Monday, April 28, 2014

MAAJABU YA DUNIA: MTOTO WA MIEZI 5 AOTA MKIA WA INCHI 5, MAMA ACHANGANYIKIWA

Mama mmoja aliwabembeleza madaktari kumfanyia opereshen mtoto wake baada ya kuona anaota mkia ambao mpaka sasa una urefu wa inchi 5. Mtoto huyo mwenye umri wa miwzi 5, alizaliwa na tatizo la uti wa mgongo (spina bifida).

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa tarehe ijumaa(25/04/2014) kwenye mtandao wa Metro, Nou Nou alipatwa tatizo hilo ambalo linaendelea kukua  ambalo husababishwa na kutokea kwa nafasi katika uti wa mgongo. Katika kipindi cha siku tano baada ya kuzaliwa mama yake aligundua kamkia kanaanza kuota na sasa mtoto huyo ana mkia unaoonekana kabisa.

Akiwa na wasi wasi kuhusu makuzi ya mtoto wake, mama yake Nou Nou amewaomba wapasuaji katika hospitali ya Changsha nchini China, kutafuta namna ya kuondoa mkia huo.


Hata hiyvo madaktari hao wanasema hakuna wanachoweza kufanya kwani mkia huo umeungana na mishipa ya fahamu, na kama wakiondoa atapata kilema cha maisha. Tatizo hilo hutokea mara chache na kumpata mtu mmoja kati ya watu 1000. Lakini pia kutokea ni nadra sana na hasa kukua kwa mkia kama huo.

TAFADHALI SHUKA CHINI UANDIKE MAONI YAKO. . .


No comments:

Post a Comment