Mama huyo, Ambra Reynolds(Juu Pichani akiwa na mwanae) alipoangalia kwa karibu akamuona Bw.Enlow akimchungulia chooni kutokea kwenye shimo hilo la maji machafu. “sio jambo la kwaida unapokuwa unajisaidia” alisema Bi. Reynolds.
“nilipiga mayowe, nikamchukua mwanangu, njiani nikambeba na mwanangu wa kiume aliyekuwa anatusubiri na kutoka nje nikiwa na wasiwasi mkubwa” alisema mama huyo.
Kundi la waokoaji walikuja na kumuibua Bw. Enlow akiwa ametapakaa vinyesi mwili mzima na kumsafisha kwa kutumia mpira wa maji.
Alikubali kosa katika mahakama ya Tulsa la kupiga chabo wiki iliyopita na kuhukumiwa.
No comments:
Post a Comment