Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati (CCM) akimkabidhi mwenyekiti wa waandishi wa habari mkoani Iringa moja ya jezi alizotoa kwa waandishi wa habari kwa ajili ya mechi mbalimbali za timu hiyo
na fredy mgunda,Iringa
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa
Ritta Kabati (CCM) ameipiga jeki timu ya wandishi wa habari mkoa wa
Iringa kwa kuwapatia jezi seti moja ,mpira na pesa taslim kiasi cha
Tsh 50O,000 ili viwasaidie katika malengo yao ya kukipiga ligi daraja
la kwanza .
Akikabidhi msaada huo kwa mwenyekiti wa chama cha
wandishi wa habari mkoa wa Iringa Frank Leonard juzi mbunge huyo
alisema kuwa yeye kama mlezi wa timu hiyo ameamu kujingiza kwa miguu
yote kuisaidi timu hiyo ambayo inaonekana kufanya vema kwenye mchezo wa
soka mkoani hapo .
Kabati alisema kuwa licha ya kuwa mpira ni
ajira pia unamsaidia mtu kuwa na afya njema itakayomsaidia kujiepusha na
magonjwa yanayoepukika ikiwemo presha .
“Niwatie moyo hichi
mulichokianzisha ni kizuri na timu yenu ina fanya vizuri na juzi tu
mumenyakua kombe la Spanest kwa kuwanyuka kitisi huu ni ushahidi tosha
mukiendelea hivi hivi mutakuja kuingia ligi daraja la kwanza na baadaye
ligi kuu .
Kabati aliwataka wadau wengine mkoa Iringa na nje
ya Iringa kuendelea kujitolea kuisaidia timu hiyo ya
wanahabari ili iendele kufanya vema ndani na nje ya mkoa wa iringa
Akipokea
vifaa hivyo mwenyekiti wa wanahabari mkoa wa Iringa Frank Leonard
alimshukuru mbunge huyo kwa vifaa na fedha alizotoa huku akimuahidi
mbunge huyo kuwa timu hiyo itakipiga na timu mbalimbali ikiwemo timu ya
bunge la jamuhuri wa muungano wa Tanzania
Frank alisema kuwa
timu hiyo imekuwa ikifanya vema kutokana na kuwa na wandishi wazuri
vijana waliona ari ya kusakata kambumbi hivyo ni vema timu ya bunge
kujipanga kisawasa kwani hawata toka salama pindi watakapokipiga nao
mjini dodoma
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati (CCM) ameipiga jeki timu ya wandishi wa habari mkoa wa Iringa kwa kuwapatia jezi seti moja ,mpira na pesa taslim kiasi cha Tsh 50O,000 ili viwasaidie katika malengo yao ya kukipiga ligi daraja la kwanza .
No comments:
Post a Comment