Monday, June 16, 2014

BREAKING NEWS: 48 WAUAWA KWA BOMU KENYA, AL-SHABAB YAHUSIKA

Kundi la wapiganaji wa Al Shabaab nchini Somalia, limekiri kufanya mashambulizi katika eneo la Mpeketoni karibu na Lamu, Pwani ya Kenya. Mashambulizi hayo yalisababisha vifo vya watu 49.

Huku wakikiri shambulizi hilo wametoa onyo kwa watalii kukoma kuja Kenya. Taarifa ya kundi hilo ilisema kuwa shambulizi hilo lilikuwa la kulipiza kisasi dhidi ya serikali ya Kenya kwa kufanya msako dhidi ya waisilamu kwa njia ya kuwafunga kiholela na kuwaua wahubiri wa kiisilamu.

Baadhi ya walioshuhudia mashambulizi hayo wamearifu BBC kuwa wameona maiti kadhaa na majeruhi wengi japo Polisi hawajathibitisha ni watu wangapi wameuawa.






No comments:

Post a Comment