Dodoma.
Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wanaunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wamepanga
kufanya mikutano ya hadhara nchi nzima ili kuongea na wananchi juu ya msimano
wao wa kususia Bunge hilo.
Akizungumza jana na waandishi wa habari mjini hapa
Mwakilishi wa kundi hilo Profesa Ibrahim Lipumba alisema kuwa katika kikao chao
wamekubaliana kuzunguka nchi nzima kufanya mikutano ya hadhara kwa wananchi
ambapo wataanza mkutano huo kesho kutwa Jumamosi Zanzibar na kusema mkutano huo
utahudhuliwa na wajumbe wa kundi hilo watakaokuwa hawana dharura.
“Tumekubaliana kwamba siku ya Jumamosi kwa pamoja wajumbe
wote ambao hatuna dharula tutaenda Zanzibar kutakuwa na mkutano wa hadhara
kuaznia saa nne asubuhi na tutaondoka na siku hiyo na Boti ya saa moja asubuhi
kuelekea Zanzibar na katika mkutano huo tutaeleza yaliyojiri katika bunge
maalaum.
TAFADHALI ANDIKA MAONI YAKO CHINI HAPA. . .
No comments:
Post a Comment