Tuesday, December 31, 2013

RAIS KIKWETE AWATUMIA SALAMU ZA MWAKA MPYA WATANZANIA WOTE

SALAMU ZA MWAKA MPYA ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA WATANZANIA,

TAREHE 31 DESEMBA, 2013


Utangulizi
Ndugu zangu;
Watanzania Wenzangu;
                  Niruhusuni nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema, kwa kutujalia uzima mpaka kufika  na kuiona siku hii ya leo ya kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka 2014.  Wapo ndugu, jamaa na marafiki zetu wengi ambao hawakupata bahati tuliyoipata sisi kwa vile wametangulia mbele ya haki.  Tuendelee kumwomba Mola wetu awape mapumziko mema na azilaze roho zao mahali pema peponi. Ameen. 
Hali ya Usalama
Ndugu Wananchi;            
Tunaumaliza mwaka 2013 nchi yetu ikiwa salama na tulivu. Mipaka iko salama na ile hali ya wasiwasi tuliyokuwa nayo kwa nyakati fulani mwaka huu sasa haipo tena. Uhusiano wetu na majirani ni mzuri na tutaendelea kufanya kila tuwezalo kuhakikisha kuwa hali inaendelea kuwa hivyo au hata kuwa bora zaidi mwaka 2014 na daima dumu. 


HAWA NDIO WALIOWASILISHA MAJINA MPAKA SASA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taasisi mbali mbali za kijamii, vyama vya kitaaluma na vyama vya siasa vipatavyo 50 hadi leo, Jumanne, Desemba 31, 2013, vimewasilisha majina ya watu wao ambao vinapendekezwa wafiriwe katika kuteuliwa kuwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba.

Taarifa iliyotolewa leo mjini Dar Es Salaam na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa taasisi hizo zimewasilisha majina yao kwa mujibu wa mwaliko uliotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa makundi yaliyobainishwa katika Kifungu cha 22(1) (c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba (Sura ya 83).



RAIS KIKWETE AMUAPISHA IGP MPYA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Ernest Mangu katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpatia nyenzo za kazi baada yakumuapisha Naibu Inspekta Generali wa Polisi (IGP) mpya Afande Abdulrahman Kaniki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam jioni hii

ANGALIA PICHA ZAIDI...


MAGAZETI YA LEO TAREHE 31/12/13





Monday, December 30, 2013

MAKABIDHIANO: RASIMU YA PILI KATIBA MPYA KATIKA PICHA


ANGALIA PICHA ZAIDI...







HUYU NDIO IGP MPYA BADALA YA SAID MWEMA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatatu, Desemba 30, 2013, amemteua Kamishna wa Polisi Ernest Mangu kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.

Taarifa iliyotolewa usiku wa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa Kamishna Mangu anachukua nafasi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini anayestaafu, Saidi Mwema.

Kabla ya uteuzi wake unaoanza keshokutwa, Januari Mosi, 2014, Kamishna Mangu alikuwa Mkurugenzi wa Inteligensia ya Jinai (Director of Criminal Intelligence)katika Jeshi hilo la Polisi.

Aidha, taarifa hiyo inasema kuwa Rais Kikwete amemteua Kamishna Abdulrahman Kaniki kuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi, ambayo ni nafasi mpya katika muundo wa sasa wa Jeshi la Polisi.

Kabla ya uteuzi wake, Kamishna Kaniki alikuwa Kamishna wa Uchunguzi wa Kijinai (Commissioner for Forensic Investigations).

Mkuu wa Jeshi la Polisi mpya ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 31, 2013 katika Viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.


MARTIN KADINDA: KWELI MSG YANGU LAKINI HAZINA UHUSIANO NA TUKIO HILI

Mbunifu wa mavazi nchini, Martin Kadinda(KULIA) amekanusha kupokea ujumbe kutoka kwa mwanadada Jackie Clifford 'Cliff' FitzPartrick(KUSHOTO)  aliye kamatwa Desemba 19 mwaka huu kwa madai ya kusafirisha dawa za kulevya huko Macao nchini China.

