Tuesday, October 15, 2013

RIHANNA AONESHA JEURI YA PESA

MSANII wa muziki kutoka nchini Marekani Rihanna amethibitisha kuwa ni miongoni mwa wasanii wadogo waliopata mafanikio baada ya kumnunulia mama yake nyumba ya kifahari kwa dola za marekani milioni 22 ambayo ni sawa na bilioni 35 za kitanzania.

Rihanna amemnunulia mama yake jumba hilo la kifahari mjini Barbados ambapo msanii huyo ndipo alipozaliwa na kukulia ingawa hurudi nyumbani hapo kila mwisho wa mwaka kwa ajili ya kusherehekea sikukuu za Christimas na familia yake.


Mbali na hilo Rihanna ameandika historia nyingine baada ya kujazaa mashabiki wengi katika shoo yake aliyoifanya katika uwanja wa mpira wa miguu nchini Afrika Kusini.

Msanii huyo ambaye yupo nchini humo kwa ajili ya ziara ya shoo yake 'Diamonds World Tour' ambapo ameweza kuvunja rekodi kwa kuweza kuujaza uwanja huo wa mpira ambao hujaa katika mechi kubwa za mpira hasa za kimataifa.

Kwa mujibu wa mtandao wa Entertainment Wise ulidai kuwa tiketi zote za show hiyo zilimalizika na zaidi ya watu elfu 67 walihudhuria show hiyo uwanjani hapo, hali iliyopelekea msanii huyo mwenye umri wa miaka 25 kuwa wa kwanza kuujaza uwanja huo na tiketi zote kuisha.





No comments:

Post a Comment