Tuesday, June 04, 2013

MATUKIO MBALIMBALI NCHINI






Mkazi wa Dar es Salaam, Kawe eneo la bondeni karibu na daraja akifanya biashara ya kuuza chenji ambapo chenji ya  shilingi elfu moja unalipa shilingi 100. Mkazi huyo sio tu anajukumu la biashara yake lakini pia ni mama mwenye mtoto ndogo. Wakati picha hii inapigwa binti huyu alikuwa anamsumbua mama yake. 





Taswira ya jiji la Dar es Salaam, hapa ni eneo la Tegeta kama linavyoonekana. Hili nie eneo lenye shughuli nyingi kwa maisha ya kila siku ya wakazi wa eneo hilo pamoja na maeneo ya Kunduchi, Wazo na hata Boko. Hapa unaweza kuchanganyikiwa upite wapi kama eneo hilo linavyoonekana katika picha.


CHINI :Mpanda baskeli akiwa amebeba magunia ya mkaa akielekea sokoni hivi karibuni, katika barabara mpya inayojengwa kutoka Msata mpaka Bagamoyo. Sehemu kubwa ya barabara hiyo imeshakamilika na kubakiza kipande kidogo chenye madaraja makubwa kadhaa likiwepo la mto Ruvu. Njia hii ndi itakayotumika kwaajili ya mabasi yanayokwenda njia ya Tanga ikiwa ni pamoja na Moshi Arusha.




No comments:

Post a Comment