Taarifa
kwa vyombo vya Habari
Vodacom
yazindua vifurushi vipya vya intanet kwa bei nafuu.
Vodacom
TZ yazindua vifurushi vya internet
ambavyo ni rahisi na vyepesi kwa wateja wao kuelewa ili kiumarisha
matumizi ya huduma za intanet nchini.
Mteja
anatakiwa kupiga *149*01# na kuchagua aina ya huduma ya intanet
anayohitaji.
Huduma
ya Facebook na Twitter kuendelea kuwa bure.
Dar
es Salaam, 18 juni 2012,
Kampuni
ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua vifurushi vipya vya intanet
ambavyo vitawawezesha wateja wake kupata huduma ya internet kwa shilingi 250 tu
kwa siku.
Huduma
hiyo ya Wajanja intanet imeboreshwa zaidi ili kuwawezesha wateja kuelewa huduma
za intanet na kuchagua kikamilifu huduma zitakazowafaa hivyo kuweza kuperuzi na
kupata taarifa kwa kasi na kwa bei nafuu kupitia mtandao wa Vodacom.
Hata
hivyo, Vodacom ilisisitiza kuwa huduma ya kuperuzi facebook na twitter
zitaendelea kuwa bure kwa wateja wote.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Vodacom Tanzania Bw. Rene Meza alisema kuwa Kampuni hiyo imerahisisha huduma hiyo kwa
wateja wake ili kuwawezesha kuelewa kiasi ambacho wanatumia katika huduma za
intanet, suala ambalo limekuwa kikwazo kikubwa kwa watumiaji wa intanet kote
nchini.
Alibainisha
kuwa Kampuni hiyo imeona umuhimu wa watoa huduma za mawasiliano kama Vodacom
kuondoa utata ambao unawazuia wateja kutumia mfumo mpya wa teknolojia ya intanet katika
mawasiliano. "Tumeiweka huduma yetu
katika njia ambayo ni rahisi kwa wateja wetu kuelewa kwani tunaamini kuwa hii
ni njia rahisi ya kuongeza matumizi ya intanet katika kueboresha maendeleo ya
kijamii na kiuchumi.
Wateja
wote wa malipo ya baada au ya kabla watapata huduma ya internet kwa kasi
kupitia simu zao za mkononi na modem.
Aliendelea kusema kuwa kutokana na huduma hiyo mpya, sasa Wateja wa
Vodacom watapata huduma isiyo na kikomo na yenye kasi kwa siku saba mfululizo
kwa Sh. 10,000 au Sh. 30,000 kwa siku thelathini.
Kuweza
kununua vifurushi vya internet mteja anatakiwa kupiga *149*01# na kupata orodha
ya huduma za intanet kwa kutuma ujumbe mfupi wa maandishi SMS wenye neno VODACOM INTERNET kwenda 15300 bure.
Vodacom
Tanzania inaongoza kwa mtandao wa 3G
iliosambaa zaidi nchini baada ya kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni 2 katika
kupanua miundombinu yake ya intanet, na tayari uwekezaji huo umewawezesha
Watanzania kunufaika na njia mpya za mawasiliano katika kujiletea maendeleo ya
kijamii na kiuchumi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment