Wednesday, December 18, 2013

ABIRIA WA ETHIOPIA AIRLINE WANUSURIKA ARUSHA

Ndege hiyo ilikuwa itue kwenye Uwanja wa Kimataifa Kilimanjaro, lakini ilitua kwenye uwanja wa Arusha ambao njia ya kutua ndege kwenye uwanja huo inasemekana ni urefu wa mita 1.620 tu, au futi 5.315. Uwanja huo hauna uwezo kumudu ndege kubwa kama hiyo aina ya Boeing 767.
Kumekuwepo na maswali mengi kuhusiana na ndege hiyo kutua katika uwanja huo kwani ni hatari kwa ndege kubwa kama hiyo kutua kwenye uwanja mdogo kama huo.
Uwanja huo, ambao kuinuliwa kwake kumo kwenye hati maalum zinazoonesha ni futi 4.550 juu ya usawa wa bahari au mita 1.387.
Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari, ndege hiyo iliyokuwa imesajiliwa kama ET-AQW ilikuwa kwenye safari namba ET815 kutoka Addis kupitia Kilimanjaro kwenda Zanzibar na kurudi Addis Ababa, Ethiopia.
Taarifa za awali, zilieleza kuwa hakuna abiria wala mfanyakazi yeyote aliyejeruhiwa na kwamba ndege hiyo ilisimama kabla ya kufika mwisho wa njia ya kutua.
Uwanja huo pia unaripotiwa kufungwa kutoruhusu ndege kuingia wala kutoka kutokana kupangwa upya kwa safari za ndege za Precision Air na ndege nyingine zinazotoka na kwenda mbuga za wanyama.
Vyanzo vya habari kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro viliongeza kusema kwamba ndege hiyo ilikuwa itue kwenye uwanja huo, lakini haikuwezekana kwa sababu kulikuwepo na ndege nyingine yenye hitilafu kwenye njia ya kutua ndege.
Uchunguzi bado unafanyika ili kujua ni kwa nini ndege hiyo ilikwenda kutua uwanja wa Arusha badala ya kwenda kutua Nairobi au Dar es Salaam kama inavyotakiwa kimataifa, hasa kutokana na uvumi kwamba ilikuwa imeishiwa mafuta.
Ndege hiyo kwenda kutua Arusha imekuwa mjadala mkali miongoni mwa wadau wa safari za ndege nchini, kwani abiria, wafanyakazi na ndege yenyewe walikuwa hatarini.
Bado haifahamiki kama ndege hiyo, B767, hata kama itaondolewa vifaa na siti, itaweza kuruka salama kutoka uwanja wa Arusha kwenda Kilimanjaro, wakati uwanja huo utakapokuwa umefunguliwa na shughuli kuanza tena.







No comments:

Post a Comment