Wednesday, April 23, 2014

CHADEMA YATOA ONYO, YAMRARUA MAKONDA VIPANDE VIPANDE

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa  angalizo na onyo kwa vijana wa CCM ambao wako kwenye maandalizi ya kuanza kufanya fujo zinazoratibiwa kimkakati kuharibu mchakato wa Katiba Mpya ili kuwapatia ‘fursa’ watawala kuweka visingizio vya kuzuia harakati za UKAWA kuuelimisha umma.

Taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari Jijini Dar es Salaam jana na Kurugenzi ya mawasiliano ya Chadema na kusainiwa na Afisa Utawala na Fedha Baraza la Vijana BAVICHA Bwana Daniel Naftal iliwataka CCM kutokujaribu  wala kudiriki kutekeleza hayo maagizo ya kuwashambulia wananchi kwenye shughuli zao mbalimbali na viongozi wa UKAWA.

Alisema kuwa Katika hilo wameomba kuwa wazi, kuwa wako tayari kusimama na kuwalinda viongozi wao.

  
Aliwataka wananchi kuungana na makundi mbalimbali katika jamii, taasisi, asasi za kiraia na watu wengine mashuhuri ambao wameamua kujitoa hadharani kusimamia maoni ya wananchi kama yalivyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya kwenye Rasimu ya Pili, ambayo inaeleza katika katiba ya sasa, ibara ya 8 inayosema mamlaka ya kuongoza nchi yote yatatoka kwa umma/wananchi.

Aidha pia alihimiza kutumia nguvu zote zilizojaa ushawishi wa hoja na mbinu halali dhidi ya njama za aina yoyote zinazofanywa kupindua na kuchakachua maoni.

“Leo pia tunaendelea kusisitiza kuwa hakuna kikundi chochote kinaweza kujitwalia mamlaka ya kwenda kinyume au kupindua maoni ya wananchi kwenye Rasimu ya Katiba Mpya, ambao ndiyo wenye hati miliki na nchi yao.”ni wazi watawala wanataka kupola na kubaka demokrasia kwenye jambo nyeti kama hili kwa manufaa ya CCM.

Alisema Bavicha  kwa kushirikiana na vijana wengine wenye machungu na Tanzania watashawishi, kuratibu na kusimamia hoja za msingi katika kuhakikisha kizazi cha sasa na vingine vijavyo, vinanufaika na matunda yatakayo andaliwa leo.

Alisema zimeanza kuonekana dalili za njama za wazi kabisa zinazofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia njia mbalimbali kutaka kutengeneza hali ya taharuki na kuwatisha wananchi wasijenge hoja za kudai maoni yao yaheshimiwe kwenye kuandika Katiba Mpya ya Tanzania.

“Njama hizo za kujenga hali ya hofu na kuibua sintofahamu ambazo zimekuwa zikizungumzwa na viongozi waandamizi wa chama hicho, zimeendelea kudhihirika tena baada ya chama hicho, kupitia kwa kada wake. Paul Makonda, kutoa tamko la kuhamasisha vurugu na ‘kuanzisha’ vita, kwa nia ya kuwatisha wananchi washindwe kudai katiba yao inayotaka kuporwa na CCM”alisema.

Naftal alisema Kada huyo ambaye anajulikana ndani na nje ya chama chake kwa namna alivyo mahiri wa kutumika kwa ajili ya maslahi binafsi ya watu au wakati mwingine hata dhidi ya chama chake, kwa ajili tu ya kutetea tumbo lake, amekuwa akitoa maneno ambayo kwa hakika yamezidi kuwachochea wananchi kujua kuwa CCM si chama cha siasa tena, bali genge la wabaka demokrasia.

Alisema kutokana na  Makonda kunukuliwa akitoa maagizo kwa vyombo vya dola na vijana wanaounda jeshi haramu la CCM (Intarahamwe), linalojulikana kwa jina la Green Guard kuanza kufanya mashambulizi dhidi ya viongozi wa UKAWA kwa sababu tu wameipiku CCM na mawakala wake, katika kujenga ushawishi kwa wananchi unaotokana na hoja zenye ushahidi wa takwimu za kitafiti na mtiririko wa mantiki katika kutetea maoni ya wananchi kwenye rasimu ya katiba.

Kauli hiyo ya Makonda ya kuwaagiza vijana wa Green Guard wajipange kufanya mashambulizi bila shaka kwa nia ya kuteka, kujeruhi, kutesa na hata kuua, ambayo imepata baraka za viongozi wakuu wa chama inadhihirsha kuwa Chama hicho ni
Interahamwe kikundi cha kijeshi kilichokuwa kinatumiwa na watawala kupambana kwa nguvu na kukandamiza demokrasia na wapinzani wa kisiasa wa serikali nchini Rwanda hadi kusababisha mauaji ya kimbari nchini humo.

Kauli ya Makonda ambayo Jeshi la Polisi nchini kupitia kwa msemaji wake, Advera Senzo limesema eti halina taarifa nayo, imedhihirisha kwa ushahidi kuwa kikundi cha ulinzi cha Green Guard huwa kinatumika kushambulia, kupiga watu, kuteka, kutesa na hata kuua kama ambavyo kimefanya mara kadhaa hususan wakati wa chaguzi ndogo.

Aidha Naftal alimuelezea Makonda wanamfahamu kwa kujulikana kwa umahiri wake wa kutanguliza tumbo lake na kulinda maslahi ya wakubwa wanaomtumia kwenye makundi ya ndani ya CCM.

“akiwa Moshi alikokuwa akiwalaghai (na kuwatapeli fedha akisingizia analipa ada) baadhi ya watu ambao huwa wanamtumia kuwa yuko chuoni anasoma, wakati hasomi, alikuwa akijulikana mji mzima kwa jinsi ambavyo mtu yeyote mwenye fedha angeweza kumtumia kwa namna mbalimbali ikiwemo kutoa matamko hali inayopelekea mara kadhaa kutumika na watu wa nje na ndani ya CCM kukihujumu chama hicho anachosema yeye ni mwanachama.”alisema

Aliongeza kuwa wakati wa uchaguzi mkuu wa chama hicho mwaka jana, baada ya kushindwa nafasi aliyokuwa akigombea, Makonda aliandika mambo mengi akionesha namna ambavyo CCM kinanuka rushwa na kimekubuhu kwa ubakaji wa demokrasia lakini kitendo cha kupachikwa cheo  alichonacho sasa ndani ya UVCCM  kimemfanya ale matapishi yake,na  anawaita ni wazalendo.

Alisema pamoja na makelele yake,  walau angelikuwa mwadilifu, bali hana hata chembe ya sifa hiyo na anatembea na lundo la tuhuma za ufisadi na ubadhirifu, huku mfano mzuri ni  kitendo chake cha kula fedha na kukwamisha uchaguzi wa Vijana wa Chipukizi wa CCM uliokuwa ufanyike mjini Morogoro.

“Tunaweza kusema mambo mengi kwa namna tunavyomjua, anajua kuwa hata jina analotumia SI JINA LAKE HALISI, lakini itoshe kusema kuwa tangu tulipomtangaza Nape Nnauye kuwa ni Vuvuzela namba moja ndani ya CCM na hadi leo anajulikana hivyo, hatukuwahi kujua kuwa mwingine anayemfuatia kwa ukaribu kwa uvuvuzela ni Paul Makonda ndio maana watu hawa wako kundi moja.

TAFADHALI ANDIKA MAONI YAKO HAPA CHINI


No comments:

Post a Comment