Thursday, March 27, 2014

KIBOKO :ASKOFU BILIONEA ALIYESTAAFISHWA NA PAPA, AMETUMIA MABILIONI KUJIRUSHA

Papa Francis amemsimamisha Askofu Franz-Peter Tebartz-van Elst wa Dayosis ya Limburg, Askofu huyo maarufu anayejulikana kama “Bling Bishop” kutokana na utata unaozunguka aina ya maisha anayoishi.

Hii imemtokea Askofu huyo mwenye umri wa miaka 53 alipotumia dola za Kimarekani milioni 42 (sawa na shilingi bilioni 68.8), katika jumba la kifahari huku akidaiwa kutumia dola 15,000 (sawa na shilingi milioni 24.5) kutengeneza bafu la kuogea pekee.


Kiasi hicho cha fedha kimetumika kutengeneza makumbusho, ukumbi wa mkutano, kanisa, pamoja na nyumba yake mwenyewe.

Mradi huo ulipitishwa na aliyemtangulia na ulikuwa na thamani ya dola milioni 7.5 (sawa na shilingi bilioni 12.2), lakini mwishowe bili hiyo ilipandishwa mpaka dola milioni 42.

Katika kitita hicho kilihusisha pia dola milioni 1 (sawa na shilingi milioni 1.6) kwa ajili ya bustani tu. Mwaka jana zaidi ya waumini 4000 waliweka saini zao kumkosoa kwa kutumia sadaka za kanisa kuendesha maisha yake ya gharama.

ANGALIA NA SOMA ZAIDI. . .


Anadaiwa pia aliidanganya mahakama kuhusu gharama za ndege aliyokodisha kwenda India kutembelea jamii maskini. Papa Fransis alilazimika kumstaafisha Askofu huyo wakati uchunguzi unaendelea.


Vatican haijasema uchunguzi huo utachukua muda gani katika Dayosisi hiyo ya Limburg huku ikikataa kueleza kwanini hawajamuondoa kabisa Askofu Franz-Peter.


No comments:

Post a Comment