Wednesday, February 17, 2016

POLENI SANA WEMA SEPETU NA IDRISSA SULTAN KWA KUPOTEZA MAPACHA, MUNGU AWATIE NGUVU KATIKA KIPINDI HICHI KIGUMU

A photo posted by Idris Sultan (@idrissultan) on


Katika hali ya kusikitisha Idrisa Sultani aliandika mapema leo alfajiri kwenye wall yake ya instagram (Pichani Juu) kwa huzuni na masikitiko makubwa baada ya kupoteza watoto mapacha. Tetesi zilianza kuzunguka katika mitandao ya jamii, kuhusu ujauzito wa Wema Sepetu (ambaye ndie aliyekuwa mjamzito wa watoto hao) kuharibika.

Tafrisi
“Kwa mapacha wangu niliowatarajia,
Mmekuja haraka sana kwenye maisha yetu, haraka sana na kuondoka. Sikupata nafasi ya kukutana nanyi. Kuna mengi nataka kusema. Nna mawazo mengi kichwani mwangu, yanatosha kunifanya nichanganyikiwe. Pamoja na kwamba mliishi kwa muda mfupi wa wiki 13, ninawapenda sana. Natamani ningewabeba, natamani kuwashika. Naomba tupate nafasi ya kukutana katika maisha mengine. Mungu amewaleta na kuwachukua kwa mpango wake na hatuwezi kulalamika bali kuomba kuwa hayo yote ni kwa mpango wenye nia njema kwetu. Tumejufunza kwa uchungu lakini hatutoacha kuendelea kujaribu tena na tena na nnaapa tutakapojaliwa kupata kaka na dada zenu tutakuwa tayari kwaajili yao.
Wenu mtiifu
Baba

Imma Matukio inaungana moja kwa moja kuomboleza msiba huo na wawili hao (Idrisa na Wema). Tunatumia fursa hii kuwapa pole wazazi hao waliotegemea kupata watoto mapacha. Mungu awaweke mahali panapostahili. Tunawaombea subira katika kipindi hiki na kuwataka Watanzania na mashabiki wote wa wool ha kuwa na moyo wa uvumilivu. Mangu awape nguvu na ujasiri katika kipindi hiki
Amina





No comments:

Post a Comment