Wednesday, April 13, 2016

KENYA YATETEA MSIMAMO WAKE KUHUSU KUWARUDISHA WATAIWAN NCHINI CHINA

Na Mwandishi Wetu

Kenya imesema inaendela na msimamo wake juu ya suala la kurudisha kundi la Wataiwan nchini China, tendo ambalo limechukuliwa kama mwanzo wa uhasama.

“wamekuja kutoka China na tumewarudisha China” msemaji wa Wiziri wa Ndani Nchini Kenya, Mwenda Njoka aliiambia Shirika la Habari la Uingereza, Reuters.

PICHA: Johnny Chiang, afisa wa chama cha Kuomintang, akionesha video ya Raia wa Taiwan kuzuiwa na kituo cha polisi nchini Kenya, katika mkutano na vyombo vya habari uliofanyika jijini Taipei, tarehe 12/04/2016

Taiwan imekuwa ikijitawala tokea mwaka 1949, na kujitambua kama taifa kamili. Lakini China inakitaja kisiwa hicho kama sehemu yake. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohammed, ameiambia Reuters “tunaamini sera za ‘China moja’.”


China imewekeza mabilioni ya dola nchini Kenya. Kenya iliwazuia raia wa Taiwan pamoja na China kwa tuhuma za kuhusika na ubadhilifu wa mawasiliano, ambapo baadhi wameonekana hawana hatia. Lakini ripoti zinazotofautiana zimekuwa zikiibuka kuhusiana na kilichotokea tokea wakati huo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Taipei, raia 8 wa Taiwan walirudishwa ijumaa iliyopita na wengine 37 jumanne, ikijumuisha na wale ambao walionekana kutokuwa na hatia kwa mujibu wa mahakama.

Nairobi imedai Wataiwan 8 walirudishwa nchini China siku ya jumatatu na wengine 16 jumanne. Wakati wanarudishwa siku ya jumanne, shirika la Reuters liliripoti, maofisa wa Kenya walitumia mabomu ya machozi kuwalazimisha Wataiwan kutoka kwenye vyumba vyao vya rumande kupanda ndege, Waziri wa Mambo ya Nje wa Taiwan aliongeza kuwa mmoja wa walifukuzwa nchini Kenya ana uraia wa Marekani. Serikali ya Marekani imedai kulifanyia kazi suala hilo.

Serikali ya China imekuwa ikieneza dhana ya utaifa wao duniani bila kujali mtazamo wa Taiwan




No comments:

Post a Comment