Martin ambaye inadaiwa alishawahi kuwa meneja wa mwanadada huyo amekanusha uvumi wa kupokea ujumbe ambao umesambaa kwenye mitandao.

Ikiwa ni siku chache tangu kukamatwa kwa mwanadada huyo, ujumbe uliodaiwa kuandikwa na Jackie kama wosiwa kwa Kadinda, ulisambaa na kusababisha kuwa ndio majadiliano kwenye mitandao ya kijamii.
Ujumbe huo uliosomeka "Ikitokea nimekufa wosia Martin Kadinda ana maagizo yangu nini cha kufanya dont ask pls".


SCHUMACHER HOI HOSPITALI HAJITAMBUI




Aliyekuwa mshindi wa mashinano ya F1 Michael Schumacher, yuko kitandani anapambana kuokoa maisha yake baada ya kupata ajali mbaya na kusababisha majeraha makubwa kichwani wakati akiwa katika mchezo wa Skiing (mchezo wa majira ya baridi wa kuteleza kwenye barafu)

Kwa mujibu wa Daily Mail online, mshindi huyo wa mara 7 wa dunia katika mchezo wa F1(mashindano ya magari), alidondoka huko Meribel, eneo la mapumziko lililoko katika miinuko ya milima iliyoko Ufaransa

Vyanzo kutoka kwa madaktari vimeeleza kuwa Schumacher amepata matatizo kwenye ubongo. Schumacher mwenye umri wa miaka 44 aliteleza pembeni ya njia alipokuwa na mwanae wa kiume Mick mwenye umri wa miaka 14.

Michael alikuwa amevaa helmet ya kulinda kichwa alipopiga kichwa kwenye jiwe kubwa. Hata hivyo alikimbizwa kwa kutumia helikopta katika hospitali ya Grenoble, iliyoko maili 80 magaribi kutokea eneo latukio huku akiwa hana fahamu. 


Lakini katika ripoti iliyotolewa jana saa 1.20 jioni, daktari alisema hali yake inaendelea kuwa mbaya, wataalamu wa ubongo na uti wa mgongo waliingia jana jioni kwaajili ya kusaidiana kuokoa maisha ya mwanamichezo huyo maarufu.

Mjerumani huyo ambaye alistaafu mchezo huo mwaka 2012, ni dereva mzuri kuwahi kutokea. Mkurugenzi wa Meribel alidai kuwa Schumacher alipatwa na mshtuko na mtikisiko.
 TAZAMA PICHA ZA MICHAEL SCHUMACHER NA ENEO LA TUKIO...


MAGAZETI LEO TAREHE 30/12/2013





TAARIFA KWA UMMA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII


TAARIFA KWA UMMA
Itakumbukwa kuwa Serikali iliamua kuanzisha “Operesheni Tokomeza Ujangili” kufuatia kukithiri kwa vitendo vya ujangili katika maeneo yote yaliyotengwa kisheria kama Mapori ya Akiba; Hifadhi za Taifa na Hifadhi za Misitu katika miaka ya karibuni. Hata hivyo, Serikali iliamua kusitisha operesheni hiyo kwa muda.


PICHA: Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kushoto) akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) alipokuwa akizungumzia msimamo wa serikali juu ya matukio ya ujangili nchini. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Profesa Japhary Kideghesho.

SOMA ZAIDI...


Sunday, December 29, 2013

AJIPIGA RISASI NA MWINGINE KUCHINJWA

Singida

Watu wawili wamekufa katika matukio mawili tofauti yaliyotokkea juzi Mkoani Singida likiwemo la mfanyabiashara kujipiga risasi kichwani na mwingine huchinjwa shingoni na kutolewa koromeo na ulimi.

Hayo yalielezwa na Kamanda wa Polisi Mkoani humo Kamishina Msaidizi Mwandamizi Geofrey Kamwela alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari Ofisini kwake mjini Singida jana alasiri.

