Thursday, January 24, 2013

NYOTA WA DESTINY CHILD AFUNGUKA


Nyota wa kundi la Destiny Child, Michelle Williams amefunguka kuhusiana na vita aliyekuwa nayo dhidi ya sononi ili kusaidia wengine wanaokabiliwa na tatizo hilo

Muimbaji huyo kwanza alipata wakati mgumu akiwa mtoto kutokana na maisha duni, alisema amekuwa akipambana na giza kwa miaka kadhaa

Lakini nyota huyo ambaye hivi karibuni ameungana na wanamuziki wenzake wanaounda kundi la Destiny akiwemo Beyonce na Kelly Rowland alisema sasa mambo yanaenda vizuri

Muimbaji huyo mwenye hofu ya mungu sasa anakusudia kutoa ushauri kwa wanawake wanaokabiliwa na matatizo "Tuna nguvu jaribu kusali na kwenda kanisani kuhusiana na shida yako mungu atakuponya"


No comments:

Post a Comment