Monday, June 24, 2013

BREAKING NEWS: HALI YA MANDELA IMEZIDI KUWA MBAYA ZAIDI KATIKA SAA 24 ZILIZOPITA




Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia mapema leo, afya ya aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Mzee Nelson ‘Madiba’ Mandela imezidi kuwa mbaya. Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amedhibitisha hayo alipomtembelea hospitali jana na kuzungumza na mke wa Mzee Mandela, pamoja na timu ya madaktari.
SOMA ZAIDI...

Rais Zuma alieleza katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa ‘Madaktari wanafanya kila kinachowezekana kumsaidia kurudi katika hali yake ya kawaida’

Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini Nelson Mandela mwenye miaka 94, alipelekwa hospitali huko Pretoria mwanzo wa mwezi juni ikiwa ni mara ya tatu mwaka huu, Mandela amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kupumua

Zuma alidai madaktari wamemweleza kuwa hali ya Mandela inazidi kuwa mbaya sana na imekuwa hiyvo katika muda wa masaa 24 yaliyopita.

“Madaktari wanapambana kujitahidi kurudisha hali yake kuwa kawaida na yuko chini ya uangalizi mzuri na katika mazingira mazuri. Madiba yuko katika mikono mizuri” alieleza Rais Zuma, kwa kutumia jina la kikabila la Mandela ambalo ndio maarufu sana Afrika Kusini.

Zuma akifuatana na kiongozi wa chama kinachotawala cha African National Congress (ANC), Cyril Ramaphosa wameomba maombi zaidi kwa Bw. Mandela na timu yake ya madaktari.

Msemaji wa Bw.Zuma, Mac Maharaj aliliambia shirika la habari la BBC kwamba "madaktari wametumia neno ‘hali mbaya sana’ inatosha kutuweka roho juu kuhusiana na hali ya Madiba".


No comments:

Post a Comment