia huku mlinzi wa eneo hilo alimkimbiza lakini hakufanikiwa kumkamata baada ya kuteleza na kuanguka. Hatua hiyo ilimwezesha mtuhumiwa kutoroka eneo la tukio kwa kutumia pikipiki.

Wednesday, July 24, 2013

WATU 1,500 WAATHIRIKA NA MSHTUKO WA MOYO


Zaidi ya watu 1,500 waathirika na mshtuko wa moyo ulio sababishwa na kushindwa kula kitu chochote asubuhi (kiamsha kinywa) , kulingana na utafiti uliofanywa nchini Marekani.

Utafiti wao uliowahusisha wanaume 27,000 ulionyesha kuwa wale wasiokula kiamsha kinywa wako katika hatari ya kupata matatizo ya moyo.

Kikundi hicho cha wataalamu katika chuo kikuu cha Havard kitivo cha afya ya umma,kilisema kuwa kukosa kiamsha kinywa kunasababisha mwili kutumia nguvu nyingi zaidi kuliko kawaida.


HALI MBAYA MISRI

Muslim Brortherhood kinalaumu maafisa wa usalama kwa utovu wa usalama Watu waliokuwa wamejihami nchini Misri wamewaua kwa kuwapiga risasi wafuasi wawili wa rais aliyeondolewa mamlakani Mohamed Morsi.

Wawili hao walikuwa njiani kuungana na wafuasi wengine wa Morsi waliopiga kambi nje ya msikiti mmoja mjini Cairo.

Chama cha Muslim Brotherhood, kinachomuunga mkono Mosri, kimelaumu maafisa wa usalama kwa utovu wa usalama , lakini mwandishi wa BBC mjini Cairo anasema madai haya ni vigumu kuyathibitisha.

Kaskazini mwa Cairo, katika mtaa wa Mansoura,bomu lililipuka nje ya ofisi za polisi na kuwajeruhi maafisa kadhaa wa polisi pamoja na raia.

Kuna ripoti kuwa mtu mmoja alifariki.




RWANDA YASAIDIA WAASI M23


Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limeikosoa serikali ya Rwanda na kusema kuwa,  serikali ya Kigali imekuwa ikiwaunga mkono waasi wa M23 wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Taarifa ya Human Rights Watch imeongeza kuwa, Rwanda ingali inawaunga mkono waasi hao wa M23 ambao wamehatarisha usalama katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Hii si mara ya kwanza kwa Rwanda kutuhumiwa kwamba, imekuwa ikiwaunga mkono waasi wa M23; tuhuma ambazo imekuwa ikizikanusha mara kwa mara.

Hayo yanajiri katika hali ambayo, serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewatuhumu waasi wa M23 kuwa wametenda jinai za kuwauwa watu 13, kubaka wanawake 7 na kupora mali za watu wiki iliyopita katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo.

 Lambert Mende Omalanga Waziri wa Habari wa Kongo amesema kuwa, ushahidi unaonesha kuwa, kundi la M23 limefanya jinai kadhaa katika mji wa Kiwanja katika jimbo la Kivu Kaskazini.


KIKI YA RONALDO YAVUNJA MKONO MTOTO



 Mtoto wa miaka 11 ambaye ni shabiki wa soka amevunjika mkono wa kushoto baada ya kupigwa na mpira wa shuti kali alilopiga mchezaji maarufu duniani Cristiano Ronaldo.

Kwa mujibu wa mtandao wa habari wa televisheni ya Sky, kijana Charlie Silverwood amevunjika sehemu mbili katika mkono wake wa kushoto baada ya kiki hiyo ya umbali wa yadi 35.

Hata baada ya kuumia kijana huyo hakuwa tayari kuondoka uwanjani kwaajili ya matibabu ambapo timu yake ya Bournemouth ilipokuwa inacheza mechi ya kirafiki na Real Madrid jumapili na kubaki kwa kipindi cha dakika 84 zilizokuwa zimebaki.



WANUSURIKA KUMEZWA NA NYANGUMI



Tuesday, July 23, 2013

KIWANDA CHA SILAHA CHAKAMATWA DAR


JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam  limefanikiwa kumkamata  Charles Masunzu (30) mmliki wa kiwanda cha kutengeneza silaha mbalimbali za kienyeji kwaajili ya uhalifu.

Akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam Ally Mlege alisema Kukamatwa kwa mmiliki huyo ni baada ya kukamatwa kwa majambazi wanne huko maeneo ya Magoni ambao ni Matola Rashid (27), Omary Hasan(43), Martha Mhagama(32), na Mwasiti Maulid(22).