Katika tuio la kwanza ambalo limezua msisimko na gumzo kwenye nji wa Singida Kamanda huyo alisema Mfanyabiashara Mashaka Omari (30) alikutwa chumbani kwake juzi mtaa wa Ipembe akiwa amefariki Dunia baada ya kujipiga risasi kichwani na kufa papo hapo.


HATARI: MAJENGO HATARINI


Wakazi wa jijini wakipita pembeni mwa nyumba zilizoko pembezoni mwa barabara ya Yombo Buza karibu na kituo cha Shule, jijini Dar es Salaam Wilaya ya Temeke, kama zilivyokutwa na kamera yetu hivi karibuni, zikiwa hatarini kudondoka kutokana na mmomonyoko wa udongo uliosababishwa na mvua zilizonyesha hivi karibuni. Eneo hilo lilikumbwa na hali hiyo baada ya upanuzi wa barabara. Imedaiwa wakazi wa eneo hilo wamelipwa fidia lakini wamegoma kuhama ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo. (picha kwa hisani ya Mdau wa Matukio)

HII IMEKAAJE: JAJI RAMADHANI AWA MCHUNGAJI?

Jaji Ramadhani awa mchungaji Anglikana

Jaji Mkuu Mstaafu, Jaji Augustino Ramadhani akitoa mkate kwa waumini wa Kanisa la Anglikana baada ya kupewa Daraja la Ukasisi katika Kanisa la Anglikana lililopo Mkunazini mjini Zanziabar jana.

MAJANGA: WAGANGA WA KIENYEJI WAITABIRIA CCM

MWANZA

Makamu  wa Rais Mtendaji wa Chama cha Waganga wa Tiba asili na Tiba mbadala,Tanzania Traditonal Treatment Organazation (TATETO), Dkt Swalehe Issa Bukukwe,amekitabiria Chama cha Mapinduzi (CCM) akisema, kitaanguka kwenye uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 kinyume na alivyotabiri awali.

Kwamba utabiri wake wa Oktoba 2 mwaka 2011,ulionyesha CCM chama ambacho kinaongozwa na nyota ya darala la juu ya Simba, kingeshinda kwenye uchaguzi huo kutokana na nyota yake kung’ara,lakini utabiri huo umegeuka.

Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti hili juzi ofisini kwake Mabatini,Mwanza, Dkt Bukukwe alisema ,CCM mwaka 2015 itaanguka kwa sababu mbalimbali zikiwemo ukiukwaji wa maadili na viongozi waliopewa dhamana kushindwa kuwajibika kwa wananchi.


ANGALI HII NAYO: LINEX NAYE AFUNGUKA JUU YA JACK CLIFF




CHELSEA NA MBWEMBWE, WANADAI LEO NI SIKU YA BLUU

WANADAI NI BENDERA ZA BLUU TU NDIO ZIWE JUU




DUH : ORIGINAL KOMEDI NA SEMBE…ACHA TU



MAGAZETI YA LEO HAYA HAPA





LAZMA USOME HII:MWISHO HII NI NOMA SASA DUH...




INASIKITISHA: OBAMA NA MKEWE MICHELLE KUTENGANA

                         Barack Obama na mkewe Michelle kila mmoja akionekana kuwa kivyake.

RAIS wa Marekani, Barack Obama na mkewe Michelle wanadaiwa kutengana. Habari zinadai kuwa wawili hao wanalala katika vyumba tofauti kwa sasa ndani ya Ikulu ya Marekani 'White House'.

Mgogoro baina ya wawili hao ulianza zamani na wameweza kuendelea kuishi pamoja kwa sababu ya watoto wao wawili wa kike Sasha na Malia na kulinda heshima ya urais.

Michelle anadai amechoka na atakutana na mwanasheria wa masuala ya talaka ili aweze kuachana na rais huyo wa 44 nchini Marekani. Michelle ataendela kuishi Ikulu 'White House' kwa muda wote uliobaki katika kipindi cha utawala wa Obama, ila ameweka wazi kuwa watakuwa wakiishi vyumba tofauti.

