Thursday, March 08, 2018

MWENYEKITI WA UWT ATEMBELEA HOSPITALI KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, LEO


Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akifurahia mtoto wa kike, alipotembelea wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Mbaala Rangi tatu, wilayani Temeke Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani, leo Machi 8, 2018. Mapema Mama Kabaka akiambatana na kina mama mbalimbali wakiwemo viongozi wa UWT kutoka maeneo mbalimbali, alishiriki kufanya usafi na baadaye kutoa zawadi mbalimbali kwa uongozi na waonjwa kwenye Hospitali hiyo. Kulia ni Mariam Salum, mzazi wa mtoto huyo.


"Haya Mama chukua kichana chetu.." akasema Mama Kabaka wakati akirejesha mtoto kwa Mariamu Salum baada ya kumkabidhi zawadi ya kanga.


Mama Gaudentia Kabaka akitoa zawadi za juisi kwa kina mama waliojifungua katika hospitali hiyo ya Mbagala Ranitatu


Baadhi ya Kinamama wakaiwa na zawadi za kanga na sabuni ambazo Mama Kabaka aliawa kwa kina amama waliojifunua katika hospitali hiyo.


"Hebu chukua kanga hii kutoka kwa kina mama wenzako.." akasema Mama Kabaka wakati akimkabidhi Mwajuma Ally aliyejfungua mtoto katika hospitali ya Mbagala Rangitatu


"Loooh mtoto umejifunugua mtoto mzuri sana..." akasema Mama Kabaka


Kisha akampatia zawadi ya mche wa sabuni


Diwani wa Viti Maalum CCM, Mariam Mtemvu na wenzake wakimsalimia mmoja wa Kina mama aliyekuwa katika Wodi ya Wazazi baada ya kujifungua katika hospitali ya Mbagala Ranitatu, leo


Ofisa wa Makao Makuu ya UWT Ndugu Kisa wapili kulia, akiwa na kina mama weningine.


Ofisa wa Makao Makuu ya UWT Ndugu Kisa (kushoto), akiwa na wauguzi na kina mama weningine kwenye hospitali hiyo ya Mbagala Ranitatu leo.


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akimpa zawadi ya kanga mmoja wa wauuzi katika hospitali ya Mbagala Rangitatu wakati wa ziara hiyo


"Wauuzi na Madaktari honereni kwa kazi nzuri na hasa kwa kujali afya za kina mama na watoto...endeleni kuchapa kazi tupo pamoja nanyi", alisema Mama Kabaka wakati akizunumza na baadhi ya wauguzi na madaktari wa hospitali ya Mbagala Ranitatu wakati wa ziara hiyo. Kushoto ni Matroni wa wodi ya Wazazi Maria Lumambo


Mama Kabaka akiendelea kuzunumza nao


Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akifuatana na Matroni wa Wodi ya Wazazi Maria Lumambo, baada ya kutoka wodini kuwaona na kuwapa zawadi wazazi


Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akizungumza baada ya kutoka wodini kuwaona na kuwapa zawadi wazazi


Picha ya kumbukumbu


Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akiwa tayari kuondoka kwenye Hospitali ya Mbagala Rani tatu baada ya ziara yake leo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment