Monday, January 20, 2014

PICHA ZA AJALI YA KUTISHA, IMEUA 13 AKIWEPO KICHANGA NA MAMA

Watu 13 akiwemo mtoto Mchanga na mama yake wamekufa papo hapo baada ya Gari walilokuwa wakisafiria aina ya Noah kugongana uso kwa uso na Lori katika Kijiji cha Isuna Wilayani Ikungi Barabara kuu ya Singida Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishina Msaidizi Mwandamizi Geoffrey Kamwela ameeleza kuwa ajali hiyo lilitokea jana saa 2:00 asubuhi wakati Gari hiyo aina ya Noah TBUX iliyotoka Itigi kuelekea Mjini Singida, ilipogongana na Lory hilo aina ya Scania T687 AXB. Umbali wa km 60 kutoka mjini hapa.

Alibaini kuwa baada ya ajali hiyo watu 13 wakiwemo wanawake wawili wanaume 10 na mtoto mchanga walikufa hapohapo na miili ya marehemu hao kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mkoa huo.


JUU: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishina Msaidizi Geofrey Kamwela akikagua ajali iliyotokea katika Kijiji cha Isuna wilayani ikungi jana.barabara kuu ya Singida Dodoma.

CHINI: Gari aina ya NOAH T.730 BUX likiwa limeharibika vibaya baada ya kugongana na lori linaloonekana mbele yake upande wa kulia wakati gari hilo dogo likitoka Itigi kwenda Singida na lori likitoka Mwanza kwenda Dar es salaam katika Kijiji cha Isuna tarafa ya Ikungi wilayani humo.

PICHA ZAIDI…






No comments:

Post a Comment