Thursday, July 04, 2013

RAIS WA MISRI OUT, MIEZI 12 BAADA YA KUCHAGULIWA KIHALALI



HOFU YATANDA,  NINI HATMA YA MISRI

 
Jeshi la Misri limeng’oa madarakani rais wa kwanza kuingia madarakani kidemokrasia, Bw. Mohammed Morsi(Kushot) Bw. Morsi aliingia madarakani miezi 12 iliyopita kwa kuchaguliwa kidemokrasia nchini Misri baanda ya kupinduliwa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo Bw. Hosni Mubarak(Pichani Kulia akiwa jela).
SOMA ZAIDI...


Maelfu ya waandamanaji walikusanyika katika eneo la Tahir Square kumshinikiza Rais Morsi kuondoka madarakani lakini alikataa.

Hata hivyo Mohammed Morsi alikaidi agizo la masaa 48 lilitolewa na jeshi la nchi hiyo la kutafuta suluisho kufuatia maandamano hayo, lakini muda huo uliisha bila ya kupatikana ufumbuzi wa tatizo. 

Jana jioni kundi kubwa la wanaompinga Bw. Morsi walisikika wakishangilia katika jiji la Cairo, eneo la Tahir Square baada ya kutangaziwa na kiongozi wa upinzani huku akiongozwa na jeshi kuhusiana na kujiuzulu kwa rais huyo. 

Jeshi limesitisha katiba ya nchi hiyo na kuikabidhi nchi  kwa Jaji Mkuu wa nchi hiyo. Jaji Mkuu huyo ataapishwa kama rais na kutakiwa kuahidi kuitisha uchaguzi wa kidemokrasia wa kuchagua rais mwingie.

Wakati viongozi wa serikali ya Bw. Morsi pamoja na Morsi mwenyewe wakiwa chini ya ulinzi mkali, Rais wa Marekani Barack Obama ameonyesha wasiwasi wake kuhusiana na kitendo hicho na hatma ya nchi hiyo na kusema ni muhimu Misri kuongozwa na serikali ya kiraia.

Bw. Obama alikataa kusema kama ni serikali ya Bw. Morsi au ya aina gani inatakuwa kuingia au kurudi madarakani. Naye katibu mkuu wa umoja wa mataifa Bw. Ban Kimoon amewataka wananchi wa Misri kuwa watulivu katika kipindi hichi.


No comments:

Post a Comment