NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
MFUKO
wa Pensheni wa PSPF, umezindua ofisi
mpya mbili moja kisiwani Pemba na nyingine kisiwa cha Ukerewe mkoani Mwanza.

“Mtakumbuka
kwamba wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba kila mwaka, huadhimishwa wiki ya huduma kwa wateja
duniani, na kwa mwaka huu, Mfuko umzindua ofisi mpya kule Pemba na Ukerewe ili
kuboresha zaidi huduma zetu.”

Bi.
Maghimbi alisema, sambamba na ufunguzi wa ofisi mpya,
hapa
makao makuu mtaona tunaadhimisha kwa kushirikiana na washirika wetu kwenye
utoaji huduma mbalimbali, ili kuwapatia fursa wananchama wetu ya kupata huduma
kutoka taasisi hizo washirika.
Aliwataja
washirika hao ambao wameweka mabanda ya kutoa huduma kuwa ni pamoja na Mfuo wa
Taifa wa Bima ya Afya, (NHIF), benki za TPB, NMB, CRDB na Benki ya Walimu,
(MCB).

Miongoni
mwa wanachama wa PSPF waliofika kupatiwa huduma ni pamoja na Mkuu wa Mkoa
Mstaafu, Dkt. Ibrahim Msengi ambaye alisifu huduma za haraka zitolewazo na
maafisa wa PSPF.
“Kwa
kweli mimi nimeridhishwa na huduma niliyopatiwa hapa, nimefika hapa kufuatilia
malipo ya mirathi ya ndugu yetu, na nimepokelewa vizuri na kupatiwa huduma
stahiki bila ya ucheleweshwaji, hili ni jambo jema na niwapongeze PSPF kwa
uchapakazi wa namna hii.” Alisema Dkt. Msengi.
No comments:
Post a Comment