Thursday, June 20, 2013

MKALI WA ‘THE SOPRANOS’ AFARIKI AKIWA NA MIAKA 51






Habari za kusikitisha na pigo kubwa kwa wapenzi wa sinema duniani pamoja na wale wanaofuatilia ‘series’ tamthiliya haswa ile maarufu ya Sopranos wamekumbwa na msiba mkubwa baada ya msanii maarufu wa tamthiliya hiyo kufariki dunia.


James Gandolfini,  anayeigiza kama kiongozi wa genge na kujulikana kama Tony Soprano katika filamu hizo za televisheni ya HBO "The Sopranos," alifariki ghafla leo akiwa na umri wa mikaka 51.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na mtandao wa Yahoo, Gandolfini alikuwa katika mizunguko 
jijini Rome, Itali katika mapumziko kabla ya kuelekea Sicily kwenye tamasha la filamu maarufu kama Taormina Film Festival ambapo aliugua. 

Kwa mujibu wa Yahoo, taarifa zinazotatanisha zilizotolewa kueleza chanzo cha kifo chake zilidai alikuwa na matatizo ya shinikizo la damu wakati taarifa nyinginze zikidai alipooza.

Msemaji wa televisheni ya HBO iliyoko Marekani ambao ndio wanaorusha vipindi vya Sopranos alidhibitisha kwa kusema “tumeshtushwa na kusikitishwa sana na kifo cha mwanafamilia mwenzetu. Aliheshimu kila mtu na kuwa mtaratibu sana na mtu mwenye upendo”

“kwa namna moja au nyingine alitugusa katika maisha yetu, kwa utani wake, upendo na utu. Mioyo yetu inaungana na mkewe na watoto wake katika kipindi hichi kigumu. Atakumbukwa sana katika familia yetu”


No comments:

Post a Comment