Thursday, April 24, 2014

RAIS KIKWETE AMCHANA LAIV DKT MWAKYEMBE MBELE YA WAANDISHI (SOMA HAPA)

Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa anaumia na kuchukizwa na kitendo cha ongezeko matukio ya dawa za kulevya huku Tanzania ikiwa ndio njia kwa kutumia viwanja vyake vya ndege  vya kimataifa (JKNI na KIA)kuwa ndio uchochoro.

Rais akizungumza katika hafla ya uzinduzi na kuweka jiwe la msingi katika uwanja mpya wa ndege ambao utakuwa ni jengo la tatu (terminal 3) katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JKNI) amemtaka na kumpa mwezi mmoja Waziri  wa Uchukuzi, Dkt Harison Mwakyembe kufanya kazi na kwamba hajaridhishwa na utendaji wake.

Alisema kitendo cha watu wanaofanya Biashara ya dawa za kulevya kuingia na kutoka nchini kirahisi na kwenda kukamatiwa nje ya nchi kinamuuma na kumkera kwani ni aibu kwake na kwa taifa na inatoa taswira kuwa wote wanafanya biashara hiyo hivyo amechoshwa na porojo anataka kazi ianze mara moja.

Rais  Kikwete alisema ni wazi  uzinduzi wa jengo hilo la kimataifa utaongeza changamoto kwani utakuwa na idadi kubwa ya watu, watendaji waelewe kuwa kama hakuna mbinu mbadala ya kudhibiti uingizaji dawa za kulevya ni tatizo.


“Mna wafanyakazi wachache, hivyo wenye dawa za kulevya wanapita watakavyo, je jengo hili litakalokuwa na wafanyakazi wengi zaidi na abiria milioni sita si itakuwa biashara huria!” alisema Rais Kikwete

“tena wanaopita au kukamatwa nasikia wanamuziki, wasanii, au mkiwaona ndio oya oya piteni. Aibu sana, inaniuma na kuniumiza mno nawambia haiwezekani ni uzembe”alisema Rais

Aliongeza kuwa afurahishwi na utendaji wa Waziri Mwakyembe ndio maana anamuuliza kila saa hivyo akikaa na watendaji wake wasinong’one


“Sifurahishwi na utendaji wako Waziri na nyie Mkurugenzi Bw Suleiman na Mwenyekiti wa Bodi mkielezwa na Waziri muelewe ni maagizo yangu na yasipotekelezwa nitaanza na nyie hasa we Suleiman” aliongeza kwa msisitizo.

SHUKA CHINI UANDIKE MAONI YAKO...


No comments:

Post a Comment