Anataka kuishi katika chumba kimojawapo cha familia kilichowazi na anajiandaa kuhamisha nguo zake na kila kilicho chake kutoka kwenye jumba lao la kifahari la mamilioni ya dola lililopo Chicago.

Michelle alichanganyikiwa zaidi baada ya Obama kupiga picha za kimahaba (PICHANI KUSHOTO) akiwa na Waziri Mkuu wa Denmark, Helle Thorning-Schmidt, wakati wa mazishi ya marehemu Nelson Mandela nchini Afrika Kusini.

Obama mwenye miaka 52, alikuwa akifurahi, kunong'enezana na kumshika begani mrembo huyo mwenye umri wa miaka 46 ambaye amekuwa Waziri Mkuu wa Denmark tangu Oktoba 3, 2011


Saturday, December 28, 2013

UJUMBE WA JACKIE CLIFF KUHUSU MARTIN KADINDA

Baada ya kukamatwa na kilo 1.1 za heroin nchini China, mrembo Jackie Cliff kwa sasa anasubiria hatima yake kutokana na kosa hilo la kusafirisha madawa ya kulevya. Ikiwa nchini humo kuna adhabu tofauti za kuwahukumu watu wanao jihusisha na madawa ya kulevya.

Kupitia Personal Message ya BBM aliyoiandika mwana dada Jackie Cliff inayosema … ” Ikitokea nimekufa wosia Martin Kadinda ana maagizo ya nini cha kufanya … dnt ask pls.” inasemekana kuwa kama mrembo huyo atashindwa kujikwamua katika tatizo hilo basi, rafiki yake wa karibu ana maagizo yote ya nini cha kufanya kama yeye hatokuwepo tena. 

Taarifa hii ni kwa mujibu wa Gongamix



MAGAZETI YA LEO TANZANIA





POMBE YAMUUA MFANYAKAZI WA TIGO

Shinyanga 

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mfanyakazi mmoja wa kampuni ya simu za mkononi ya TIGO mkoani Shinyanga amekufa papo hapo baada ya kudaiwa kunywa pombe nyingi aina ya Konyangi kupita kiasi. 

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamemtaja mfanyakazi huyo kuwa ni Godi Mangala (34) aliyekuwa akiishi mtaa wa Majengo mapya kata ya Ngokolo manispaa ya Shinyanga ambalo limetokea juzi saa moja usiku wakati wa sikukuu ya krismasi. 



Thursday, December 26, 2013

VIDEO: JILINDE SIR TINO FT. MR BLUE



MEGATRADE YATOA MISAADA KWA WATOTO

Arusha

KAMPUNI ya Megatrade Ivestment kupitia kinywaji chake cha K-vant Gin imetoa misaada ya vitu mbalimbali ikiwemo chakula kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwaajili ya sikukuu ya krismasi na mwaka mpya katika kituo cha New Paradise kilichopo kata ya sokoni 1 jijini Arusha

Akikabidhi msaada huo juzi kituoni hapo Meneja mauzo na masoko Goodluck Kway wa kampuni ya hiyo kupitia kinywaji chake cha K-vant Gin alisema utowaji wa misaada kwa makundi maalum yenye uhitaji ni utaratibu wao wa kurudisha faida waliopata kwa mwaka mzima kwa jamii


HAYA NDIO MAGAZETI YA LEO TANZANIA





Wednesday, December 25, 2013

AIRTEL YATUMA SALAM ZA CHRISTMAS NA MWAKA MPYA

Kampuni ya mitandao ya simu za mkononi ya Airtel imewaasa Watanzania wote kote nchini kulinda amani na utulivu wa nchi katika kipindi hiki cha sikukuu ikiwa ni baada ya kuwatakia heri ya Christmas na mwaka mpya.

Akizungumza kwenye ofisi za makao makuu ya Airtel, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema sikukuu za Christmas na mwaka mpya ni sikukuu muhimu sana kwa wananchi wa taifa hili hivyo zinapaswa kusherehekewa kwa amani na utulivu.

