Friday, December 20, 2013

BREAKING NEWS: AJALI MBAYA YAUA WANNE, TABORA

Na mwandishi wetu, Tabora

Habari zilizotufikia ni kwamba leo majira ya saa tano asubuhi gari na T 829 AHA ISUZU lilokuwa limebeba watu waliokuwa wanakwenda mnadani limepata ajali mbaya na kusababisha vifo vya watu wanne hapo hapo na wengine kumi kujeruhiwa vibaya.

aitha katika ajali hiyo watu wengine 15 wana majeraha madogo madogo, na kufanya idadi ya majeruhi kuwa ni 28, majeruhi wote wanapata huduma katika hospitali ya Mkoa wa Tabora ya Kitete.

Gari hilo lililokuwa likiendeshwa na Ally Athmani Kufula, lilikuwa limebeba watu wasiopungua 30, lilidaiwa kupata ajali baada ya kupasuka tairi la mbele upande wa kushoto na kusababisha dereva kushidnwa kulimudu na kusababisha ajali hiyo katika eneo la Lalangulu, mkoani Tabora.

No comments:

Post a Comment