‘Hatutakubali watu wavuruge nchi yetu kwa tamaa zao tu za umaarufu
wa kisiasi, hili hapana, atakaye jaribu tutamchukulia hatua zinazohusika, na
aliyemuongoza naye pia
hatutamuacha, hata kama ana mapembe makubwa kiasi gani,
tutayakata tu’
Hayo ni maneno ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Jakaya Kikwete akiongelea vurugu zinazoendelea Mtwara. Rais alielekeza
lawama kwa wanasiasa akidai kuwa wao ni sehemu ya kuchochea vurugu hizo.
Katika vurugu hizo, polisi wamedai kukamata zaidi ya watu 90
jana waliohusishwa na matukio mbalimbali yanayohusisha vurugu hizo ikiwa ni
pamoja na mikusanyiko katika makundi yasiyo maalumu pamoja na uharibifu wa
mali.
Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara Linus Sintumwa amekanusha
kuwepo kwa mtu yeyote kuuwawa katika vurugu hizo ambapo vyombo mbalimbali vya habari
vimeripoti vifo kutokea.
Vurugu za Mtwara zimetokana na vipeperushi vyenye ujumbe
uliosambazwa siku za karibuni na watu wasiojulikana ukiwataka wananchi wa
Mtwara kubaki nyumbani kusikiliza bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini
iliyosomwa jana na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Mhongo.
Hatma ya mgogoro huo itajulikana leo baada ya kamati ya
uongozi ya bunge kuwakilisha mapendekezo yake kama ilivyo agizwa na Spika Anne
Makinda hapo jana ambapo shughuli za Bunge zililazimika kusimama.
Mtwara ni moja wapo ya mikoa masikini zaidi nchi Tanzania,
ambapo hakuna viwanda vikubwa mkoani humo vyenye kutoa ajira. Wanamtwara
wanaolala mika walikuwa na ndoto ya kuona gesi hiyo inabaki mkoani humo ili kuanzisha
miradi itakayo wakomboa kiuchumi na kijamii.
No comments:
Post a Comment