“Ninawaomba wateja wa Airtel na watanzania wote kwa ujumla kutambua umuhimu wa sikukuu hizi na kuepuka kufanya matukio ambayo yanaweza kuhatarisha amani na utulivu wa taifa,” alisema Mmbando.



LEMBELI ATAKIWA KUMUOMBA RADHI MAIGE

Shinyanga 

Katika hali isiyokuwa ya kawaida wakazi wa jimbo la Msalala wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga wamemuomba mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya bunge ya ardhi, maliasili na mazingira, James Lembeli(Pichani kushoto) kumuomba radhi Mbunge wa jimbo lao Ezekiel Maige(Pichani Kulia) kutokana na kashifa aliyomzushia na kusababisha apoteze uwaziri wake. 

Madai ya wakazi wao yametolewa siku chache baada ya Lembeli ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kahama kupokelewa kama shujaa mara baada ya kurejea kutoka bungeni akipongezwa kwa kazi aliyoifanya na kusababisha kuwajibishwa kwa mawaziri wanne wanaotuhumiwa kushindwa kuwajibika katika operesheni tokomeza ujangili. 

Wakazi hao walisema wamelazimika kumtaka Lembeli amuombe radhi Maige ili amsafishe mbunge wao huyo kutokana na tuhuma kali alizomzushia wakati akiwa waziri wa maliasili na utalii akimtuhumu kwa madai yasiyokuwa na ukweli kwamba alihusika na utoroshaji wanyamahai kwenda nje ya nchi kinyume cha sheria. 

Walisema madai yao hayo yanatokana na ukweli alioukiri Lembeli bungeni wiki iliyopita wakati akiwasilisha taarifa ya kamati yake iliyochunguza vitendo viovu vilivyotendwa na askari mbalimbali waliokuwa wakitekeleza operesheni tokomeza ambapo alikiri kutohusika moja kwa moja kwa waziri mwenye dhamana, Khamis Kagasheki.

Akifafanua mmoja wa wakazi hao waliozungumza na Majira jana aliyejitambulisha kwa jina la Masanja Joseph alisema katika taarifa yake bungeni wiki iliyopita Lembeli alimsafisha aliyekuwa waziri wa wizara hiyo (Kagasheki) akidai hakuhusika katika kashfa ya wananchi kutendewa vitendo viovu katika operesheni hiyo bali watendaji wake.



ANASWA KWA TUHUMA ZA KUUZA SILAHA

Tabora

JESHI La Polisi Mkoani Tabora limemkamata mkazi mmoja wa Mjini Kigoma kwa
kuwa na Bunduki ya Kivita pamoja na magazine yake.

Kamanda wa Polisi Mkoani Tabora, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Peter Ouma,
amemtaja kuwa ni Salumu Musa maarufu kwa jina la Malembeka aliyekamatwa
katika stendi kuu ya Mabasi mjini Tabora akitokea Kigoma kwenda wilayani
Sikonge.


VIDEO: I WISH - DAVID FT. JACOB



MAGAZETI SIKU YA CHRISTMAS HAYA HAPA






Tuesday, December 24, 2013

DR. SLAA AHITIMISHA ZIARA YAKE YA SIKU 22 NCHINI

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibroad Slaa amehitimisha ziara yake ya siku 22 ya kuimarisha na kukagua uhai wa chama katika majimbo 19 mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Singida, akiitaka Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha manyanyaso na ukatili wanaofanyiwa wananchi.

Amesema kuwa baada ya kuzungumza na wananchi hususan maeneo ya vijijini ambako alijikita kwa siku hizo 22, ameendelea kuthibitisha kuwa sehemu kubwa ya kero zinazowakabili Watanzania, hazihitaji gharama yoyote kuzimaliza ili wananchi waishi kwa amani katika nchi yao, akitolea mfano wa kero ya manyanyaso mbalimbali, hususan kutoka kwa vyombo vya dola.


