ATEKWA, ATISHIWA KISU, KISHA ABAKWA BILA KINGA
Mwandishi Wetu
Polisi inadaiwa kuchunguza tuhuma nzito ya uvamizi na ubakaji usio wa
kawaida kwa kijana wa miaka 30 linalodaiwa kutokea hivi karibuni ambapo
wanawake wawili wanadaiwa kuhusika.
Tukio hilo lililotokea ijumaa iliyopita linadaiwa kuwa ni moja ya
matukio hatari ambayo yamekuwa yakitokea nchini, na kuwaacha polisi kutojua la
kufanya.
Muathirika mmoja wapo, kwa mujibu wa polisi ni mtembea kwa miguu mmoja
ambaye alikuwa anaelekea jijini Harare na kulazimika kuomba lifti akiwa katika
kituo cha mafuta cha AMTEC karibu na barabara ya Lobengula, jijini.
Ilikuwa ni baada ya saa 3 jioni, tarehe 29 aprili, muhusika alifuatwa
na mwanamke aliyemuelezea kuwa na umri unaokisiwa kuwa miaka 40 ambaye
alimwambia katika maongezi yao kuwa nay eye anaelekea Harare.
“dereva akasema anauwezo wa kubeba abiria wengine wawili tu kuelekea
Harare. Mlalamikaji akaingia nyuma na mwanamke akaingia kiti cha mbele” alidai
msemaji wa polisi Inspector Patrick Chademana.
Polisi wanadai kuwa kilometa chache baadae nje ya Gweru, dereva
aliwasha endiketa na kupunguza mwendo kuashiria kusihiwa mafuta na kuingia
kituo cha mafuta cha Consilla.
“ghafla, mwanaume aliyekaa kiti cha nyuma na mlalamikaji akatoa
kitambaa kinachodaiwa kuwa na dawa ya usingizi na kumziba mlalamikaji mdomo na
pua na kisha upoteza fahamu” inspekta Chademana aliongeza
alipozinduka alijikuta ndani ya chumba chenye zulia la rangi ya brown
na sofa la ngozi. Mwanaume aliyekuwa abiria akiwa ameshika kisu, polisi
walieleza.
“mlalamikaji wanawake wale wawili walivua nguo zote na kubakia uchi wa
mnyama na kumfuata. Akalazimishwa kufanya ngono zembe na wanawake hao wawili
huku akiwa ameshikiwa kisu,” alisema Chademana.
Baada
ya shambulio hilo, polisi wanadai mlalamikaji alizibwa tena mdomo na dawa mpaka
akapoteza fahamu na alipozinduka mapema jumamosi asubuhi alijikuta katika pori
karibu na kona ya St.Patrick karibu na njia kuu ya kuelekea Harare kutoka
Gweru.
Pamoja
na tukio hilo pia alporwa pesa zote, simu yake ya mkononi, na mali alizokuwa
nazo zenye thamani isiyopungua laki mbili na nusu.
Chademana aliongeza: “tuna toa rai kwa watu wote wenye kujua lolote
kuhusiana na watuhumiwa hao atoe taarifa katika kituo chochote cha polisi
kilicho karibu”
“pia tunatoa taadhari kwa wasafiri wote kuacha
kuingia kwenye magari wasiyoyatambua ili kupunguza uwezekano wa matukio ya
ubakaji”
No comments:
Post a Comment