TAARIFA KUHUSU HESHIMA ZA
MWISHO NA MAZISHI
YA ALIYEKUWA MHARIRI WA JAMBO
LEO
MAREHEMU WILLY EDWARD OGUNDE
1.
Jukwaa
la Wahariri Tanzania (TEF) linapenda kuuarifu umma kwamba, shughuli za kuuaga
(kutoa heshima za mwisho) kwa aliyekuwa Mhariri Mkuu wa gazeti la Jambo Leo na
mwanachama wa TEF, Willy Edward Ogunde zitafanyika kesho, Jumatano Juni 20,
2012, katika viwanja vya Mnazimmoja (Arnatouglou) jijini Dar es Salaam.
2.
Shughuli
hii ya mwanzo wa kuhitimisha safari ya mwisho ya mwenzetu, itafanyika kuanzia
saa 4.00 asubuhi ikiongozwa na wanafamilia kwa kushirikiana na Kampuni ya Jambo
Concept alikokuwa akifanya kazi Willy na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).
3.
Baada ya
shughuli za kutoa heshima za mwisho kukamilika, safari ya kuusafirisha mwili wa
marehemu Willy kwenda Mugumu, Serengeti itaanza majira ya mchana kwa ajili ya
mazishi yanayotarajiwa kufanyika Jumamosi, Juni 23, 2012 hukohuko Serengeti.
4.
Jukwaa
la Wahariri katika mazishi hayo litawakilishwa na ujumbe wa watu wanne
wakiongozwa na Mwenyekiti wa TEF, Absalom Kibanda, Mhariri Msanifu wa New
Habari Ltd, Revocatus Makaranga na Mhariri Msanifu wa Magazeti ya Uhuru na
Mzalengo, Jane Mihanji. Kadhalika Mkuu wa Wilaya ya Magu mkoani Mwanza,
Jacqueline Liana ambaye alikuwa mwanachama wa TEF pia anatarajiwa kuungana na
ujumbe huyo kwenye mazishi.
5.
TEF
tukiwa tumeguswa sana na msiba huu, tunachukua fursa hii kuwashukuru wadau wetu
wote ambao kwa namna moja au nyingine walitufariji, kutuma salaam za rambirambi
nakutoa michango yao ya hali na mali tangu mauti yalipomkuta mwenzetu mkoani
Morogoro usiku wa kuamkia Jumapili Juni 16, 2012 alikokuwa amekwenda kushiriki
semina ya masuala ya Sensa ya Watu na Makazi ya 2012.
6.
Kwa
uchache tunaomba shukrani zetu ziwafikie Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel
Bendera, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, waandishi wa habari wa mkoa wa
Morogoro na Ofisi ya Taifa ya Sensa (NBS) ambao kwa namna moja au nyingine
waliwezesha kusafirishwa kwa mwili wa marehemu kutoka Morgororo hadi hosipitali
ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.
7.
Pia
tunawashukuru Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Shirika la Nyumba la Taifa
(NHC),
8.
Kwa mara
nyingine tunawapa pole wale wote walioguswa kwa namna moja au nyingine na msiba
huu wa ghafla, wakiwamo familia ya marehemu, hususan mke wake na watoto, wafanyakazi
wa gazeti la Jambo Leo na wanahabari wote katika tasnia nzima ya habari nchini.
9.
Sisi
katika Jukwaa la Wahariri tumeguswa kwa namna ya pekee na msiba huu mkubwa.
Willy Edward Ogunde ametuacha na ametuachia majonzi makubwa, pia pengo kubwa
katika fani ya habari. Kama tulivyosema katika taarifa yetuya awali, tunamshukuru
Mungu aliyetupa nafasi ya kushirikiana naye katika maisha ya kitaaluma na zaidi
tukiwa wahariri.
10.
Kwa wale
wanaosafiri kwenda Serengeti, tunawatakia Baraka za Mungu katika safari hiyo na
Mungu awatangulie ili wakatuwakilishe vyema katika mazishi ya mwenzetu Willy
Edward Ogunde. Bwana alitoa na Bwana ametwa jina lake lihimidiwe.
KATIBU WA JUKWAA LA WAHARIRI (TEF)
No comments:
Post a Comment