Sunday, May 04, 2014

INATISHA, NI KWELI, MZIMU LIVE (VIDEO) WAMKUMBA JAMAA NA KUMBURUZA


Angalia kipande cha video kinachosambaa sasa hivi kwenye mitandao kinachomuonesha mtu aliyepigwa na kuangushwa na kitu kisichojulikana na wala hakionekani zaidi ya kivuli. Tukio hilo lilinaswa na kamera za CCTV katika corridor ambapo mtu aliyejifunika kichwani  kwa kutumia hood alipokumbwa na mkasa huo.

Picha hiyo haina sauti, inaelekea ni kamera ya ulinzi ndio ilikamata tukio hilo, kwani kamera hiyo inaonesha haina microphone kwaajili ya kunasa sauti.

Video hiyo inaonesha mtu huyo alipofika mwisho wa korido kivuli kisichokuwa na sura kilitokea kusikojulikana kinaonekana. Jamaa na kujiamini kwake kote ghafla kulionekana kupotea baada ya kuvamiwa na kudondoshwa chini, kabla ya kufanya lolote alishikwa mguu na kuanza kuburuzwa huku akiwa mgongo chini.
(ANGALIA VIDEO LIVE UONE, BOFYA CHINI)



Mwathirika huyo wa janga la mzimu, ambaye hakuweza kutambuliwa, lazma alihisi siku zake ndio zimefikia mwisho, aliinuka upesi na kutimua mbio kuelekea alikotokea.




TAFADHALI SHUKA CHINI UTOE MAONI YAKO. . .

No comments:

Post a Comment