Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akizungumza na
wafanyakazi wa Gereji ya Spring City Enterprises inayomilikiwa na raia
wa China iliyopo Mikocheni B Mlalakuwa Barabara ya Mwai Kibaki
Dar es Salaam leo, alipofika kusikiliza malalamiko yao mbalimbali
yakiwemo ya kutokuwa na mikataba ya kazi licha ya kuwa kazini kwa zaidi
ya miaka saba,hicho ni kitambulisho dhaifu wanavyotumia wafanyakazi hao
ambacho hakiwezi kutumimika kumuwekea mtu dhamana na shughuli
mbalimbali.
DC Makonda (kulia), akiangalia bomba la maji wanayotumia wafanyakazi hao
kwa kunywa. Hata hivyo wafanyakazi hao walilalamikia maji hayo kuwa si
salama kwa kuwa yanatoka eneo la chooni.
Kiongozi wa gereji hiyo, Mr Yu Viangqian (kushoto), akizungumza na
wanahabari kuhusu madai ya kuwanyanyasa wafanyakazi wa kitanzania na
kutokuwa na mikataba
Ofisa Uhamiaji wa Wilaya ya Kinondoni, Evarist Mlay akizungumza na
waandishi wa habari eneo la tukio baada ya kuwepo madai ya baadhi ya
wachina kuishi nchini kinyemela.
Sehemu ya gareji inayolalamikiwa
No comments:
Post a Comment