Mgahawa mmoja nchini India unakuwezesha kula chakula na wafu…najua unashangaa, ndio wafu…watu waliokufa. Hoteli hiyo imejengwa makaburini na kuzunguka makaburi ya zamani, hivyo makaburi yako ndani kama unavyoona pichani.
Mmiliki wa hoteli hiyo iliyoko Ahmedabad, kule wanakotoka
Wahindi wanaoongea kiGujrati, nchini India, anasema biashara ya makaburini inalipa sana.

Yeye anasema makaburi hayo yamekuwa kivutio kikubwa na
yanaleta bahati nzuri. Biashara yetu imeendelea kufanikiwa sababu ya makaburi
hayo. Yanawapa watu mvuto tofauti. Tumeyaacha kama yalivyo, wateja wetu wala
hawana shida.
SOMA ZAIDI . . .
SOMA ZAIDI . . .


“Tunaanza siku kwa kutoa heshma kwenye makaburi hayo, kisha tunayafuta
vizuri alafu tunayafunika na kitambaa alafu tunaweka maua mazuri, ni muhimu
sana kuheshimu wafu” alisema Kutti.
"Wateja kwa upande mwingi hawajali uwepo wa wafu katika
hoteli yetu, wanakuja kunywa chai na mikate bila wasiwasi wowote" alimaliza Kutti.
No comments:
Post a Comment