Tuesday, July 26, 2016

TAARIFA ZA KUPOTEA KWA MTOTO GERALD DAVID BWANAMGANGA

Mtoto  GERALD DAVID BWANAMGANGA anayetafutwa na wazazi wake.

Mtoto GERALD DAVID BWANAMGANGA ambaye anatafutwa na wazazi wake, ana umri wa miaka MIWILI NA NUSU. Amepotea jumapili tarehe 25/7/2016 mida ya saa 09 (tisa) mchana huku juhudi kubwa ya kumtafuta inayofanywa na wazazi, ndugu zake zikiwa bado hazijafanikiwa. Mara ya mwisho mtoto GERALD DAVID BWANAMGANGA alikuwa akicheza na wenzake KANISANI akiwa amevaa T-SHIRT NYEKUNDU na SURUALI YA KAKI maeneo ya BABANA, GONGO LA MBOTO jijini DAR ES SALAAM.

Tunaomba Watu, Mtu yeyote atakayeweza kumuona, basi anaweza kumfikisha Kituo Cha Polisi kilicho karibu nae. Au unaweza kuwasiliana na wazazi wa mtoto kwa namba 0713 040 615 ama 0712 185 226. Pia unaweza kupiga simu namba 0675 306 990.

 Mtoto  GERALD DAVID BWANAMGANGA anayetafutwa na wazazi wake.

Lakini Endapo mtu atamuona basi anaweza kutoa taarifa Polisi au hata Pia Kutoa taarifa kupitia makundi mbalimbali ya Whatsapp ambayo tunaamini pia taarifa itawafikia haraka wazazi au hata ndugu kama ambavyo taarifa ya kupotea kwake ilivyoweza kutufikia sisi na kuamua kutoa msaada wa kutangaza kupitia hapa.

Tunajua ni jinsi gani Maumivu wanayoyapata wazazi wake lakini Tunamuombea kwa Mungu amlinde huko aliko na Malaika wake wamrudishe mtoto wetu GERALD DAVID BWANAMGANGA Salama Salimini kwenye himaya ya wazazi wake.

Tunatoa pole kwa Wazazi kwa kupotelewa na Mtoto wao Kipenzi lakini tunapenda kuwaambia kuwa Wamwamini Mungu kwa maana Kila hatua wazikabidhizo kwake na kuamini basi Mungu atawatendea.

TUNAOMBA MSAADA KUSAMBAZA TAARIFA HIZI.


No comments:

Post a Comment