Tuesday, June 25, 2013

BREAKING NEWS: BERLUSCONI NDANI KWA NGONO




Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Italia, Silvio Berlusconi amehukumiwa kwenda jela miaka 7 na kuzuiwa kuingia katika ofisi zozote za serekali baada ya kupatikana na kosa la kufanya ngono na watoto wadogo.


Kwa mujibu wa BBC, Berlusconi anaendelea kuwa huru baada ya kukata rufaa dhidi ya mahakama ya Milan.

Washtakiwa wote wawili mmoja akiwa ni tajiri wa vyombo vya habari, Bw Berlusconi na msichana wa Moroco, Karima El Mahroug wamekataa kuwa waliwahi kukutana kingono.

“Ntapinga hukumu yangu kwasababu sina kosa lolote” alieleza Bw. Berlusconi baada ya hukumu kutolewa

Lakni Bw. Berlusconi bado amezungukwa na kesi nyingie ambapo mwezi oktoba 2012 alihukumiwa kwenda jela kwa miaka 4 kwa kosa la kukwepa kodi, ambapo pia alikata rufaa.


No comments:

Post a Comment