Tuesday, January 26, 2016

KIKONGWE ANUSURIKA KUFA KWA MOTO, KISA MTOTO WA MIAKA 6 ACHOMA MOTO NYUMBA

Na Mwandishi Wetu, Tanga

WATOTO wa  kiume wenye umri wa miaka sita majina tunalihifadhi amechoma moto nyumba yao yenye thamani ya zaidi ya shilingi million 300 kwa kutumia kibiriti hali iliyosababisha kuteketea yote, baada ya magodoro katika chumba chao kushika moto ikiwemo vifaa vya magari matairi  vilivyokuwemo ndani ya chumba hicho.

 Akizungumza na Majira mfanyakazi wa ndani Semeni Masele 20 alisema aliona chumba cha watoto kikiwa kinawaka moto na moshi mkubwa ambapo alilazimika kuwatoa nje akiwemo Bibi kikingwe mwenye umri wa zaidi ya miaka 100 kisha kuwahifadhi kwa majirani zao na kulazimika kukimbilia faya kuomba msaada.


Semeni alisema baada ya kuona hali tete aliwapigia simu Askari wa zimamoto lakini  alipoona namba haipokelewi alilazimika  kukondi pikipiki na kwenda fanya kuomba msaada kwa lengo la kuokoa mali zilizokuwepo  ndani.

Tukio hilo la kusikitisha limetokea juzi majira ya saa 14:30 kijiji cha Mikanjuni  Tarafa ya Ngamiani kati kata ya Mabawa wilayani Tanga ambapo Tanesco na askari wa kikosi cha zimamoto walifanikiwa kufika katika eneo la tukio na kuzibiti  moto huo usizingile nyumba za majirani ambapo nyumba hiyo iliteketeza vyumba vinne kati ya vyumba saba.

Uchunguzi wa awali uliofanywa na Gazeti hili katika eneo la tukio ulibaini kuwa watoto hao walikuwa wawili ambapo mmoja alikuwa na miaka sita na mwingine saba baada ya chakula cha mchana waliambiwa na dada yao Semeni walale lakini cha kushangaza mtoto huyo  alikuta box la vibiriti ndani na kuwasha kisha kuchoma box hilo hali iliyosababisha matairi ya gari yaliyokuwa  ndani kuteketea kwa moto na kusababisha moshi mkubwa.

Kwa upande wake wakazi wa Mikanjuni walipongeza hatua ya Tanesco kufika kwa wakati kuzima umeme licha ya kuwa miundombinu ya nyumba ilikwa imekushika moto lakini jitihada zilionekana ambapokikosi cha zimamoto kilifanikiwa kuzibiti moto huo mkubwa ambao ungeweza kuteketeza nyumba za mtaa mzima katika eneo hilo.

“Sisi wananchi wa mkoa wa Tanga hatutambui namba ya kikosi cha uwokoaji cha zimamoto pindi majanga yanapotokea hivyo tunaomba kuelimishwa kwa kutangaza namba zao ili tuweze kunusuru mali wakai wa majanga” walisema baadhi ya wananchi katika tukio hilo.

Akizungumzia tukio kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Mihayo Msikhela  alisema tukio hilo limetokea juzi majira ya saa nane mchana baada ya watoto hao kutakiwa kwenda kulala na dada yao ambaye ni mfanyakazi wa ndani ambapo mtoto wa kiume alichukuwa kibiriti na kuchoma box kisha moto huo kuteketeza magodoro  ikiwemo  viashiria vya vimiminika.

Hata hivyo kamanda Msikhela aliwataka wananchi kuacha tabia ya kuweka vitu vya hatari ndani ya vyumba vya kulala watoto ili kunusuru madhara kama hayo yasitokee.

“Ninawaomba wananchi wa mkoa wa Tanga kuwa makini wakati wa kuwalea watoto kuondoa thana ndani ya vyumba vyao vya kulala ili kunusuru madhara pamoja na majanga yasitokee kutokana watoto ni watu wa kujaribu pindi anapoona kitu anataka kukitumia bila kuchukuwa tahadhari yeyote.

Top of Form
Bottom of Form




No comments:

Post a Comment