Monday, May 21, 2018

TAMASHA LA 7 LA 4CCP LAZINDULIWA HAYDOM MKOANI MANYARA


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akimsikiliza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga mara baada ya kuwasili kwenye kituo cha Utamaduni cha Haydom cha 4CCP kilichopo mjini Haydom kwa ajili ya kuzindua maandalizi ya Tamasha la Saba la 4CCP linalotarajiwa kufanyika kuanzia Tarehe 3-6 mwezi Oktoba mwaka huu mjini Haydom wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara.

Katibu Mkuu Bi Suzan Mlawi pia ametembelea jamii za makabila manne makuu ya Afrika yanayopatikana katika kituo hicho na kujionea nyumba na tamaduni mbalimbali kutoka kwa wananchi wa Jamii za Wahzabe, Watatoga, Wabantu na jamii ya Wakhosain , Kulia ni Nelson Faustine Afisa Miradi wa Kituo cha 4CCP Haydom.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akimsikiliza Bw. Nelson Faustine Afisa Miradi wa Kituo cha Utamaduni cha 4CCP Haydom wakati alipokuwa akiangalia ngoma ya kabila la Wahadzabe wakati alipotembelea katika kituo hicho leo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akimsikiliza Bw. Nelson Faustine Afisa Miradi wa Kituo cha Utamaduni cha 4CCP Haydom wakati alipokuwa akiangalia ngoma ya kabila la Wahadzabe wakati alipotembelea katika kituo hicho leo kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga na Eliminata Awet Mratibu wa kituo cha Utamaduni Haydom.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akimsikiliza Bw. Bi Eliminata Awet Mratibu wa Kituo Cha Utamaduni Haydom cha 4CCP wakati akimpa maelezo kuhusu tamaduni zinazopatikana kituoni hapo kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga na Nelson Faustine Afisa Miradi wa Kituo cha 4CCP Haydom


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akimsikiliza Bw. Nelson Faustine Afisa Miradi wa Kituo cha Utamaduni cha 4CCP Haydom wakati alipokuwa akiangalia ngoma ya kabila la Watatoga alipotembelea katika kituo hicho leo.




Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akiongozana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga na Eliminata Awet Mratibu wa Kituo cha Utamaduni 4CCP cha Haydom alipokuwa akielekea kuangalia nyumba za makabila hayo kulia ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Haydom Dk. Emanuel Nuwass.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi Bi Eliminata Awet Mratibu wa Kituo cha Utamaduni cha 4CCP Haydom wakiangalia nyumba ya wanyilamba wakati alipotembelea katika kituo hicho leo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi na Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wakitoka nje ya nyumba ya kabila ya Wanyiramba huku wakiongozwa na mzee Salum Shaban Mwakilishi wa wabantu na aliyekuwa akitoa maelezo kuhusu tamaduni za kabila hilo alipokuwa akiangalia nyumba ya kabila la Wanyiramba wakati alipotembelea katika kituo hicho leo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akiakiondoka mara baada ya kutembelea nyumba ya Wanyiramba na Wanyisanzu inazopatikana katika Kituo cha utamaduni cha 4CCP Haydom alipotembelea katika kituo hicho leo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akionyeshwa picha mbalimbali zinazoonyesha matukio ya Kituo cha Utamaduni cha 4CCP Haydom wakati alipotembelea katika kituo hicho leo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akimsikiliza Bw. Edward Mashimba Mwenyekiti wa Kabila la Wahdzabe wakati akitoa maelezo kuhusu nyumba ya kabila hilo inayopatikana katika Kituo cha Utamaduni cha 4CCP Haydom wakati alipotembelea katika kituo hicho leo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akipiga picha ya pamoja na Bw. Edward Mashimba Mwenyekiti wa Kabila la Wahdzabe pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga, kulia ni Mratibu wa Kituo hicho Bi. Eliminata Awet.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tamasha hilo uliofanyika leo kwenye kituo cha Utamaduni cha 4CCP mjini Haydom.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga wakifurahia jambo wakati MC Pilipili alipokuwa akizungumza katika uzinduzi huo.


Baadhi ya wananchi wa Jamii za Watatoga, Wahadzabe Wakhosain na wabantu wakiwa katika hafla hiyo.


Jamii ya watatoga wakifuatilia hafla hiyo


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akizindua rasmi maandalizi ya tamasha hilo.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi , Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu na Mratibu wa kituo cha Utamaduni cha 4CCP cha haydom wakipiga makofi mara baada ya uzinduzi huo.




Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akiwa katika picha ya pamoja na jamii hizo pamoja na viongozi wa kituo hicho na Halmashauri ya Mbulu.




Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akivishwa mgorole na wazee wa kimila.







Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akizungumza na jamii hizo wakati wa uzinduzi huo

No comments:

Post a Comment