SONG : ZAHARA DESTINE



MWANAMKE ANUSURIKA KIMAAJABU

Asakari wa Zimamoto wakimsaidia dereva wa gari dogo lililopata ajali Kusini mwa China, baada ya kugonga roli kwa nyuma. Kushoto ni abiria aliyekuwa katika gari hilo kichwa chake kikiwa kimechomoza nje ya kioo cha mbele.

MKAZI mmoja mwanamke wa mjini Guizhou Kusini na China, ambaye hakuweza kufahamika jina lake amenusurika kufa katika ajali ya gari, lililokuwa limembeba huku akiwa hajafunga mkanda, baada kichwa chake kugonga kioo cha mbele ambacho kilimzuia asitoke nje ya gari hilo.

Abiria huyo na dareva wake walinusurika kimaajabu kufa kutokana na gari hilo kugonga nyuma ya lori lililokuwa mbele ya gari hilo na kichwa chake kugonga kioo hicho.


NEY AUMIZWA NA HALI DUNI KWA WANAWAKE


MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Ney wa Mitego amejikuta akitokwa na machozi, baada ya kukutana na mwanamke akiwa amewabeba watoto wawili wadogo huku akiendesha baiskeli mkoani Morogoro wilayani Ifakara.

Hali ilimkuta baada ya kumuona mama huyo, akiwa ametoka shamba akiwa amewabeba watoto wake wa kike wadogo, huku akiwa anaendesha baiskeli hiyo na ndoo ikiwa imening'inia mbele.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi msanii huyo alisema wazi kuwa ugumu wa maisha, unawaumiza wanawake na watoto wadogo ambao mara nyingi hawaelewi chochote kinachoendelea.


MSICHANA AIBA KADI YA BENKI KULIPIA GESTI.

msichana mwenye umri wa miaka 24 amehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela baada ya kuiba kadi ya benki ya mama yake na kutoa fedha alizotumia kulipia hoteli aliyolala na mtoto wa miaka 14.

Msichana huyu aliyetambulika kwa jina la Natalie Williams, mkazi wa Darlington, nchini Uingereza, alisema alilazimika kuiba kadi ya mama yake na kwenda kutoa pauni 1,000 (zaidi ya sh. milioni mbili ya kitanzania), ambapo aliweza kulipia hoteli yenye hadhi ya nyota nne alikolala na mtoto huyo.


SHEREHE JIJINI LONDON KUZALIWA MWANA WA MFALME


Tangazo la kuzaliwa kwa mwanamfalme
Ujumbe wa heri njema umeendelea kutolewa kutoka kote duniani baada ya Kate na Prince William ambaye atakuwa wa tatu kwenye foleni katika kurithi ufalme wa Uingereza.

Mwanamfalme William na mkewe Kate ,wameamkia hospitalini asubuhi ya leo mjini London baada ya kupata mtoto wao wa kwanzaJumatatu jioni.


Monday, July 22, 2013

HATIMA YA MASOGANGE KUJULIKANA AGOSTI 13

Hatimaye msanii anayeshiriki katika video za wasanii wa muziki wa bongo fleva, Agnes Jerald 'Masogange' na mwenzake Melisa Edward, waliokamatwa Afrika Kusini na dawa za kulevya teyari walishapanda kizimbani, na kesi yao inatarajiwa tena kusomwa 13 Agoust mwaka huu nchini humo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa aliweka wazi kuwa wanadada hao wawili teyari walishapandishwa kizimbani wiki iliyopita.

Alisema kuwa kutokana na ushahidi bado haujakamilika wadada hao wanatarajia kupanda kizimbani tena tarehe 13 mwezi Agoust mwaka huu.



Kamanda Nzowa aliweka wazi kuwa nchi zote mbili zinashirikiana kwa ajili ya kufanya upelelezi wa jambo hilo, hivyo anaamini kuwa kila jambo litaenda sawa.


MWINGEREZA MKENYA AWEKA REKODI

Mwendesha baiskeli mzaliwa wa Kenya ingawa raia wa Uingereza Chris Froome, anasema kuwa anatumai ushindi wake wa mashindano ya Tour de France utaweza kuwapa motisha vijana wa kiafrika.

Froome alishinda awamu ya miamoja ya mashindano ya Tour De France mnamo Jumapili akiwa anawakilisha Uingereza.



