Mwanamuziki maarufu duniani wa miondoko ya Hip Hop nchini Marekani, Snoop Dogg (Pichani kulia) na
kampuni yake ya Casa Verde Capital wanapanga kuwekeza katika sekta ya bangi
nchini Marekani. Wakati Snoop hatowekeza moja kwa moja katika kliniki na biashara yoyote inayolenga kutengeneza au
kulima bangi, ameshawekeza katika zaidi ya makampuni 8 yanayosaidia kuendesha
biashara ya kuzalisha bangi.
Dola milioni 45 za Marekani (sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 101.5 ), ni moja ya uwekezaji mkubwa
kuwahi kufanywa na kampuni ya Casa Verde Capital kwa mwaka jana pekee. Snoop
ameripotiwa kutokuwa tayari kuwekeza chini ya dola za Marekani milioni 1 (sawa na shilingi Bilioni 2.25 za Tanzania) kwa
kila kampuni kwa madai kuwa sekta hiyo ni kati ya sekta muhimu kwa kizazi
kijacho.
Karan Wadhera, Mkurugenzi Mtendaji wa Casa Verde Capital, ameeleza
lengo lao la baadae, “ Tunalenga makampuni yanayojenga uwezo wa muda mrefu
sababu malengo ya muda mfupi hayawezi kutusaidia katika mazingira ya kisheria”
Snoop Dogg amekuwa mmoja wa watu wachache walioihalalisha
wazi bangi na kufahamika kama ‘mkongwe’ wa bangi. Uwekezaji huo ni mkubwa haswa
kutegenewa kutoka kwa mtu ambaye analipenda zao la bangi kutokea moyoni.
No comments:
Post a Comment