Wednesday, May 28, 2014

VIFAA VYA KISASA VYA MICHEZO VYAINGIA NCHINI

Kampuni kongwe na maarufu nchini kwa kusambaza vifaa mbalimbali vya michezo na yenye uzoefu wa siku nyingi, imeingiza vifaa vipya na vya kisasa kabisa vya michezo kwaajili ya wana michezo wote nchini.

Kampuni hiyo inayojushughulisha na usambazaji wa huduma hiyo imesema lengo lake ni kuinua ubunifu na hari ya michezo nchini ili kuinua viwango vya michezo.

Kampuni ya Isere Sports imewataka wanamichezo ikiwa ni pamoja na wapenzi wa michezo nchini kuchangamkia vigfaa hivyo kwani ni vya kisasa na vimetengenezwa kwa viwango vya kimataifa vyenye kuzingatia mahitaji ya msingi ya mtumiaji.

Akizungumza na ImmaMatukio Blog, Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Bw. Abasi Isere (kushoto), amesema anawakaribisha wa michezo haswa wana UMISETA na UMISHIMUTA na kwamba Isere kuna kila wanachohitaji kukidhi mahitaji yao.

“Sisi tunazingatia mahitaji ya wanamichezo, ikiwa ni pamoja na viwango vya hali ya juu ili kuwawezesha watumiaji kutumia na kufikia malengo yao kirahisi” alisema Bw. Abasi.



Kati ya vifaa hivyo ni pamoja na jezi za soka, netball, riadha na michezo mingine kama tenis, volleyball, n.k lakini pia kuna mipira, filimbi, viatu , sox, na mengineyo mengi


No comments:

Post a Comment