Wednesday, January 29, 2014

AMUUA MWENZIE KWA KISU, KISA- POMBE,MAPENZI

Songea

Jeshi la Polisi mkoa wa Ruvuma linamshikilia  Fikiri Mapunda (32) mkazi wa kitongoji cha Msirikasi kilichopo kijiji cha Malunga  kata ya Tingi wilaya ya Nyasa kwa tuhuma za kumchoma kisu shingoni  Yakobo Mbungu (29) mkazi wa kitongoji hicho  wakati wakinywa  pombe za kienyeji  ambapo alifariki  muda mchache wakati akikimbizwa kwenye hospitali ya Wilaya ya Mbinga kwa ajili ya matibabu.

Kamanda wa Polisi  mkoa wa Ruvuma  Deusdedit Nsimeke  amesema tukio hilo limetokea  juzi majira ya saa nne usiku kwenye klabu za pombe za kienyeji  ,ambapo Marehemu na mtuhumiwa walikuwa wakinywa pombe ghafla  walianza kurushiana maneno  ambapo inadaiwa  chanzo cha ugomvi huo  ni wivu wa mapenzi.

Amefafanua zaidi kuwa, Yakobo anadaiwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Vumi Kawonga ambaye kwa siku za nyuma kabla ajaanza kuwa na mahusiano na mapunda alikuwa ni mpenzi wa  marehemu.

Ameongeza kuwa, siku ya tukio inadaiwa mapunda na Marehemu walikutana  kwenye hicho klabu ambapo walianza  kurushiana maneno na kila mmoja alimtuhumu mwenzake kuwa alimuibia mpenzi wake  na baadaye ulizuka ugomvi mkubwa  kisha Yakobo alichomwa kisu na kumwaga damu nyingi ambazo zilisababisha apoteze maisha.

Amesema, mara baada ya uongozi wa serikali ya kijiji kupata taarifa za mauaji hayo ulimkamata mtuhumiwa na kumpeleka kwenye kituo cha polisi cha Mbambabay ambapo  anaendelea kushikiliwa na Jeshi hilo hadi upelelezi wa polisi utakapokamilika kwa ajili ya kumpeleka mahakamani.


No comments:

Post a Comment