Friday, June 28, 2013

OBAMA KUMTEMBELEA MANDELA





 

Baraka Obama atawasili leo nchini Afrika ya Kusini na kutegemewa kutembelea mahali alipokuwa anaishi rais wa kwanza wa taifa hilo ambaye yuko maututi kitandani kwa matatizo ya kupumua.

Rais Obama na Bw. Mandela  ambaye wanatarajiwa kukutana na kwa muda usiojulikani na kuishia kupiga picha tu.

Kutokana na afya ya Mandela kuwa mbaya, wawili hao hawatarajii kukaa muda mrefu hata mbele ya kamera za waandishi wa habari.

Rais huyo wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini ambaye atatimiza miaka 95 mwezi ujao, alikimbizwa hospitali wiki tatu zilizopita akiwa na matatizo ya mapafu.

Afya ya Bw Mandela imezidi kuwa mbaya siku chache kabla ya ujio wa Obama nchini Afrika Kusini, lakini pia hali hiyo haijabadilika na kusababisha Rais Jacob Zuma kufuta ziara yake nchini Msumbiji.


“anaendelea vizuri sana leo” alidai Bw. Zuma baada ya kumuona Mzee Mandela jana jioni ikiwa ni mara ya pili katika kipindi kisichozidi masaa 24.

Raia wa nchi hiyo wamekuwa wakimuombea Mzee Nelson ‘Madiba’ Mandela katika sala zao aendelee kupona.

"Siwezi kudanganya, hali sio nzuri” alisema mtoto wa kike wa Mzee Mandela, Makaziwe Mandela.  "tukiongea naye anajibu na kujaribu kufungua macho-bado tunaye”

"Lolote laweza kutokea, lakini ningependa kusisitiza tena kwamba ni mungu tu ndio anajua ni saa ngapi ataondoka” aliiambia radio moja nchini Afrika Kusini.


No comments:

Post a Comment