Saturday, March 15, 2014

HAYA MNAOTUMIA HEINEKEN BIA, HEINEKEN YASUSA KISA MASHOGA KUTENGWA

Katika taarifa iliyotufikia muda si mrefu, imeeleza kuwa kampuni mbili kubwa kuliko zote nchini Marekani za kutengeneza bia zimejitoa katika udhamini wa matembezi ya hiari ya siku ya Mtakatifu Patrick (St. Patrick's Day) kwa sababu wasenge na mashoga hawatoruhusiwa kujitambulisha katika matembezi hayo.

Katika taarifa iliyotolewa muda si mrefu na shirika la habari la CNNMoney(CNN) lililoko New York, imedai kuwa Sam Adams, ambaye ndio mmiliki wa kampuni ya kutengeneza bia ya Boston Beer Co. imebadili mawazo na kwamba haitafadhili matembezi hayo yanayotarajiwa kufanyika kesho jumapili.

SOMA ZAIDI . . .


Nalo shirika linalozalisha bia ya Heineken, ambayo pia ni maarufu nchini Tanzania na hupendwa na watu wengi ilijitoa katika kufadhili wa matembezi ya hisani ya Ney York City toka jumatatu.

“tunaamini katika usawa kwa kila mmoja” alisema msemaji wa Heineken tawi la Marekani.

Sam Adams inadaiwa kujaribu kuwabembeleza waandaaji wa matembezi ya Boston kubadilisha sharia zao na kuwaruhusu kundi la LGBT (wasagaji,  mashoga, mabasha na waliobadili jinsia) kushiriki matembezi hayo.

“tulitegemea kufikia makubaliano kuruhusu kila mtu kushiriki bila kujali hali yake kushiriki katika matembezi hayo” kampuni hiyo ilieleza katika taarifa yake, “lakini kutokana na hali ya makubaliano ilivyo sasa, hilo halitowezekana”

nao waandaaji wa matembezi hayo, The South Boston Allied War Veterans Council, walisema katika taarifa yao iliyoko kwenye tovuti yao kuwa haizuii LGBT(Lesbians, Gay Bisexual na Transsexual)  kushiriki katika matembezi hayo, bali hawaruhusiwi kuonesha au kutangaza na kubeba mabango yanayowatambulisha.

Ilieleza kuwa mashoga na wasagaji wakongwe waliotaka kushiriki maandamano kama sehemu ya kundi la wakongwe wa LGBT  bado wanaweza kushiriki kwa masharti kwamba hawatatambulika kuwa ni mashoga na kuvaa tisheti na alama zinazoonesha hivyo.

“tunawakaribisha wote kuja kusherehekea tukio hili la kihistoria, lakini ni lazma tuendelee kushinikiza sharia kwa ajili ya usalama wa kadamnasi” walisema waandaaji.

Hata Meya wa jiji anadukuduku, Meya wa jiji la New York Bill de Blasio amegomea matembezi hayo, wakati Meya wa jiji la Boston Martin Walsh ameripotiwa akijaribu kubembeleza waandaaji kubadilisha sharia kabla hajafanya maamuzi.




No comments:

Post a Comment