Friday, November 02, 2012

TARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


BUSINESS TIMES LIMETED

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUVAMIWA NA KUDHURIWA KWA MHARIRI WA BUSINESS TIMES, MNAKU MBANI

AGOSTI mosi mwaka huu, Mhariri wa Gazeti la Business Times linalotoka mara moja kwa wiki (kila Ijumaa), alijeruhiwa kwa risasi akiwa njiani kurudi nyumbani kwake Mbagala, Dar es Salaam.

Tukio hilo lilitokea saa mbili usiku, eneo la Mtoni Madafu, akiwa katika gari binafsi aina ya Noah inayomilikiwa na Bw. Mgeme Singili (namba ya gari imehifadhiwa) na abiria wengine wakitokea Kariakoo kwenda Mbagala.

Walipofika Mtoni Mtongani, gari hiyo ilisimamishwa na majambazi sita waliokuwa katika pikipiki. Majambazi hao walichomoa funguo ya gari na kudai wapewe begi lenye pesa kutoka kwa mmoja wa abiria waliokuwa ndani ya gari hiyo.

Abiria waliwajibu hakuna mtu mwenye begi la pesa ndipo majambazi hao walipoanza kufyatua risasi mfululizo (zisizo na mwelekeo), wakiwalenga abiria ndipo moja kati ya risasi hizo ilimpata Bw. Mnaku Mbani.

Bw. Mnaku alipigwa risasi juu ya mdomo, upande wa kulia ikatoke kwenye shavu la kushoto. Risasi hiyo iliondoa meno matatu ya juu.

Uongozi wa kampuni umezungumza na Bw. Mnaku ili kuelezea mazingira ya tukio hilo lakini kutokana na maumivu aliyonayo, hatukuweza kuzungumza naye kwa kirefu.

Hali ya Mnaku inaendelea kuimarika na anendelea kupata uchunguzi wa madaktari katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Zaidi ya jeraha hilo, Mnaku hana majeraha mengine katika mwili wake kutokana na tukio hilo.

Uongozi wa Makampuni ya Business Times Limited unaendelea kufuatilia hali ya Mnaku kwa karibu ili kuhakikisha anapata huduma na uangalizi unaostahili.

Taarifa Za Polisi

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, David Misime alisema mmiliki wa gari hiyo ni mfanyabiashara ambapo uchunguzi wa polisi umebaini kuwa majambazi hao waliamini kuwa amebeba pesa, hivyo baada ya kushuka kwenye pikipiki walidai kupewa pesa.

Alisema katika gari hiyo watu watatu walijeruhiwa kwa risasi akiwemo Bw. Mnaku, mwingine katika bega la kushoto na watatu alikwaruzwa na risasi kisogoni.

Jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na watahakikisha wahusika wote wanatiwa mbaroni haraka iwezekanavyo.

Nachukua fursa hii kuwapa pole wanahabari wote nchini, ndugu jamaa na marafiki wote kwa tukio hilo, tuendelee kuwa pamoja na kushikamana kuondoa uhalifu kila mmoja katika nafasi yake.

Imma Mbuguni
Mhariri Mtendaji
Majira

PICHANI 

MNAKU MBANI AKIPEWA POLE NA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA BTL LEO 






No comments:

Post a Comment