MADEE, CHEGE KUWASHA MOTO COCO BEACH XMASS DAY

 Katika kuhakikisha sikukuu za krismas inaenda vyema, kampuni ya mawasiliano ya Vodacom imeandaa Tamasha kwa wateja na mashabiki wa Muiki katika viwanja vya fukwe za Coco wakati huu ikiwaleta wasanii ambao wako juu kimuziki Madee(Kulia chini) na Chege(kushoto chini).

Wasanii hao watatoa burudani bure kwa wakazi wa Dar wote watakao jitokeza katika viwanja hivyo huku pamoja na mambo mengine watashuhudia simu za kisasa za Huawei zikiuzwa katika wakati huo wa Burudani.

Tamasha hilo litafanyika kwa siku tatu yaani krismas yenyewe yaani tarehe 25 na, 26 maarufu kama Boxing Day pamoja na mwaka mpya ambao litawawezesha wateja kujinunulia simu za kisasa kwa bei nafuu ambazo zitakuwa zimeunganishwa moja kwa moja na vifurushi vyenye nguvu vya intaneti vya mtandao huo.

Akizungumza na chombo hichi cha Habari Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twisa amesema wameona si kitu kizuri kumaliza mwaka hususani katika kipindi hiki muhimu cha sikukuu na kuukaribisha mwaka mpya bila ya kuwapatia kitu chochote cha kusindikiza shamrashamra hizi za sikukuu wateja wao.


WAZIRI MKUU APOKEA MSAADA WA PIKIPIKI 44

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amepokea pikipiki 44 zikiwa ni msaada kutoka Ubalozi wa China na Kampuni ya Fu-Tang ya kutoka China.

Amekabidhiwa msaada huo leo mchana (Jumanne, Desemba 24, 2013) mbele ya viongozi wa wilaya ya Mlele katika hafla fupi iliyofanyika kijiji cha Kibaoni, wilayani Mlele, mkoani Katavi na kushuhudiwa na wakazi wa kijiji hicho.

Akizungumza na viongozi wa wilaya hiyo pamoja na wakazi wa kijiji hicho kabla ya kukabidhi msaada huo, Balozi wa China hapa nchini, Dk. Lu Youqing alisema anaamini kupatikana kwa pikipiki hizo kutasaidia kuleta maendeleo ya haraka ya wilaya hiyo.

“Tunataraji matumizi ya pikipiki hizi yatasaidia kuleta maendeleo ya haraka na hatimaye kuongeza kipato cha wakazi wa wilaya hii,” alisema Balozi Lu ambaye ofisi yake imekabidhi pikipiki 20.


TAHADHARI: KIMBUNGA KINATARAJIWA MAENEO YA PWANI




BREAKING NEWS: WAFANYAKAZI WA MAJANI YA CHAI WAGOMA






MUGABE AZIDI KUMSUTA TSZANGIRAI AMWAMBIA "KAFIE MBELE"

Rais Robert Mugabe kavunjilia mbali matumaini ya ushirikiano na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai, kwa kusema wapinzani wa MDC-T na kiongozi wao “Wakafie Mbele”

Akiongea jumapili iliyopita akiwa Bulawayo alipokuw akizindua sanamu ya marehemu makamu wa rais Joshua Nkomo aliyefariki mwaka 1999, Mugabe aliwataka mashujaa wa vita kurudi ZANU PF.

“Simuongelei (Morgan) Tsvangirai na MDC; hao wakafie mbele. Nawaambia (mashujaa wetu) wanaopambana na maadui, hamuoni uchungu unaowapata watu” Mugabe alisema

“Vifo na majeraha yaliyowapata wakati wa mapambano na mnadiriki kushirikiana na adui wa watu wenu wenyewe? Naongelea kuhusu msimamo wa upinzani leo kugeuka na kukimbilia Waingereza na Wamarekani ili tu watupinge”

MAGAZETINI LEO TAREHE 24/12/2013