JIJI HILI LIMEFILISIKA



Jaji Rosemarie Aquilina wa jimbo la Ingham, Michigan Marekani ametoa hukumu kwa mujibu wa ibara ya 9 ya kufilisika kwa jiji la Detroit mwishoni mwa wiki iliyopita.
 SOMA ZAIDI


MJANE ATIMULIWA NJE



Hata kabla ya maziko askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa Darfur, Sudan hayajafanyika, mchumba wa mmoja wa wapiganaji hao, Amina Juma ameonja chungu nyingine baada ya kutimuliwa kwenye nyumba aliyokuwa akiishi na marehemu mwenza wake.

Amina ambaye inadaiwa kuwa alikuwa akiishi na Fortunatus Msofe aliyekuwa askari katika Kambi ya Msangani, 36KJ Pwani alisema jana: “Kumekuwa na mzozo wa hali ya juu na ndiyo maana tumeshindwa hata kufika Uwanja wa Ndege kuupokea mwili na hata kesho (leo) sidhani kama nitakwenda... kuna mtafaruku mkubwa wa kifamilia.”


MAGAZETI LEO





Sunday, July 21, 2013

KANYE WEST AMSHUKIA PAPARAZI


 Msemo unaosema kuwa Hasira hasara, msemo huo ulitaka kumpeleka pabaya muimbaji Kanye West pale alipokuwa ameamua kumsulubu mpiga picha mmoja .

Kanye West anaonekana kuwa na hasira na mapaparazi, hasira zake hizo jana zimemfanya amshambulie mmoja wao kwenye uwanja wa ndege wa LAX huku akitaka kumnyanga'nya camera.

Kutokana na kitendo hicho sasa Rapa huyo anashtakiwa kwa kesi ya jaribio la unyang'anyi


WAGONJWA WATIBIWA NJE MUHIMBILI

Inasemekana hii ndiyo hali ya Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ilivyo sasa baada ya kupisha zoezi la upulizwaji wa dawa ya kuua wadudu na mazalia yake katika wodi za wagonjwa za kibasila na Mwaisela 

Friday, July 19, 2013

KALA AJIPANGA KUACHIA 'NGOMA' MPYA



Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Kala Jeremiah awataka mashabiki wake kujiandaa kuipokea ngoma mpya ambayo anatarajia kuiachia hivi karibuni.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kala aliweka wazi kuwa baada ya mfungo wa mwenzi mtukufu wa ramadhani anatarajia kuachia nyimbo mpya ambayo itaendana na mazingira ya kipindi hicho.



RIHANNA ASHAMBULIWA NA CHIPS JUKWAANI


Kutokana na kitendo chake cha kuchelewa mara kwa mara kwenye shoo mwanadada Rihanna ajikuta yupo katika wakati mguu baada ya mashabiki kumwagia chipsi.

Mashabiki hao walionyesha kuchoshwa na tabia yake ya kuchelewa ovyo kwenye maonyesho yake,safari hii mashabiki hao walionekana kujipanga ili kuikomesha tabia hiyo ya mwanadada huyo kwa kumwagia chips jukwwani baada ya kuchelewa kufika katika onesho lake la Diamonds huko Manchester, Uingereza . onyesho hilo lilifanyika siku ya Jumanne wiki hii.


VIDEO : RIHANNA AKIWAJIBU MASHABIKI WAKE



MEZ B AFUNGUKA JUU YA KUFUNGA NDOA


BAADA ya baadhi ya washabiki wa muziki wa bongo fleva nchi kujiuuliza maswali mengi juu ya baadhi ya wasanii kushindwa kuoa pamoja na kupata watoto, msanii  wa muziki wa kizazi kipya nchini Moses 'Mez B 'Bushagama ameweka wazi sababu zinazopelekea baadhi ya wasanii hao kushindwa kuoa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, msanii huyo alisema kuwa mazingira wanayoishi ni miongoni mwa sababu inayopelekea kushindwa kupata mwanamke sahihi wa kutengeneza naye maisha.


KONDOMU DILI UGANDA

Nchi ya Uganda inakabiliwa na ukata wa kondomu, hali inayoleta utata juu ya ongezeko la kasi la maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Kwa mujibu wa mganga mkuu wa wilaya ya Masaka Dk. Stuart Musisi, aliweka wazi kuwa wilaya yake haijapewa kondomu kwa karibu miezi miwili sasa hivyo wilaya hiyo ipo kwenye hatari ya ongezeko la kusambaa magonjwa ya zinaa hususani ukimwi.


MAGAZETI LEO