Tuesday, March 25, 2014

DUH: MASKINI YANGA WASHINDWA KESI, INATAKIWA KULIPA MILIONI 106

Dar es Salaam,

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea amri ya Mahakama Kuu (Kitengo cha Kazi) kukamata sh. milioni 106 za Klabu ya Yanga kutokana na mapato ya milangoni kwenye mechi zake, ili kuwalipa waliokuwa wachezaji wake Stephen Malashi na Wisdom Ndlovu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema tayari wameanza utekelezaji wa amri hiyo ambapo katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Rhino Rangers iliyochezwa Machi 22, mwaka huu mjini Tabora wamezuia sh. 9,221,250 ambazo ndizo zilizokuwa mgawo wa Yanga katika mchezo huo ulioingiza jumla ya sh. 38,655,000.

SOMA ZAIDI. . .


Alisema wachezaji hao walifungua kesi kortini kupinga mikataba yao na klabu hiyo kuvunjwa bila kulipwa haki zao za kimkataba. Malashi na Ndlovu walishinda kesi hiyo, hivyo korti kuwapa tuzo hiyo ya sh. milioni 106.

"Tunawakumbusha wanachama wetu (klabu za Ligi Kuu, vyama vya mpira wa miguu vya mikoa na vyama shiriki) kuzingatia mikataba wanayoingia na watendaji wao wakiwemo wachezaji, makocha na maofisa wengine," alisema Wambura.


Alisema iwapo wanataka kuvunja mikataba ya ajira, wafuate taratibu kwa vile hakuna mkataba ambao hauelezi jinsi ya kuvunjwa iwapo upande mmoja unataka kufanya hivyo.


No comments:

Post a Comment