Mkuu wa wilaya ya Hai ,Gelasius Byakanwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai kuhusu ubadhilifu uliofanyika wakati wa zoezi la utengenezaji wa madawati.Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Yahana Sintoo.
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai wakiwa katika kikao hicho.
Na Dixon Busagaga,Hai.
MKUU wa wilaya ya Hai, Gelasius
Byakanwa ametoa jukumu kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya
hiyo,Yohana Sintoo la kuamua hatma ya watumishi wake watano wanaotajwa
katika tuhuma za ubadhilifu wa fedha wakati wa zoezi la utengenezaji wa
madawati.
Akiwa ndio mamlaka ya nidhamu kwa watumishi wa
halmashauri hiyo,Mkurugenzi Sintoo ndiye mwenye maamuzi ya kuwasimamisha
kazi watumishi hao baada ya tume iliyoundwa na mkuu wa wilaya hiyo,
Byakanwa kumaliza kazi yake ya uchunguzi dhidi ya watumishi hao na
kubaini mapungufu kadhaa.
Akihitimisha taarifa yake wakati wa
kikao na watumishi wa halmashauri hiyo,Byakanwa aliagiza taasisi ya
kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kuchunguza na kuchukua hatua
dhidi ya watumishi hao akiwemo aliyekuwa kaimu Mkurugenzi ,Mhandisi
Kweka.
“Mamlaka ya nidhamu ya watumishi wa Halmashauri ni
mkurugenzi pamoja na baraza la madiwani ,lakini mwajiri ni ofisi ya
katibu tawala mkoa ,Ofisi hizi mbili ndizo zinazoweza kukaa na kuchukua
hatua za kuzuia matukio au vitendo kama hivyo.”alisema Byakanwa.
“Niishauri ofisi ya Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro pamoja na ofisi
ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ambayo ndio mamlaka ya
nidhamu kwa watumishi hao kupima kuhusu hatua za kuchukua dhidi ya
watumishi hawa”aliongeza Byakanwa.
Mkuu huyo wa wilaya
alisema tuhuma zinazowakabili watumishi hao ,majina yao tumeyahifadhi
kwa sasa ni pamoja na kupitisha barua ya malipo bila kujiridhisha kama
kuna mkataba wa kutengeneza madawati na kufanya malipo ya fremu za
madawati badala ya madawati.
Tuhuma nyingine inaihusu timu ya
ukaguzi iliyokiri kukamilika kwa kazi bila ya kuonesha kama walipokea
madawati au walienda kukagua kazi ya mzabuni licha ya mzabuni kuomba
malipo ya fremu za madawati badala ya Madawati kamili.
Ofisi ya
elimu msingi,ofisi ya mkurugenzi,ofisi ya Mhasibu wa Halamshauri na
kitengo cha manunuzi pia zinatuhumiwa kushindwa kubaini nyaraka
zilizowasilishwa na mzabuni endapo zilikuwa ni kwa ajili ya fremu za
Madawati badala ya Madawati kamili.
Katika kikao hicho
kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo Byakanwa alisema
kampuni iliyopewa zabuni ya kutengeneza madawati ni ya Ujenzi na
haijawahi kufanya kazi ya kutengeneza madawati, kuwa na karakana wala
vifaa vya uselemala .
Byakanwa alisema kwa malipo yaliyofanyika
Halmashauri ilipoteza zaidi ya sh Mil 12 huku akishangazwa na hatua ya
mmoja wa watumishi wanaotuhumiwa kuomba malipo badala ya mzabuni.
Akionyesha
namna watumishi hao walivyokiuka taratibu Byakanwa alisema taarifa ya
uchunguzi inaonyesha Halmashauri iliunda timu ya ukaguzi ambayo katika
cheti cha ukaguzi na mapokezi ya bidhaa kinaonyesha bidhaa au madawati
yalipelekwa ,Julai 16, 2016 ,siku 12 tangu siku ya mkataba na mzabuni.
“Mmoja
w wajumbe wa kamati hiyo ya ukaguzi alikuwa ni mjumbe wa kamati ya
kuratibu zoezi la Madawati ,alikuwa na jukumu la kusambaza mbao kwa
wazabuni na alikuwa anajua kuwa hajapeleka mbao za kutosha kwa mzabuni
,katika maelezo yake mbele ya tume anakiri kuwa mzabuni hajamaliza kazi
kwa sababu Halmashauri haijampa mbao.”alisema Byakanwa.
Alisema
mzabuni aliieleza tume kuwa anadaiwa madawati 246 na halmashauri na kuwa
amekamilisha kutegeneza madawati 154 na ueleza kua alishindwa
kukamilisha kutokana na kukosa mbao kutoka halmashauri.
“June
9,2016 malipo ya Sh Mil 19.2 yakalipwa kwa ajili ya fremu za madawati
siyo Madawati.Vocha ya malipo ikasainiwa na DT na kuandaliwa na mtumishi
mwingine (jina tunalo) ikakamilisha mchezo.”alisema Byakanwa.
Mkuu
huyo wa wilaya alisema kufanya hivyo ilikuwa ni kinyume cha taratibu za
malipo kwa kuwa wahusika walipaswa kujiridhisha na nyaraka walizokuwa
wakitumia ,kwa nini mzabuni aliamua kudanganya Halmashauri.
Byakanwa
aliishauri ofisi ya Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro pamoja na ofisi
ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai ambayo ndio mamlaka ya
nidhamu kwa watumishi hao kupima kuhusu hatua za kuchukua dhidi ya
watumishi hao.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya
wilaya ya Hai,Yahana Sintoo alisema licha ya kwamba amefika wakati zoezi
la uchunguzi lina kamilika bado atafanyia kazi taarifa hizo kwa umakini
mkubwa ili kujiridhisha na utendajji kazi wa watumishi wa halmashauri
hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanwa akionesha sehemu ya nyaraka ambazo zinaonesha namna baadhi ya watumishi walivyoshiriki kufanya ubadhilifu wa fedha za madawati.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Gelasius Byakanawa (katikati) akiwa na katibu tawala wa wilaya hiyo,Upendo Wela (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Halamshauri ya wilaya hiyo Yohana Sintoo (kushoto).
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai,Yohana Sintoo akizungungunza wakati wa kikao hicho .
No comments:
Post a Comment