Showing posts with label SPOTS. Show all posts
Showing posts with label SPOTS. Show all posts

Sunday, March 20, 2016

WAFANYAKAZI WA MFUKO WA PENSHENI WA PPF WASHIRIKI BONANZA MAALUM JIJILI DAR

Meneja wa Fedha wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Musoffe Laurance,akimkabidhi Cheti mshindi wa kwanza waMbio za Magunia kwa wanawake, Magreth John, aliyeibuka kidedea katika mbio hizo wakati wa Bonanza maalum la Wafanyakazi wa PPF lililofanyika kwenye Uwanja wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama jijini Dar es Salaam, leo Machi 19,2016.

Mfanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, akishiriki mchezo wakukimbiza kuku, wakati wa Bonanza maalum la Wafanyakazi wa Mfuko huo lililofanyika kwenye Uwanja wa Chuo cha Ustawi wa Jamii,jijini Dar es Salaam,leo Machi 19,2016.


Tuesday, January 14, 2014

BREAKING NEWS: NI RONALDO NDIO MSHINDI, SIO MESS WALA RIBERY

Mshambuliaji wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Christiano Ronaldo jana usiku alinyakua tuzo ya mchezajii bora wa soka wa fifa wa mwaka 2013 na kuwashinda Lionel Mess wa Barcelona na Frank Ribery wa Bayern Munich.

Ronaldo ambaye alinyakuwa tuzo hiyo ya mchezaji bora wa dunia kwa mara kwanza mwaka 2008 alitangazwa kunyakua tuzo mwaka 2013 baada ya kupigiwa kura na makocha, manahodha na waandishi wa habari.

Kwa mujibu wa matokeo Ronaldo alipata kura 1365 akimshinda Messi aliyepata kura 1,205 na Ribery akiambulia kura 1,127.


Tuesday, October 15, 2013

BRAZIL KUKIPIGA NA ZAMBIA MUDA SI MREFU

Timu ya taifa ya Zambia, Chipolopolo ndani ya saa moja kutokea sasa wataingia uwanjani kucheza mechi ya kirafiki na timu ya taifa ya Brazil. Mechi hiyo ambayo ni muhimu kwa Zambia ikiwa ni mechi yao ya kwanza kucheza na Brazil ambao ni mabingwa mara tano wa kombe la dunia.

“Tunawaheshimu lakini hatuwaogopi” alisema mmoja wa wachezaji wa timu ya Chipolopolo ambao wako jijini Beijing kwaajili ya mechi hiyo, itakayochezwa saa saba kamili saa za Zambia ambayo ni sawa na saa moja usiku Beijing China, katika uwanja maarufu uliojengwa kama kiota cha ndege.

Huku Chipolopolo ikiwa imetolewa katima michuano ya maandalizi ya kombe la dunia mwaka 2014, Brazil itaingia uwanjani, ikiwa ni mechi muhimu pia kwa katika maandalizi ya michuano ya dunia.


Wednesday, August 28, 2013

ARSENAL YAFANYA KWELI


Aaron Ramsey alifunga mabao mawili na kuipa klabu yake Arsenal ushindi wa wazi bila upinzani mkali dhidi ya Fenerbahce ya Uturuki.

Katika mechi iliyochezwa hapo jana kwenye uwanja wa Emirates, Arsenal imefuzu kwa Ligi ya Mabingwa kwa mwaka wa kumi na sita mfululizo.

Wageni Fenerbahce walibaki nyuma tangu mechi ya awamu ya kwanza walipofungwa mabao matatu kwa bila na Arsenal. 



Friday, July 12, 2013

VILABU VINNE VYAPIGWA MARUFUKU NIGERIA



Vilabu vinne ambavyo vilihusika na njama ya kupanga matokeo ya mechi vimepigwa marufuku nchini Nigeria.Katika mechi moja klabu moja iliilaza nyingine magoli 79-0 na magoli 67-0 katika mechi ya pili.

Jumla ya magoli 146 zilifungwa katika mechi hizo mbili, idadi ambayo inaingia katika vutabu vya kumbukumbu kama mechi iliyokuwa na idadi kubwa zaidi ya magoli duniani.

Klabu ya Plateau United Feeders iliilaza timu ya Akurba ili hali timu ya Polisi ya Machine FC kwa upande wake ikailaza Bubayaro magoli 67-0.

Thursday, May 16, 2013

BARTHEZ, CHANONGO WAITWA STARS


KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen jana ametaja kikosi cha wachezaji 26 watakaoingia kambini kujiwinda kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.

Katika kikosi hicho, Kim ameita wachezaji wapya sita ingawa baadhi yao wamewahi kuchezea timu hiyo, huku akiacha wengine watatu aliokuwa nao kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Morocco ambapo Taifa Stars ilishinda mabao 3-1.


TANZANIA YAJITOA COSAFA



TANZANIA (Taifa Stars) imejitoa kwenye michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA), itakayofanyika nchini Zambia kuanzia Julai 2-26 mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah alisema Stars ambayo iliingizwa katika michuano hiyo kama timu mwalikwa imejitoa kutokana na mwingiliano wa ratiba kati ya michuano hiyo na mechi za Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).