Akizungumzia kukosekana Kwa huduma hiyo ya Maji, Kaimu Meneja Uhusiano wa DAWASCO, Bi. Everlasting Lyaro, ameeleza sababu ya kuzimwa kwa mtambo wa Ruvu Juu, ni kumruhusu Mkandarasi (WABAG) kuunganisha mtambo mpya wa Maji na ule wa zamani, ambapo baada kukamilika kwa kazi hiyo, uzalishaji wa Maji utaanza mara moja.
“Tuko kwenye hatua ya mwisho ya kuunganisha mtambo mpya wa Maji na ule wa zamani, kazi hii ikikamilika, uzalishaji utapanda kutoka wastani wa lita Milioni 70 hadi kufikia lita Milioni 106 kwa siku hivyo kuweza kutimiza lengo letu la kumtua mama ndoo ya Maji kichwani” alisema Lyaro
Lyaro, ameeleza kuwa kuzimwa kwa mtambo huo, kutasababisha maeneo ya Mlandizi, Kibaha, Kibamba, Mbezi, Kimara, Ubungo, Kibangu, Makuburi pamoja na eneo lote la Tabata, Segerea hadi Kinyerezi kukosa huduma ya Maji.
Hivyo, ametoa wito kwa wateja na wananchi wote kuhifadhi Maji ya kutosha na kuyatumia kwa matumizi muhimu na lazima ili kukidhi mahitaji yao kwa kipindi chote cha kukosekana kwa huduma hiyo.
No comments:
Post a Comment